• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WANUFAIKA wa TASAF washauriwa kutumia ruzuku kwa malengo yaliyokusudiwa

Imewekwa kuanzia tarehe: January 27th, 2022

WANUFAIKA wa mpango wa kunusuru kaya maskini katika kata ya Amani Makolo Halmashauri ya wilaya Mbinga,wametakiwa kutumia  kiasi cha fedha wanazopata kuwekeza katika  elimu  ya watoto wao kwa kuwapeleka  shule, badala ya kuzitumia katika anasa.

Wito huo umetolewa hivi karibuni  na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge,wakati akizungumza na wanufaika wa mpango huo wa kata ya Amani Makolo Halmashauri ya wilayani Mbinga akiwa katika ziara ya siku moja kutembelea kaya maskini zinazopokea ruzuku ya fedha kutoka mfuko wa maendeleo ya jamii(Tasaf).

Alisema, madhumuni ya mpango  kunusuru kaya maskini ni kuziwezesha jamii hasa kaya hizo kuongeza kipato,fursa na uwezo wa kugharamia mahitaji ya msingi ikiwamo chakula,malazi,afya, elimu na kuziwezesha kuwekeza kwenye rasilimali watu kwa kuwapa ruzuku yenye masharti  kwa watoto kuhudhuria shule na kliniki.

Ibuge amewataka walengwa hao, kutumia fedha hizo kama ilivyo mpango wa Serikali  ambao unalenga kuhakikisha kila mtoto hapa nchini anayetoka katika familia maskini anapata elimu,matibabu kwa  wazazi na walezi kujiunga na mfuko wa afya ya jamii na wanufaika kujikimu kimaisha.

Alisema, ni muhimu kutambua uzito wa kile wanachopokea  na Serikali ambayo ina nia njema na wananchi kwa kutafuta na kutoa fedha ili ziweze kubadili maisha ya  baadhi ya watu wenye kipato duni ili kuwajengea uwezo kiuchumi na kushiriki kazi mbalimbali za maendeleo katika jamii.

Alisema, unufaikaje huo ni lulu na hauwezi kuendelea milele, hivyo amewakumbusha wanufaika wa  mpango huo kukumbuka kujiwekea akiba na kuanzisha miradi ya kiuchumi  ili waweze kujitegemea siku za baadaye badala ya kuendelea kuitegemea Serikali.

Aidha Jenerali Ibuge,amewataka wananchi wa wilaya ya Mbinga  kutunza mazingira  na  kulinda vyanzo vya  maji wakati huu ambao wanaendelea na shughuli zao za kilimo na kuwaagiza viongozi wa vijiji,kata na wilaya kusimamia sheria za mazingira zilizopo.

Amewapongeza baadhi ya wananchi waliojiunga na mfuko wa afya ya jamii,hata hivyo amewataka viongozi wa wilaya hiyo kuendelea kuhamasisha watu wengine kujiunga na mfuko huo  ili waweze kupata matibabu kwa urahisi pindi wanapougua.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mbinga Aziza Mangosongo alisema, wilaya hiyo yenye Halmashauri mbili imepokea jumla ya Sh.3,122,582,400.00 kwa ajili ya malipo ya  walengwa 12,067 wa mpango wa kunusuru kaya maskini katika vijiji 195.

Alisema,Halmashauri ya wilaya imepokea Sh.2,243,912,400.00 kwa ajili ya malipo ya kaya 8,669  na Halmashauri ya Mji Mbinga imepokea Sh.878,670,000.00 kwa ajili ya kaya 3,398.

Mamgosongo alimueleza Mkuu wa mkoa kuwa, mwaka wa fedha 2020/2021 malipo yamefanyika katika awamu sita na kaya 8669 zimenufika kwa vipindi vya miezi miwili katika kila dirisha la malipo kwa kupokea ruzuku ya msingi na ruzuku ya  masharti na Sh.2,243,912,400.00 zimelipwa kwa kaya maskini.

Alisema,kupitia mpango huo kumekuwa na mafanikio makubwa ambapo fedha zinazohawilishwa kwa kaya   za walengwa vijijini zimeweza kutoa msukumo katika shughuli mbalimbali za kiuchumi kutokana na ongezeko la mzunguko wa fedha.

Mangosongo alitaja mafanikio mengine ni baadhi ya kaya kutumia sehemu ya fedha wanazopata kujiunga na mfuko wa afya ya jamii iliyoboreshwa ambapo jumla ya kaya za walengwa 4,918 kati ya kaya 8,669 sawa na asilimia 77 zimejiunga na mfuko  huo.

Alisema, kupitia mpango huo kasi ya   watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kupelekwa kliniki ni kubwa na mahudhurio ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari yameongezeka kufuatia kuboreka kwa maisha ya watoto wanaotoka katika kaya maskini.

Mwisho.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.