• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Nyasa kunufaika na mradi wa maji wa milioni 60

Imewekwa kuanzia tarehe: February 28th, 2025

Wananchi wa Kijiji cha Kimbanga, Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, wamepata afueni baada ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutoa Shilingi milioni 60 kwa ajili ya uchimbaji wa kisima cha maji safi na salama. Hatua hii inalenga kumaliza tatizo la muda mrefu la upatikanaji wa maji katika kijiji hicho.

Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa, Athuman Chola, amesema kuwa Shilingi milioni 300 zimetengwa kwa uchimbaji wa visima vitano wilayani humo, ambapo Kimbanga ni miongoni mwa wanufaika wa mradi huu.

“Kwa sasa, uchimbaji wa kisima umekamilika na ujenzi wa kioski cha kuchotea maji umefikia zaidi ya asilimia 40. Kazi zinazoendelea ni usambazaji wa mabomba, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji, ufungaji wa mashine za kusukuma maji, na uwekaji wa umeme jua ili kuboresha upatikanaji wa huduma hiyo.”,alisema 

Hata hivyo amesema katika vijiji vinne kati ya vitano vilivyopangwa kunufaika na mradi huo, uchimbaji wa visima haujafanikiwa kupata maji chini ya ardhi. Chola amesema RUWASA inatumia mbinu mbadala kama kuboresha chemchem zilizopo na kuanzisha miradi ya mserereko kwa kutumia maji kutoka milimani.

Baadhi ya wakazi wa Kimbanga wameeleza furaha yao kwa hatua hii ya serikali. Adelius Mwingira amesema kuwa mradi wa kisima utawaondolea adha ya kutumia maji yasiyo salama kutoka visima vya asili, huku Bonus Kapinga akisema kuwa kijiji hicho hakijawahi kuwa na maji ya bomba kwa zaidi ya miaka 50.

Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maji vijijini, ikilenga kupunguza na hatimaye kumaliza kabisa tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.