• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Tunduru waishukuru TARURA kwa ujenzi wa daraja

Imewekwa kuanzia tarehe: August 12th, 2023

WAKAZI wa kijiji cha Mandepwende na kitongoji cha Zanzibar kata ya Lwinga wilaya ya Namtumbo,wameishukuru serikali kupitia wakala wa Barabara za mijini na vijijini(Tarura) wilayani humo kukamilisha ujenzi wa daraja katika mto  Kotoko ambalo limechochea uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Wamesema,kukamilika kwa daraja hilo na ufunguzi wa Barabara mpya inayounganisha kijiji hicho na maeneo ya uzalishaji,hivyo kurahisisha usafirishaji wa mazao kutoka shambani kwenda sokoni na kufanya shughuli mbalimbali za kujiongezea kipato.

Hasibuna Lutumbo makzi wa Mandepwende alisema,kabla ya kujengwa daraja la Kotoko changamoto kubwa ilikuwa namna ya kupita katika eneo hilo kwenda upande wa pili kwani wakati wa masika ujaa maji na hivyo kuwa vigumu kwenda maeneo mengine kufuata huduma muhimu za kijamii.

Aidha alisema,kukosekana kwa  Barabara ya uhakika kwa muda mrefu,kumechangia kuongezeka kwa  umaskini miongoni mwao licha ya jitihada kubwa wanazofanya  za uzalishaji.

“tunaishukuru sana serikali yetu ya awamu ya sita kupitia Tarura kukamilisha ujenzi wa daraja,awali eneo hili halikuweza kupitika kirahisi kutokana na kujaa maji,tunawapongeza sana wataalam wetu kutoka Tarura kukamilisha kazi kwa haraka na  kwa viwango”alisema.

Mwajuma Athuman alisema,awali akina mama wajawazito waliteseka pindi wanapotaka kwenda kliniki kwani walilazima kuwabeba wajawazito kwenye machela jambo lililopelekea baadhi yao kupoteza maisha kabla ya kufikishwa kwenye vituo vya kutolea huduma.

Saidi Mtawanyi,ameiomba serikali kuu kuiongezea Tarura fedha za kujenga kipande cha Barabara kilichobaki ili kurahisisha mawasiliano kati ya Kitongoji maarufu cha Zanzibar chenye idadi kubwa ya watu na kijiji cha mama cha Mandepwende.

Alisema,hatua hiyo itasaidia kuunganisha mawasiliano ya barabara kati yam kitongoji hicho na maeneo mengine ya wilaya ya Namtumbo ambayo ni maarufu kwa uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Kwa upande wake Meneja wa TARURA wilayani Namtumbo Mhandisi Fabian Lugalaba alisema,ujenzi wa daraja hilo umegharimu kiasi cha Sh.milioni 50 na ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 98 na limeanza kupitika.Alisema,daraja hilo ni sehemu ya ujenzi wa mradi wa barabara ya Lwinga,Mandepwende Msengenengem na ufunguzi wa barabara mpya ya Mfwate hadi Msengenengem yenye urefu   wa kilomita 41  ambayo inayohusisha na ujenzi wa box kalavati 2 ambapo gharama za mradi wote ni Sh.milioni 638.Alisema,kwa sasa ufunguzi wa barabara yote kilomita 41 umekamilika na kazi inayoendelea na ujenzi wa box kalavati mbili na mradi unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu ili kuruhusu shughuli na maisha ya wananchi kuendelea kama kawaida.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.