• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANANCHI washauriwa kuacha mila zinazochochea maambukizi ya HIV

Imewekwa kuanzia tarehe: December 1st, 2024

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, amewataka wananchi wa Tanzania kuzingatia Elimu inayotolewa kupitia kampeni mbalimbali ili kuachana na mila zinazoweza kuwa vichocheo vya maambukizi ya VVU.

Ametoa rai hiyo wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani ambayo kitaifa imefanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma.

"Ninaendelea kutoa rai kwa watanzania kuzingatia maudhui ya Elimu inayotolewa kupitia kampeni mbalimbali, kuachana na mila zinazoweza kuwa vichocheo vya maambukizi na kuendelea kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI," alisema Mhe. Dkt. Mpango.

Ameongeza kuwa kundi la vijana hasa wa kike wapo kwenye hatari zaidi ya kupata VVU, hivyo ameiagiza Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) kushirikiana na wadau na jamii kwa ujumla kuweka mkazo katika kudhibiti mazingira yanayochochea maambukizi.

Kupitia maadhimisho hayo ametoa wito kwa vijana kujitambua, kujithamini na kutunza maisha yao kwa kujikinga dhidi ya maambukizi mapya ya VVU, na ambao wanaishi na maambukizi kuendelea kutumia dawa za kufubaza makali ya virusi kwa usahihi na kuimarisha afya zao.

Kwa upande mwingine Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ya mwaka huu ambayo inasema Chagua Njia Sahihi, Tokomeza UKIMWI inakumbusha umuhimu wa kuwa na mikakati na mbinu bora za kuendelea kushirikisha jamii ili kufikia malengo ya kuwa na Tanzania isiyo na maambukizi ya VVU ifikapo mwaka 2030.

Hata hivyo amesema kuwa maadhimisho hayo mwaka huu yanatoa msisitizo kwa vijana kuendesha mijadala na kuwa na matukio mbalimbali ili kuwawezesha kupata Elimu kwa pamoja kuhusiana na masuala ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Naye Waziri wa Afya, Mhe. Jenista Mhagama, amesisitiza kuwa Wizara ya Afya itaendelea kuongeza jitihada kuhakikisha inafanya mapitio ya kisera, mikakati na miongozo ya kutoa huduma bora kwa jamii katika afua zote za mwitikio dhidi ya VVU na UKIMWI.

Amesisitiza kwamba UKIMWI bado upo, hivyo Taifa lina kila sababu ya kuendelea kuzuia maambukizi mapya na kuhakikisha walio na maambukizi wanafubaza VVU.

Siku ya UKIMWI Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 1 Desemba ambayo inalenga kueneza ufahamu kuhusu UKIMWI, kuwakumbuka waliopoteza maisha kutokana na UKIMWI,  kuhamasisha hatua za kuzuia maambukizi mapya, na kupambana na unyanyapaa unaohusiana na VVU au UKIMWI.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.