• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATALAAM 180 wa mikoa 26 waanza mafunzo ya Mfumo mpya wa ununuzi wa umma Dodoma

Imewekwa kuanzia tarehe: August 1st, 2023

Na Albano Midelo,Dodoma

WATAALAM 180 kutoka Sekretarieti za mikoa 26 Tanzania Bara wameanza mafunzo ya siku tano kuhusu mfumo mpya wa ununuzi wa umma (NeST).

Mafunzo hayo yanayofanyika kwenye ukumbi wa PSSSF jijini Dodoma yameandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi ya Umma (PPRA).

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo Mtendaji Mkuu wa PPRA Joakim Maswi  amesema PPRA imeunda mfumo mpya wa ununuzi wa umma unaoitwa National eprocurement Sytem of Tanzania (NeST) ambao umeanza kutumika Julai Mosi 2023.

Amesema serikali imepitisha sheria ya kuanza kutumika mfumo mpya wa ununuzi wa umma NeST baada ya kubaini changamoto za kiufundi zilizojitokeza kwenye mfumo wa ununuzi wa awali (TANePS) na lengo ni kuhakikisha hadi Agosti 15,2023 Taasisi zote zianze kutumia mfumo wa NeST.

“Mfumo wa TANePS utakoma kutumika ifikapo tarehe 30 Septemba 2023,kwa hiyo mara baada ya mafunzo haya,ninyi RS zote 26 ambao mmefika hapa Dodoma mtakwenda kuwa  walimu wa mfumo mpya wa ununuzi NeST katika Halmashauri zote 184 za Tanzania Bara’’,alisema Maswi.

Amezitaja faida za mfumo mpya wa ununuzi wa umma kuwa ni Pamoja na kuongeza wigo wa ushiriki kwenye ununuzi,uwajibikaji,kupunguza muda wa mchakato,upatikanaji wa taarifa na  kupunguza mianya ya rushwa.

Faida nyingine amezitaja kuwa ni uandaaji wa zabuni zote na uombaji wa zabuni utafanyika ndani ya mfumo,wazabuni watajisajiri na kupandisha nyaraka zao zote kwa mara moja na nyaraka zote zitasainiwa ndani ya mfumo.

Akuzungumza wakati anafungua mafunzo hayo,mgeni rasmi Katibu Mkuu wa TAMISEMI Adolf Ndunguru amesema wataalamu ngazi ya mikoa  baada ya kuhitimu mafunzo hayo wanakwenda kuwa walimu  kwa watumiaji wengine wa mfumo wa NeST .

Amesema sekta ya ununuzi wa umma inachukua takriban asilimia 70 ya Bajeti ya Serikali hivyo amesisitiza kuwa ununuzi wa umma ni eneo nyeti hali iliyosababisha serikali kutenga fedha nyingi ili kufanikisha malengo na matarajia ya nchi kwenye ununuzi.

Ameutaja uamuzi wa serikali kuamua kuanza kutumia mfumo wa NeST ni kuingia katika mapambano ya adui rushwa ambaye ameshamiri kwenye mfumo wa ununuzi wa umma na kwamba mfumo utaongeza uwajibikaji kwa watendaji hasa PPRA wanaosimamia mfumo wa ununuzi wa umma.

“Mfumo huu umepewa uwezo wa kufuatilia mienendo yote ya ununuzi kwenye Taasisi za umma,hata ikitokea kumefanyika uzembe,ni rahisi kumtambua mtu aliyefanya uzembe huo,natoa wito kwa wote wanaohusika kwenye mfumo wa ununuzi wa umma kufanya kazi kwa kuzingatia maadili,sheria na taratibu zote’’,alisisitiza Ndunguru.

Hata hivyo Katibu Mkuu huyo amepongeza ujasiri wa  Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuridhia mfumo mkubwa wa ununuzi wa umma  wenye maslahi mapana kwa Taifa letu kujengwa na wataalam wa hapa nchini hivyo kuepuka wataalam wa nje.

Mfumo wa NeST utakuwa mbadala wa mfumo unaotumika hivi sasa wa TANePS,unatarajiwa kutatua changamoto za kiufundi na hivyo kukidhi mahitaji ya Serikali Katika Sekta ya ununuzi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.