• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI wa Masonya Tunduru wamshukuru Rais kwa kuboresha barabara

Imewekwa kuanzia tarehe: March 2nd, 2023

WAKAZI wa Kata ya Masonya Halmashauri ya wilaya Tunduru mkoani Ruvuma,wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa  fedha zilizofanikisha kujenga barabara ya Tunduru-Masonya-Nambalapi yenye urefu wa kilomita 6  ambayo ilikuwa ni changamoto kwa wakazi hao.

Wametoa shukurani hizo jana mbele ya Diwani wa kata ya Masonya Said Bwanali ,wakati wa ziara yake ya kukagua matengenezo ya mradi wa barabara  hiyo yanayofanyika kutoka kiwango cha udongo  na kwenda kiwango cha changarawe na kusimamiwa na wakala wa barabara za mjini na vijijini Tanzania (Tarura)wilaya ya Tunduru.

Habibu Ali mkazi wa kijiji cha Masonya alisema,changamoto kubwa ya barabara hiyo ilikuwa wanapohitaji kwenda Tunduru mjini kufuata huduma mbalimbali za kijamii hakukuwa na usafiri wa uhakika kutokana na ubovu na  hapakuwa na barabara nyingine mbadala.

Habibu ambaye ni dereva wa Bajaji inayofanya safari kati ya Tunduru mjini na kijiji cha Masonya alisema,barabara hiyo iliyowapa wakati mgumu hasa wanapohitaji kufika Tunduru mjini kufuata huduma za kijamii au kusafirisha wagonjwa ambapo ameipongeza serikali kwa kuipatia fedha Tarura ziliwezesha kufanya matengenezo ya barabara hiyo.

Alisema,hata walipotaka kusafirisha vifaa vya ujenzi ilikuwa kero kubwa maana walilazimika kutumia watu kubeba na kufikisha sehemu husika hali iliyosababisha gharama za maisha kuwa juu.Cheva Saleh aisema kuwa,hali ilikuwa mbaya zaidi hasa nyakati za masika kutokana na utelezi uliokuwepo ambapo walilazimika kutembea kwa miguu au kupanda baiskeli, jambo lililochelewesha  sana maendeleo ya wananchi wa Masonya.

Diwani wa kata ya Masonya Said Bwanali,amempongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anazozifanya katika kuharakisha maendeleo ya wananchi na ukuaji wa uchumi hapa nchini.

Bwanali ambaye ni makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Tunduru alisema,katika kipindi cha miaka miwili cha uongozi wa Dkt Samia kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa wananchi wa wilaya hiyo nan chi kwa ujumla.

Ametaja baadhi ya mafanikio hayo ni kuimarika kwa huduma za afya,maji na barabara na kwa mara ya kwanza tangu Uhuru wa Tanganyika na sasa Tanzania kata hiyo imepata barabara bora na imara iliyojengwa kwa changarawe inayopitika majira yote ya mwaka.

Alisema,kata ya Masonya ni ya kilimo hivyo sehemu kubwa ya wakazi wake ni wakulima ambapo awali walishindwa kusafirisha mazao kwenda sokoni kutokana na miundombinu mibovu ya barabara na kuwapongeza watendaji wa Tarura kwa kusimamia vuzuri matengenezo ya barabara hiyo.

Kwa upande wake kaimu meneja wa Tarura wilaya ya Tunduru Msolwa Julius alieleza kuwa,mradi huo unajumuisha ujenzi wa barabara tatu za Marumba-Mbesa kilomita 12,Kangomba-Marumba-Njenga kilomita 24 na Tunduru-Masonya-Nambalapi kilomita 6.

Alisema,gharama za mradi huo ni shilingi milioni 650 na katika kipande cha Tunduru-Masonya kazi iliyofanyika ni kufungua barabara hiyo na kuweka kifusi umbali wa km zote 6 na ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 100 na wananchi wameanza kuitumia barabara hiyo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.