• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Ruvuma wamshukuru Rais kwa bandari ya Ndumbi

Imewekwa kuanzia tarehe: March 19th, 2024

Na Albano Midelo,Mbambabay

WANANCHI wa Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma wamemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutenga fedha kiasi cha shilingi bilioni 12.2 kwa ajili ya ujenzi wa bandari mpya ya Ndumbi ziwa Nyasa.

Mbunge wa Jimbo la Nyasa Mhandisi Stella Manyanya akizungumza mjini Mbambabay amesema ujenzi wa bandari hiyo umekamilika kwa asilimia 100 na kwamba serikali pia imetenga shilingi bilioni 70 kwa ajili ya ujenzi wa bandari ya kisasa ya Mbambabay wilayani Nyasa.

“Kwa namna ya pekee tunamshukuru Jemedari wetu Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa mabilioni ya fedha kutekeleza miradi mikubwa ya bandari katika wilaya ya Nyasa’’,alisisitiza.

Manyanya amesema  serikali inaendelea kuifungua wilaya ya Nyasa katika sekta ya usafiri na usafirishaji hivyo kutoa fursa kwa wawekezaji kufika kuwekeza katika wilaya hiyo yenye fursa nyingi za kiuchumi na uwekezaji,

Meneja wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari za Ziwa Nyasa Manga Gassaya  akizungumzia utekelezaji wa ujenzi wa bandari ya Ndumbi,ameitaja miundombinu iliyojengwa katika bandari ya Ndumbi kuwa ni ujenzi wa Gati lenye urefu wa mita 160 kwenda ziwani na sehemu ya kupokea lango la meli yenye urefu wa mita 40.

Miundombinu mingine iliyojengwa katika bandari ya Ndumbi ameitaja kuwa ni ghala la kuhifadhia mizigo lenye mita za ukubwa 1,020,eneo la sakafu ngumu kwa ajili ya kuhifadhia mizigo isiyoathiriwa na mvua lenye mita za ukubwa 9030 na jengo la kupumzikia abiria lenye uwezo wa kuhudumia abiria 70,000 kwa mwaka.

Gassaya amesema bandari ya Ndumbi baada ya kukamilika Desemba 2022 imeongeza uwezo wa kuhudumia shehena kwa bandari za ziwa Nyasa  kwa mwaka kutoka tani 76,000 hadi kufikia tani 110,000.

 Amesema bandari hiyo pia imeongeza uwezo wa kuhudumia abiria kutoka abiria 56,000 kwa mwaka hadi kufikia abiria 126,000.

Meneja huyo wa bandari za ziwa Nyasa amesema  serikali pia imeanza kutekeleza ujenzi wa bandari mpya ya kisasa ya Mbambabay lengo likiwa ni kuimarisha ushoroba wa maendeleo ya Mtwara ambayo ni njia fupi na rahisi kuhudumia mizigo ya Malawi kutokea bandari ya Mtwara.

“Serikali ya Awamu ya Sita imetenga shilingi bilioni 70  kuanza kutekeleza mradi huo ambao unatarajia kukamilika ndani ya miezi 24,ujenzi wa bandari ya Mbambabay ukikamilika utaongeza uwezo wa kuhudumia shehena ya mizigo katika bandari  kutoka tani 110,000 hadi kufikia tani 550,000 kwa mwaka’’,alisema.

Hata hivyo amesema baada ya ujenzi wa bandari mpya ya Mbambabay kukamilika,makao makuu ya bandari za ziwa Nyasa yatahamia Mbambabay wilayani Nyasa mkoani Ruvuma kutoka bandari ya Kiwira iliyopo wilayani Kyela mkoani Mbeya.

Amesema kutokana na maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali katika bandari za ziwa Nyasa,katika kipindi cha miezi  sita ya mwaka 2023/2024 bandari zimehudumia jumla ya abiria 7,358 na mizigo tani 1,828.6.

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inasimamia bandari 15 katika ziwa Nyasa  zilizopo katika mikoa ya Ruvuma,Mbeya na Njombe.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.