• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI waomba kuendelea kuboreshwa bustani ya Ruhila Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: January 22nd, 2025

Wanchi wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma,wameishauri Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kuboresha Bustani ya wanyamapori Ruhila Zoo ili kushawishi na kuvutia watu wengi zaidi kwenda kutembelea bustani hiyo ya wanyama.


Wamesema,licha ya Mamlaka ya Udhibiti wa Wanyamapori Tanzania(Tawa) kanda ya Kusini kupeleka wanyama,lakini katika eneo hilo kuna changamoto nyingi ambazo serikali inatakiwa kuzifanyia kazi ili bustani ya wanyamapori Ruhila iwe chanzo kikubwa cha mapato ya Serikali.


Aidan Komba,Mkazi wa mtaa wa Mshangano katika Manispaa ya Songea alisema,bustani ya Ruhila ikiboreshwa kwa kuwekwa miundombinu mizuri na rafiki kama maeneo mengi ya kucheza watoto,mabwawa ya kuogolea na kutembea kwa mitumbwi na wanyama wa kila aina itawashawishi watu wengi kutembelea tofauti na ilivyo sasa.



Agostino Nombo,ameiomba Serikali kutupia jicho bustani ya wanyamapori Ruhila kwa kuweka mazingira mazuri ili kuwavutia watu kwenda kuona vivutio mbalimbali vilivyopo kama vile wanyama,ndege na miti aina mbalimbali iliyozunguka kwenye bustani hiyo iliyoanzishwa tangu mwaka 1973.


Helen Kavishe,ameipongeza TAWA kwa kuleta wanyama mbalimbali katika Bustani ya Ruhila Zoo ambapo alieleza kuwa, sasa wananchi wa Ruvuma hususani wanaoishi katika manispaa ya Songea wamepata sehemu nzuri ya mapumziko na kuwataka wananchi wenzake kuhakikisha wanakwenda kutembelea bustani hiyo ili waweze kujifunza na kujionea vivutio mbalimbali vilivyopo.


Serikali kupitia mamlaka ya usimamizi Wanyamapori Tanzania(TAWA) chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii imeleta Simba wawili majike waliopewa majina ya Lucy na Liana katika Bustani hiyo kutoka Hifadhi ya Wanyamapori ya Seva jijini Arusha ili kuchochea utalii wa ndani.

Bustani hiyo imeanzishwa kwa ajili ya wananchi wa mkoa wa Ruvuma na Watanzania kwa ujumla, kama mkakati wa Serikali ya mkoa wa Ruvuma katika kumuunga mkono Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.


Lengo la kuanzishwa kwa Bustani ya Wanyamapori Ruhila iliyopo katika Manispaa ya Songena yenye wanyama aina mbalimbali kama vile Pofu,nyumbu Pundamilia,kakakuona,sungura,nyani,kuro na swalapala ili wananchi waweze kupata sehemu maalum ya kupumzika ambapo mbali na.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.