• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI Tunduru wapo tayari kuhhesabiwa

Imewekwa kuanzia tarehe: August 22nd, 2022

ZIKIWA zimebaki saa chache kufanyika kwa zoezi la sensa ya  watu na makazi,Serikali wilayani Tunduru imekamilisha kwa asilimia mia moja maandalizi yote muhimu ya zoezi hilo  linalotarajiwa kufanyika Agosti 23 mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa wilaya hiyo Julius Mtatiro, alipokuwa akitoa taarifa ya maandalizi ya sensa kwa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ambaye yuko kwenye ziara ya kuhamasisha wananchi kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi katika wilaya zote za mkoa huo.

Kwa mujibu wa Mkuu wa wilaya, jumla ya makarani 1,392 wasimamizi wa tehema 39 na wasimamizi wa mahudhui 141 wamepata mafunzo ya siku kumi na tisa kutoka kwa wakufunzi 53 waliopata mafunzo ngazi ya mkoa.

Alisema,wakati wa maandalizi ya zoezi hilo makarani hao wamepata mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo ikiwamo namna ya kuuliza maswali na kupata taarifa muhimu kutoka kwa wananchi ambao wako tayari kushiriki zoezi hilo ambalo kwa mara ya mwisho limefanyika hapa nchini mwaka 2012.

Mratibu wa sensa mkoa wa Ruvuma Mwantumu Athuman alieleza kuwa,makarani wa sensa watapita kwenye makazi ya wananchi kwa ajili ya kupata taarifa  juu ya kaya, hali ya ndoa,walemavu,watoto,elimu na mambo mengine muhimu na kila mwananchi atapaswa kuhesabiwa mara moja tu na sio vinginevyo.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas,amewaomba watendaji na watumishi wa serikali kutumia siku chache zilizobaki kwenda kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kushiriki  sensa ya watu na makazi.

Alisema,katika sensa  ya mwaka 2012 wilaya ya Tunduru haikufanya vizuri kutokana na baadhi ya wananchi kukataa kuhesabiwa kutokana na upotoshaji wa baadhi ya watu kuingiza zoezi hilo na imani ya dini.

Alisema,matokeo yake serikali ilishindwa kupata idadi kamili ya wananchi wake na hivyo kushindwa  takwimu na taarifa sahihi ambazo zingesaidia wilaya hiyo kuwa na  sifa ya kupata Halmashauri  ya pili.

“kama wananchi hawatajitokeza kwa wingi na kutoa taarifa sahihi kwa makarani wa sensa,basi itakuwa vigumu kwa serikali kufikiria kuwapa Halmashauri nyingine”alisema Kanali Laban.

Aidha,amewaagiza viongozi wa wilaya hiyo  kwenda kusimamia na kuratibu vizuri mchakato wa kusajili majina ya wakulima wenye sifa ya kupata mbolea ya ruzuku na  kuonya kuwa,mwananchi au kiongozi atakayekwenda kinyume na zoezi hilo  atachukuliwa hatua.

“ni marufuku kwa mwananchi au kiongozi kuuza mbolea hiyo,nawaomba sana endeleeni kuhamasisha wakulima kujiandikisha kwa ajili ya kupata mbolea ya ruzuku ili iweze kuongeza uzalishaji  mashambani”alisisitiza Kanali Laban.

Alisema,zoezi hilo halihitaji kutoa fedha wala rushwa ya aina yoyote ni zoezi la bure na kuwaomba viongozi wa ngazi mbalimbali katika wilaya hiyo kwenda kusimamia utekelezaji wake.

Kanali Laban alisema kuwa,kama  zoezi hilo litasimamiwa vizuri mkoa wa Ruvuma utaendelea kuwa wa kwanza katika uzalishaji na hata kaya maskini zinazopokea ruzuku kupitia Tasaf zitapungua.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Tunduru Said Bwanali alisema,wananchi na watumishi wa wilaya hiyo hawana shaka juu ya utendaji wake.

Bwanali,amempongeza Kanali Labani kwa kuteuliwa kuwa Mkuu wa mkoa  wa Ruvuma, ambapo amehaidi  kuwa Halmashauri  hiyo itampa ushirikiano mkubwa katika kutekeleza majukumu yake ikiwamo kushiriki na kusimamia vyema zoezi la sensa ya watu na makazi

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.