• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA wa mahindi Namtumbo wataja changamoto ya kukosa elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo

Imewekwa kuanzia tarehe: August 19th, 2024

WAKULIMA wa mahindi wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma,wameitaja changamoto ya  kukosa elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo ikiwemo mbegu bora na mbolea kutoka kwa maafisa ugani hali iliyosababisha kuzalisha mazao yasiyo kidhi viwango kulingana na mahitaji ya soko la Serikali.


Wamesema hayo,wakati wa kazi ya uuzaji na ununuzi wa zao la mahindi unaofanywa na Serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya chakula(NFRA) katika kituo cha Rwinga wilayani humo.


Faraji Abed amesema,wakulima wako tayari kuzalisha,lakini elimu ya uzalishaji wa mazao bora ni kikwazo kikubwa ambacho kimesababisha baadhi ya wakulima kukata tamaa na kushindwa kuendelea na uzalishaji mashambani.


“tunaiomba Serikali  maafisa ugani tuwe nao mashambani ili sisi wakulima tusiendelee kupata hasara ya kuchagua mazao yetu pindi tunapofikisha sokoni,kama maafisa kilimo tungekuwa nao kuanzia wakati wa maandalizi ya shamba hadi msimu wa mavuno basi tusingepata hasara kubwa namna hii”alisema Abed.


Amesema,wakulima wana mwamko mkubwa wa kulima,lakini changamoto kubwa ni kupata mazao yenye sifa ya kufikisha sokoni yakiwa na ubora wake ule ule hali inayopelekea wakulima kuamini kama kilimo ni kazi inayoweza kuwaletea manufaa katika maisha yao.


Ameishukuru serikali kwa kununua mahindi kwa bei ya Shilingi 700 kwa kilo moja ikilinganisha na bei ya Shilingi 350 ya wafanyabiashara wa mitaani ambayo haikidhi mahitaji na gharama za uzalishaji.

Mkazi wa kijiji cha Rwinga Salum Idd,ameishukuru Serikali kuwaletea kituo cha ununuzi wa mahindi,lakini changamoto kubwa wanatumia muda mrefu kusafisha mahindi kabla ya kupokelewa.

Amesema,hali hiyo imetokana na uzembe wa maafisa ugani ambao hawakwenda mashambani kuwapa elimu ya kilimo cha kisasa hasa katika matumizi ya mbegu bora na mbolea.



Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.