• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Nyasa waishukuru serikali kwa matengenezo ya barabara zilizojifunga

Imewekwa kuanzia tarehe: March 17th, 2023

BAADHI ya wananchi wa kata ya Ngumbo wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wameishukuru serikali kwa kuifungua barabara ya Hinga-Litolomelo na Ngumbo-Litoho zinazounganisha wilaya ya Mbinga na Nyasa na maeneo mengine mkoani humo ambazo awali zilikuwa hazipitiki kirahisi.

Wamesema,kufunguka kwa barabara hizo  katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kumerahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa mbalimbali za kilimo na  samaki na kumaliza  kero ya usafiri iliyokuwepo kwa muda mrefu.

Wamesema,changamoto kubwa  kwa wananchi wa kata ya Ngumbo ilikuwa barabara za kuunganisha kata hiyo na maeneo mengine,lakini sasa kero hiyo haipo baada serikali  ya awamu  ya sita  kupitia wakala wa barabara za vijijini na mijini(Tarura) kutoboa na kufanya matengenezo ya  makubwa ya barabara hizo kwa kiwango cha changarawe.

John Mkomola mkazi wa kijiji cha Ngumbo amesema,serikali  ya awamu ya sita imewatendea haki kwa kuboresha huduma za kijamii ikiwemo  barabara zinazokwenda kuchochea na kuharakisha shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Alisema,baadhi ya maeneo katika wilaya ya Nyasa hayakuweza kufikiwa na baadhi ya huduma  za kijamii kwa kukosa barabara, hivyo kusababisha maisha ya wananchi kuwa magumu licha ya wilaya hiyo kuwa na rasimilia kubwa ya ardhi na ziwa Nyasa lenye samaki wengi.

Adolat Kapinga mkazi wa kijiji cha Lugali amesema,awali barabara ya Ngumbo-Litoho inayounganisha wilaya ya Nyasa na Mbinga haikuweza kupitika kwa urahisi kutokana na ubovu hasa mashimo makubwa na wakati wa masika kuwa na utelezi na hivyo kusababisha magari kukwama na hata kulala barabarani.

Aidha ameeleza kuwa,katika kipindi cha miaka miwili ya utawala wa Rais Samia barabara hiyo imeimarika na kurahisisha shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa wilaya hizo mbili ambao sasa wanatembea kifua mbele na kufaidi matunda ya serikali yao.


Kapinga ameipongeza wakala wa barabara za vijijini na mijini Tarura wilayani Nyasa kufanya matengenezo ya barabara na kurudisha mawasiliano katika maeneo mengi ya wilaya hiyo ambayo hapo awali hayakufikika kwa urahisi.

“miaka miwili ya Rais Dkt Samia  tunaona mabadiliko mengi na makubwa katika wilaya yetu,barabara hii haikuweza kupitika kirahisi, lakini sasa serikali imefanikiwa kuunganisha mawasiliano kati ya wilaya ya Mbinga na Nyasa”amesema Kapinga.

Kwa upande wake meneja wa Tarura wilaya ya Nyasa Thomas Kitusi alisema,barabara ya Hinga-Litolomelo ni moja ya barabara saba zilizotengenezwa kwa fedha za tozo kwa mwaka wa fedha 2022/2023 yenye urefu kilomita 11.7 kwa gharama ya shilingi milioni 174 kwa kiwango cha changarawe.

Kitusi alitaja barabara nyingine ni Ngumbo –Litoho yenye urefu wa km 6.59 ambayo ilitengewa jumla ya shilingi milioni 84 kwa ajili ya kufanya matengenezo kwa kiwango cha chanagarawe.

Alisema,katika kipindi cha miaka miwili ya utawala wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kumekuwa na mabadiliko makubwa kwenye sekta ya barabara ikilinganisha na miaka ya nyuma. na ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kutenga fedha nyingi ambazo zimewezesha Tarura kufanya matengenezo ya barabara nyingi za vijijini zilizoleta mabadiliko makubwa.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.