• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZAZI 763 wakamatwa Tunduru kwa kutopeleka watoto shule

Imewekwa kuanzia tarehe: January 27th, 2023

AIDI ya wazazi 763 wamekamatwa katika operesheni maalum ya nyumba hadi nyumba, ya kuwasaka wazazi na walezi wasiopeleka watoto wao waliochaguliwa kuanza masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu katika wilaya yaTunduru mkoani Ruvuma.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru  Mheshimiwa Julius Mtatiro amesema,kukamatwa kwa wazazi hao kumetokana na muda wa siku 14 waliopewa kupeleka watoto shule kwa hiari kumalizika licha ya  uhamasishaji mkubwa uliofanywa na viongozi wa serikali,kamati ya ulinzi na usalama na madiwani.

Kwa mujibu wa Mtatiro,msako huo unafanyika usiku na mchana,na ni mkakati wa kuwapata watoto wote 5,869 waliomaliza darasa la saba mwaka jana na kuchaguliwa kuendelea na kidato cha kwanza,lakini hadi mwishoni mwa wiki iliyopita wamebaki nyumbani.

Aidha amesema,katika msako huo wazazi wengine  600 wamejisalimisha kwa kupeleka watoto wao shule baada ya kushuhudia  wenzao wamekatwa na kufikishwa polisi kwenye operesheni inayoendelea katika maeneo mbalimbali wilayani humo.

Mtatiro alisema,operesheni hiyo imekuwa yenye mafanikio makubwa kwani katika muda wa siku tatu wamewapeleka zaidi ya watoto 1,335  shule kati ya 5,868 wanaotakiwa kuanza kidato cha kwanza na wanaendelea kuwatafuta watoto waliobaki.

Mtatiro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilayani Tunduru alisema,watahakikisha hadi Jumatatu ya wiki ijayo watoto wote wanaotakiwa kuanza  kidato cha kwanza  katika muhula wa masomo ulioanza tangu tarehe 9 Januari wanaripoti kwenye shule walizopangiwa.

“tunendelea kuwasaka na kuwachukulia hatua za kisheria wazazi na walezi ambao baada siku 14 tulizowapa za maandalizi ya watoto wao kupita lakini wameshindwa kutumia  fursa hiyo vizuri,tunataka vijana wote wanaotakiwa kuanza kidato cha kwanza katika wilaya yetu wanaripoti kwenye shule walizopangiwa na sio vinginevyo”alisema Mtatiro.

Alisema,serikali ya awamu ya sita imetoa fedha nyingi za kujenga shule mpya, kuongeza madarasa mapya kwa baadhi ya shule za zamani,kununua meza na viti na kusimamia sera ya elimu bila malipo kuanzia  darasa la awali hadi kidato cha sita.

Alisema,licha ya serikali kukamilisha ujenzi wa shule mpya na vyumba vya madarasa kwa asilimia 100,lakini inasikitisha kuona mpaka baadhi ya wanafunzi bado wako nyumbani huku wazazi wao wakitoa visingizio visivyokuwa na msingi.

Amewakumbusha wazazi na walezi wilayani humo kutambua kuwa,muda wa kupeleka watoto shule kwa hiari umepita na sasa wanatakiwa kupeleka kwa lazima na atakayeshindwa atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwamo kufikishwa mahakamani.

“hakuna kikwazo kwa wazazi kushindwa kupeleka watoto shuleni,serikali  ya Mama Samia  Suluhu Hassan imefanya mambo makubwa kwa kutengeneza madawati,viti na meza ambazo awali mzazi alilazimika kutumia kati ya Sh.80,000 hadi 100,000, lakini vifaa hivyo  vinapatikana bure shuleni”alisema.

Mkuu huyo wa wilaya,amewaasa watoto waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza mwaka huu, kuhakikisha wanatumia fursa hiyo kusoma kwa bidii kama njia itakayo wawezesha kutimiza ndoto zao pindi watakapokuwa watu wazima na kamwe wasikubali kufanyishwa kazi za nyumbani kama kuchunga mifugo na kazi za ndani.

Alisema,tunapohitaji maendeleo katika nchi yetu suala la uwekezaji wa elimu ni jambo muhimu sana, ndiyo maana serikali imeamua kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne ni ya lazima,kwa hiyo  wazazi na viongozi wana wajibu kuhakikisha watoto wote wanakwenda shule na wanafikia malengo yao.

Baadhi ya wazazi waliokamatwa katika opresheni hiyo,wameoimba serikali iwaongezee muda wa kupeleka watoto shule ili waweze kufanya maandalizi ya watoto kutokana na hali ngumu ya kiuchumi.

Rehema Waziri alisema,licha ya serikali kuagiza watoto waende shule hata kama hawana mahitaji yote muhimu,lakini kama mzazi bado ana wajibu kumpatia mtoto wao mahitaji ya shule ikiwamo sare na madaftari badala ya kuitegemea serikali kufanya kila kitu.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.