• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAKULIMA wa ufuta Tunduru waingiza bilioni 17

Imewekwa kuanzia tarehe: August 2nd, 2023

wakulima wa ufuta Wilayani Tunduru mkoani Ruvuma ,wamefanikiwa kuvuka lengo la uzalishaji baada ya kuvuna kilo milioni 4,800,997 sawa na ongezeko la asilimia 88.36 zilizowaingizia Sh.bilioni 17.688 ikilinganisha na malengo ya kuzalisha kilo milioni 3,822,561 katika msimu wa kilimo 2023/2024.

Wakulima hao wameuza ufuta  kupitia vyama vya msingi vya ushirika(Amcos),katika minada saba iliyofanyika kwa mfumo wa stakabadhi ghalani na ongezeko hilo la uzalishaji ni kubwa ikilinganisha na msimu 2022/2023 ambapo walizalisha takribani kilo milioni 2,548,815 zenye thamani ya Sh.bilioni 7.7.

Mkuu wa wilaya hiyo Julius Mtatiro alisema,ongezeko hilo limewezesha wakulima kupata fedha nyingi,hivyo kusaidia kuongeza mzunguko wa uchumi kwa wananchi wa wilaya hiyo kwa zaidi ya asilimia 43.59  katika kipindi cha mwaka mmoja kupitia zao la ufuta.

“kwa ujumla tumepata mafanikio makubwa kwenye zao la ufuta,kama nilivyosema  uzalishaji umeongezeka kwa asilimia 88.36 na kwenye uchumi bei zimeimarika sana,kwa hiyo ukichanganya na ongezeko la uzalishaji utaona kwamba tija iliyoongezeka katika uchumi ni zaidi ya asilimia 43.59”alisema Mtatiro.

Amewaomba wanunuzi,kwenda wilayani humo na kuhakikisha wanashiriki kikamiifu katika ununuzi wa zao hilo ili kuimarisha bei kwa kuwa wilaya hiyo imejipanga kuongeza uzalishaji kufikia kilo milioni 12 katika msimu ujao.

Alisema,suala la kilimo cha ufuta litakuwa ajenda ya kwanza kwenye mikutano yote na wananchi kwa kuwa mpango wa serikali ya wilaya ni kuhakikisha kila mkulima anakuwa na shamba la ufuta.

Mtatiro alisema,hatua hiyo itasaidia sana kupunguza malalamiko na manung’uniko kila inapofika msimu wa  kuuza korosho,kwa sababu hawapati fedha  za kutosha kutokana na kushuka kwa bei ya zao hilo katika soko la Dunia.

Alisema,wakati  Rais Dkt Suluhu Hassan akiendelea kuleta viuatilifu vya bure kwa ajili ya zao la korosho ni vyema wakulima kuwa na mashamba ya mazao mengine ikiwemo ufuta ili kuwaongezea kipato  kwenye familia zao.

Kwa upande wake Meneja wa Chama kikuu cha Ushirika(Tamcu)Iman Kalembo alisema,bei ya ufuta  imeongezeka kutoka wastani wa Sh.3,019.80 kwa msimu 2022/2023 hadi Sh.3,661.72 msimu wa 2023/2024 tangu ulipoanza mnada wa kwanza.

Aliongeza kuwa,katika msimu wa mwaka huu wadau wamenufaika kutokana na matumizi ya mfumo wa stakabadhi ghalani katika mauzo ya ufuta na wakulima wameendelea kuona uimarikaji wa bei ambao ni muhimu kwa wakulima na serikali kupata takwimu  sahihi za mazao yanayozalishwa na ukusanyaji wa mapato yake.

Kalembo,amemshukuru Mkuu wa wilaya kwa kusimamia vema na kutoa ushauri wa mara kwa mara  katika uendelezaji wa shughuli za ushirika ambapo amemuomba kuwasimamia na kuwaongoza katika msimu mpya wa kilimo 2023/2024.

Amewahimiza wakulima,kuongeza jitihada za uzalishaji wa zao hilo lililoanza kuonyesha mafanikio makubwa kwao binafsi,vyama vya msingi na serikali kwa ujumla.

Naye makamu mwenyekiti wa Tamcu Pino Chikojola,amewashukuru wakulima,viongozi wa vyama vya msingi(Amcos) na Chama kikuu cha Ushirika kwa kusimamia suala la mauzo ya ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.