• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WALIMU 56 Ruvuma wapatiwa mafunzo ya elimu jumuishi

Imewekwa kuanzia tarehe: March 11th, 2022

MAAFISA Elimu na Walimu wa Elimu Maalumu 56 wamepatiwa mafunzo  ya Elimu Jumuishi kwa muda wa siku tatu mkoani  Ruvuma.

Akifunga mafunzo hayo  Mkurugenzi wa Elimu Maalumu TAMISEMI Juliasi Migeha amesema Mafunzo hayo yanafanyika katika Mikoa ya Morogoro,Iringa ,Mtwara na Ruvuma ili kuwezesha maafisa na walimu wa elimu maalum kufanya kazi kwa viwango.

Mkurugenzi huyo amezitaja changamoto za watoto wenye mahitaji maalumu kuwa ni kutengwa na kuwaweka katika madarasa maalum wakati wanafundishwa ikiwa wakitoka.

Migeha amesema watoto hao wanapaswa kukua na kujifunza kwa pamoja kupitia  walimu jumuishi wa kuwafundisha na kuwawekea mikakati ya kuwawezesha kufanya vizuri katika masomo yao.

Hata hivyo Migeha ametoa rai kwa walimu hao kuwa na Mkakati wa utekelezaji wa Elimu Jumuishi katika mfumo mzuri na kwamba kila Halmashauri iweze kutambua idadi ya watoto wenye uhitaji maalumu ili wanapoanza masomo yao wasipate changamoto za kukosa kujiunga na Masomo kwa wakati.

“Changamoto ya Elimu Jumuishi ni miundombinu kuto kuwa rafiki,vifaa,walimu wenye uwezo wa kufundisha na kuwafanya wanafunzi  kuelewe “,alisema.

Kwa pande wake Katibu Tawala Msaidizi Elimu Mkoa wa Ruvuma Imanuel Kisongo  kupitia mafunzo hayo amewaasa Maafisa na walimu wa elimu maalum kutoa matunda kupitia  mafunzo ya elimu jumuishi.

Kisongo ameahidi kutembelea shule zote za elimu maalum katika Mkoa huo kujua changamoto zake na amewaomba  maafisa na walimu wa elimu maalum kujituma kutokana na kazi ambayo wamepewa pamoja na kutoa Taarifa kwa wakati  ili kuhakikisha wanafunzi wanapata Elimu iliyo sahihi.

Mmoja kati ya washiriki kutoka katika Shule ya St Vicent Ruhuwiko Manispaa ya Songea  Sister Agneta Mlelwa amesema kupitia mafunzo ya   Elimu Jumuishi  yatawawezesha kuwafundisha wanafunzi wa aina zote wenye ulemavu na wasiokuwa na ulemavu.

Mlelwa ameiomba Serikali kutoa mafunzo hayo mara kwa mara sanjari na  vifaa vya kufundishia ili kutoa elimu bora.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kitengo cha Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma

Machi 10,2022.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.