• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WALIMU Mbinga washiriki bonanza

Imewekwa kuanzia tarehe: November 9th, 2022

WALIMU wa shule za msingi na Sekondari katika Halmashauri ya wilaya Mbinga,wamefanya mabonanza ya michezo  ili kuimarisha afya zao,na kupata mbinu zitakazo saidia wanafunzi wao kufanya vizuri wanaposhiriki michezo mbalimbali.

Mabonanza hayo yanayofahamika  Sabina Lipukila KUT CWT Cup 2022-2023,yamefanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari Kihamili kata ya Kigonsera wilayani Mbinga.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo mdhamini Mkuu wa michezo hiyo Sabina Lipukila alisema,michezo hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuwapa mbinu mbalimbali walimu katika kufundisha michezo wanafunzi wa mkoa wa Ruvuma na kuondokana na kufanya vibaya katika mashindano ya  shule za msingi(Umitashumta) na Sekondari(Umisseta).

Aidha alisema,kupitia mabonanza hayo walimu watakutana,kufahamiana na kuwa na hali  ya kushiriki katika michezo ambayo itaongeza hisia ya mafanikio na uzalendo  katika majukumu yao ya kila siku.

Amewapongeza walimu wa Halmashauri  ya  wilaya Mbinga, kwa kushiriki bonanza hilo ambalo linakwenda kusaidia kuibua vipaji na hatimaye kupata wanamichezo bora watakao iwakilisha wilaya ya Mbinga na mkoa wa Ruvuma kwenye mashindano mbalimbali.

Lipukila  ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji wa Chama cha Walimu Tanzania(CWT) kutoka mkoa wa Ruvuma alisema, CWT kinatambua sana umuhimu wa michezo ambapo kwa nyakati tofauti walimu wamepata nafasi ya kushiriki michezo ndani na nje ya nchi.

Amehaidi kuendelea kudhamini michezo kwa wanafunzi na walimu wa shule za msingi na sekondari ili na kuwaomba wadau wengine kusaidia  kudhamini katika sekta ya michezo ambayo imeanza kuleta manufaa makubwa kwa wana michezo na Taifa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu wilaya ya Mbinga Ahmad Mwalimu amesema, katika kuunga mkono michezo Chama hicho kitatoa seti moja  ya jezi kwa kila timu.

Baadhi ya walimu,wamempongeza mdhamini wa bonanza hilo Sabina Lipukila kwa kuamua kuanzisha mabonanza ya michezo ambayo yatasaidia kuibua vipaji vingi na kuimarisha afya za walimu.

Katika Bonanza hilo Timu ya walimu ya mpira wa miguu kutoka Bonde la Hagati imeibuka mshindi baada ya kuifunga Timu ya kanda ya Kigonsera kwa Penati 5-3 huku timu ya Netball  wanawake  ya Walimu ikiifunga timu ya Halmashauri  ya wilaya Mbinga.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.