• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATAALAMU washauriwa kushirikiana,kudhibiti magonjwa ya milipuko

Imewekwa kuanzia tarehe: October 6th, 2020

MTAALAMU wa Epidemiolojia na Udhibiti wa  Magonjwa wa Wizara ya Afya na Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na Watoto Dr.Azma Simba, ametoa rai kwa wataalam kuungana na kushirikiana  ili  kukabiliana na magonjwa ya milipuko na kuimarisha usalama wa afya duniani.

Dr.Simba ametoa rai hiyo wakati anawasilisha mada ya agenda ya kukabiliana na matukio muhimu ya kiafya ya kimataifa, kwenye mafunzo ya utayari wa kukabiliana na magonjwa mlipuko kwa timu za dharura kwa wataalam kutoka mikoa ya Ruvuma na Mtwara.

Akizungumza katika mafunzo hayo ambayo yamefanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Tiffany mjini Mtwara, Dr.Simba amesema dunia imeathirika zaidi na magonjwa ya milipuko yakiwemo ebola na COVID 19 na kwamba mwaka 2014 Agenda ya Afya Duniani ilianzishwa kwa lengo la kuhakikisha Dunia inakuwa salama kutokana na milipuko ya magonjwa hayo.

“Nchi nyingi duniani zimeweka jitihada kubwa katika kujilinda na magonjwa ya mlipuko,hata hivyo ni vema watalaam kufanya kazi kwa ushirikiano ili pawepo na usalama wa afya duniani’’,alisema.

Mtaalam huyo wa kudhibiti magonjwa amesema, kupitia agenda ya afya duniani,imetolewa miongozo na kanuni za kimataifa zinazoongoza kukabiliana na magonjwa ya milipuko.

Ameyataja madhumuni ya Agenda ya afya ya dunia kuwa ni  kuwepo kwa mifumo ya afya ambayo imejikita kuzuia,kutambua mapema na kukabiliana na ugonjwa unapotokea na kwamba milipuko mingi ya magonjwa inayotokea inaweza kuzuilika kwa njia ya chanjo.

Hata hivyo ametoa rai kwa  timu za dharura za kukabili magonjwa ya mlipuko katika ngazi za Halmashauri na Mkoa  kufanya ufuatiliaji wa magonjwa kwa wakati na kutoa taarifa mapema katika ngazi husika.

Kwa upande wake Daktari wa mifugo  Dr.Moses Ole Neselle kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Duniani(FAO) akitoa mada kwenye mafunzo hayo,ameyataja magonjwa sita ya kipambele ambayo yanaambukiza kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu kuwa ni Kichaa cha mbwa  ambacho kinatarajiwa kutokemezwa mwaka 2030.

Ameyataja magonjwa mengine kuwa ni homa ya bonde la ufa,kutupa mimba kwa wanyama,mafua ya ndege,kimeta na ugonjwa wa ebola na amesisitiza kuwa magonjwa hayatambui mipaka ya nchi hivyo ni vema wataalam wote kushirikiana kukabiliana na magonjwa hayo.

Amesema asilimia 50 ya magonjwa yote yanaambukizwa kupitia virusi na kwamba asilimia 60 ya magonjwa ya binadamu yanasababishwa na wanyamapori hivyo ameshauri kuwepo mpango mkakati wa kukabiliana na magonjwa hayo.

Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Profesa Rudovick Kazwala imesisitiza kuwa katika kutokomeza magonjwa ya mlipuko ni lazima wataalamu wafanye kazi kwa kushirikiana ili kutoa matokeo chanya.

Imeandikwa na Albano Midelo na Netho Credo

Maafisa serikalini

Mtwara

Oktoba 6,2020

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.