• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATUMISHI Ruvuma walia na mishahara midogo

Imewekwa kuanzia tarehe: May 2nd, 2021


WAFANYAKAZI mkoani Ruvuma wamelalamikia mishahara yao kuwa bado ni midogo ukilinganisha na hali halisi ya maisha ya wafanyakazi.

Akisoma risala ya wafanyakazi wa Mkoa wa Ruvuma katika sherehe ya Mei Mosi iliyofanyika kimkoa mjini Mbambabay wilayani Nyasa,Katibu wa TUGHE Mkoa wa Ruvuma Ismail Mudathir amesema katika sekta ya umma na binafsi mishahara haikidhi mahitaji ukilinganisha na kupanda kwa gharama za maisha.

“Tunaiomba serikali kupitia Mei Mosi hii,kwa itutazame jicho la kipekee kabisa iongeze mishahara na kuboresha maslahi kwa wafanyakazi kwa sababu ni muda mrefu sana mishahara haijaongezwa’’,alisisitiza Katibu wa TUGHE.Amesema watumishi wa Mkoa wa Ruvuma,wanakabiliwa na changamoto za kiutumishi zikiwemo baadhi ya waajiri kutowatendea haki baadhi ya watumishi hali ambayo ina punguza molali kwa wafanyakazi.

Amezitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni kutolipwa madeni ya uhamisho wa watumishi,baadhi ya watumishi kutopandishwa madaraja kwa wakati na baadhi ya waajiri kutolipa nauli za watumishi na mizigo yao wanapostaafu.

Hata hivyo licha ya changamoto hizo Katibu huyo wa TUGHE kwa niaba ya watumishi mkoani Ruvuma amesema,wafanyakazi wanaahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa maslahi mapana ya nchi ya Tanzania.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Isabela Chilumba ametoa rai kwa watumishi kuwa na subira kwa sababu serikali ya Awamu ya sita imedhamiria kuboresha maslahi ya watumishi.

“Serikali mwezi huu imeanza kutoa barua za kuwapandisha madaraja watumishi wa umma wanaostahili katika nchi nzima na katika Halmashauri za wilaya baadhi ya watumishi wameanza kupata barua za kupandishwa madaraja kupitia maafisa utumishi’’,alisema Chilumba.

Hata hivyo amewaagiza waajiri kuhakikisha wanawalipa mafao na haki zao zote watumishi wanaostaafu na kuwaagiza waajiri kwenye Halmashauri na Taasisi zote za serikali kuacha kuchelewesha fedha za malipo ya likizo kwa watumishi wanaokwenda likizo.

Mei Mosi ni siku ya wafanyakazi wote duniani inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo Mei Mosi,kauli mbiu ya mwaka huu ni maslahi bora,mishahara juu,kazi iendelee.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Tarehe 2/5/2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.