• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANAWAKE Ruvuma waaswa kuacha ukatili dhidi ya wanaume

Imewekwa kuanzia tarehe: March 6th, 2025

Baadhi ya wanawake wamekuwa wakifanya vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanaume wao, hasa wale ambao wamepata fursa za kipato. 

Tabia hii inatajwa kusababisha msongo wa mawazo kwa wanaume, hali inayoweza kuchangia vifo vyao vya mapema. 

Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, wanawake wa mkoa wa Ruvuma wamehimizwa kuacha tabia hiyo.

Akizungumza katika kongamano la wanawake wa Ruvuma, Mbunge wa Viti Maalum wa mkoa huo, Mhe. Jacqueline Ngonyani Msongozi, alisema kuwa mwanamke kuwa na kipato haimaanishi kumvunjia heshima mume wake. 

Alisisitiza kuwa heshima kwa mume ni wajibu wa mwanamke, hata kama anajitegemea kifedha.

Mhe. Msongozi alibainisha kuwa baadhi ya wanaume wanapitia changamoto kubwa za kisaikolojia kutokana na ukatili wa wake zao, hali inayowafanya kushindwa kufurahia maisha ya ndoa. Alisema kuwa heshima na maelewano kati ya wanandoa ni msingi wa familia imara na yenye furaha.

Aidha, aliwahimiza wanawake kutumia fursa za kiuchumi kuboresha maisha ya familia zao badala ya kuzitumia kama sababu ya kudharau au kutawala wanaume wao. Alieleza kuwa mafanikio ya mwanamke yanapaswa kuwa chachu ya maendeleo ya familia nzima, si chanzo cha migogoro.

Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani, wanawake waliombwa kujitathmini na kuhakikisha kuwa wanachangia katika kujenga jamii yenye usawa na heshima kwa wote. Wito ulitolewa kwa wanandoa kushirikiana kwa kuheshimiana ili kuepuka athari za msongo wa mawazo unaoweza kuleta madhara makubwa kwa wanaume.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.