• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATU 2900 Mbinga kunufaika na mradi wa maji wa bilioni 1.8

Imewekwa kuanzia tarehe: November 23rd, 2022

WAKAZI zaidi ya 2900 wa kijiji cha Mbangamao Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma wanatarajia kunufaika na mradi wa maji unaogharimu shilingi bilioni 1.8.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Meneja RUWASA Wilaya ya Mbinga Mhandisi Mashaka Sinkala amesema mradi huo ambao utekelezaji wake umefikia asilimia 65 unatarajia kukamilika Januari 2023.

Hata hivyo amesema mradi umechelewa kukamilika kutokana na Mkandarasi wake kuongezewa muda wa utekelezaji kutoka miezi sita hadi tisa. 

“Hadi sasa ujenzi wa chanzo umekamilika kwa asilimia 100,ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji la lita 200,000 umefikia asilimia 95 na uchimbaji mtandao wa maji umefikia umbali wa kilometa 14”,alisema.

Akizungumza baada ya kukagua mradi huo,Mkurugenzi Mkuu wa RUWASA Mhandisi Clement Kivegalo amewaagiza watumishi wa RUWASA kuanza kujenga vituo vya kuchotea maji kwa sababu tayari maji yapo ndani ya tanki la mradi.

Amesema wananchi wanahitaji maji hivyo RUWASA isisubiri uzinduzi wa mradi utakapokamilika badala yake waanze kuwasambazia maji wananchi wa Mbangamao. “Kwenye miradi ya maji ya mserereko unapokuwa umejenga tanki unatakiwa uanze kuwanywesha maji wananchi  “,alisema.

Amesema hakuna sababu ya wananchi kuendelea kuteseka kwa sababu maji ni bidhaa muhimu katika maisha ya kila siku.

Naye Joseph Kapinga Mkazi wa kijiji cha Mbangamao amesema wanamshukuru Rais Samia kwa mradi wa maji ambao unakwenda kumaliza kero ya kusafiri umbali mrefu kwa akinamama na watoto kutafuta maji.

Mradi wa maji Mbangamao ni miongoni mwa miradi nane ya maji katika Wilaya ya Mbinga inayotekelezwa na RUWASA kwa fedha za mfuko wa maji na serikali kuu.

Imeandikwa na Albano Midelo,Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.