• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI wa Litumbandyosi kuwashiwa umeme

Imewekwa kuanzia tarehe: October 8th, 2023

Wananchi wa Kijiji cha Litumbandyosi kilichopo Kata ya Litumbandyosi, Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kupata umeme kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kijijini hapo, ambapo Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga anatarajia kuwasha umeme kesho Oktoba 8, 2023.

Pongezi hizo zimetolewa leo Oktoba 7, 2023  wakati wa mahojiano maalum na wananchi wa kijijini hicho, namna walivyopokea ujio wa umeme, changamoto walizokuwa wakipitia kutokana na kukosa umeme pamoja na fursa watakazoenda kuziibua kutokana na ujio wa umeme wa REA.

“Tunampongeza Mhe. Rais kwa kutuletea umeme, tumekuwa tukiona umeme kwenye miji mikubwa, hatukuwahi kufikiria siku moja na sisi kijiji chetu kitakuja kuwa na umeme. Tunashukuru kesho Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga anatuwashia umeme hapa kijijini,” amesema Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Litumbandyosi, Mikael Mwingira.

Ameendelea kusema kuwa, umeme huo utafungua fursa mbalimbali kijijini hapo ikiwemo uanzishwaji wa mashine za kusaga za umeme, tofauti na mashine za mafuta ambazo wamekuwa wakizitumia. Vilevile amesema kuwa, ujio wa umeme kijijini hapo utawezesha uanzishwaji wa mashine za kubangulia korosho, ambazo zilikuwa hazipo kijijini hapo, kutokana na kutokuwepo kwa umeme wa uhakika.

Naye Diwani wa Kata wa Litumbandyosi, Mhe.  Prisca Haule amesema walikuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa viwanda kijijini hapo, licha ya kuwa ni wazalishaji wakubwa wa korosho na mpunga. Hivyo kufika kwa umeme wa REA kutawezesha kuanzishwa viwanda mbalimbali vikiwemo vya kubangua korosho na kukoboa mpunga.

Kwa upande wake mfanyabiashara wa vinywaji kijijini hapo, Elbert Kinunda amesema walikuwa wakipata changamoto mbalimbali katika kutumia umeme wa sola, ikiwemo kipindi cha mvua, ambapo betri zinashindwa kujichaji kutokana na kukosekana kwa jua, hivyo biashara katika mazingira magumu ya kukosa mwanga wakati wa usiku.

“Baada ya kuwashiwa umeme wa REA nina amini maendeleo yatakuwa makubwa sana, hata sisi wafanyabiashara wa vinywaji tutaanza kuuza vinywaji vya baridi. Umeme pia utatuwezesha kuanzisha viwanda vya kuchomea vyuma, ambayo tulikuwa tunashindwa kuvianzisha kutokana na kukosekana kwa umeme wa uhakika,” amesema Kinunda. Wampongeza Rais Samia Kufikiwa Umeme wa REA

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.