• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI Mhagama azindua kampeni ya Masta Boda mkoani Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: February 18th, 2020

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Ajira na Watu wenye ulemavu Jenista Mhagama(Mb) amezindua huduma ya  masta boda iliyoratibiwa na Benki ya NMB.

Kwa mara ya kwanza kampeni hii ilizinduliwa Oktoba 2019 jijini Dar es salaam na kufuatiwa Mkoa wa Pwani na sasa Mkoa wa Ruvuma.

Uzinduzi huo  wa kampeni hiyo umefanyika kwenye ukumbi wa Misheni Peramiho nje kidogo ya Mji wa Songea,lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa vijana wanaendesha pikipiki wanaingizwa katika mfumo rasmi wa kifedha kupitia  benki ya NMB.

Akizungumza kabla ya kuzindua kampeni hiyo Waziri Mhagama amewataka vijana kuunga mkono dhamira ya kujiunga na  masta boda  ambayo inaweza kuleta mabadiliko ya kiumfumo katika sekta ya bodaboda iliyoajiri vijana wengi.

Amesema asilimia 56 ya nguvukazi  nchini ni vijana na kwamba ajira rasmi hivi sasa ni chache na kwamba vijana wanaweza kutafuta mifumo tofauti ya ajira na kujiajiri au kusaidiwa kutengeneza ajira.

“Leo hii Benki ya NMB inataka kubadilisha mfumo wa ajira ya masta  boda kwenda kuwa ni ajira rasmi iliyorasmishwa na kuwa  ajira yenye staa miongoni mwa ajira nyingine zinazopatikana Tanzania’’,alisisitiza.

Kwa upande wake Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya NMB  Makao makuu  Benedikto Baragomwa amesema huduma ya mastaboda  itawawezesha vijana kuwa na mfumo rahisi wa  malipo ya huduma za bodaboda.

Amesema huduma sasa itawaweka bodaboda katika mfumo rasmi wa kifedha kupitia benki  ya NMB  na kwamba benki hiyo inatarajia kuwafikia waendesha bodboda zaidi ya 75,000 katika nchi nzima.

Amesema idadi kubwa ya waendesha pikipiki tayari wamefungua akaunti na kwamba NMB inatarajia kuwafikia bodaboda 2000 wilayani Songea  kutoa mikopo ya bodaboda na bajaji kwa vijana  160.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo,katika nchi nzima kuna waendesha pikipiki zaidi ya milioni mbili ambao bado hawajaingia kwenye mfumo wa kibenki hivyo amesema NMB inatoa fursa ya vijana hao kuingia katika mfumo rasmi wa kifedha.

Naye Ofisa wa NMB Kitengo cha Mastakadi  Filbert Kazimili akizungumza katika uzunduzi huo amesema biashara ya pikpiki ilianzia mkoani Ruvuma mwaka 2004 ambapo amesema masta boda ni njia nyepesi ya kupokea malipo kwa njia ya simu.

“Benki ya NMB imeshirikiana na masta kadi kuhakikisha kwamba madereva wa bodboda wanapokea malipo kwa njia salama na uhakika kupitia mtandao’’,alisema.

Kwa mujibu wa Kazimili,kwa muda mrefu wamekuwa wanaangaika na ajira na kwamba sekta ya bodboda imekuwa moja ya sekta zinazotengeneza ajira kwa vijana na kwamba NMB imeamua kutoa fursa za kibenki kwa vijana kupitia boda masta boda.

Amesema NMB imekusudia vijana waweze kuaminika na kukopeshwa na kwamba kwa kuanzia kila kijana anayefanya kazi ya bodboda atafungua akaunti ya benki ili akipokea malipo kupitia boda masta ambapo  pesa inaingia moja kwa moja kwenye akaunti yake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodaboda mkoani Ruvuma Hamisi Hassan Maulid  amesema huduma ya usafirishaji ilianza mwaka 2004 katika Manispaa ya Songea kukiwa na wasafirishaji wachache ambapo hadi kufikia mwaka 2008 idadi kubwa ya vijana waliokuwa wanakosa  ajira waliamua kujiingiza kwenye huduma hiyo.

Kiongozi huyo wa bodbado ambaye amehitimu chuo kikuu na kukosa ajira rasmi amesema  hadi kufikia mwaka 2019 idadi ya madereva bodaboda katika Mkoa wa Ruvuma ilifikia 85,000.

Anayataja mafanikio ambayo madereva boda wameyapata hadi sasa kuwa ni  kupata kipato,kusomesha watoto,ujenzi wa nyumba za makazi na kwamba kazi hiyo ni ajira mbadala ambayo imepunguza kasi ya vijana kushinda vijiweni.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Pololet Mgema  ameipongeza NMB kwa kuanzisha huduma hiyo  ambapo amewaomba waendesha bodaboda kujiunga na huduma hiyo sanjari na  kuchukua vitambulisho vya wajasiriamali ambavyo vitawawezesha kupata mikopo kupitia NMB.

“Nawaomba vijana wa bodboda tujiunge,tutambuane kwa sababu kuna manufaa makubwa ya kiuchumi na kiusalama endapo mtajiunga na huduma ya boda masta’’,alisisiza.

Uchunguzi umebaini kuwa dereva wa boda boda kwa siku anapofanyakazi vizuri anaweza kuingiza kipato cha kati ya shilingi 200,000 hadi 300,000 ambao ni mshahara anaolipwa mtumishi anayefanyakazi mwezi mzima.

Ameshauri waendesha pikipiki wote kujiunga na mfumo wa masta boda kwa  sababu utasaidia kujenga tabia ya kutunza akiba na kuleta mabadiliko chanya katika maisha.

Mfumo wa  masta boda utamwezesha dereva wa pikipiki kupata malipo moja kwa moja kutoka kwa mteja hali ambayo itasaidia  fedha zake kuwa salama kwenye akaunti  na kupandisha hadhi ya biashara.

Mwandishi ni Mchangiaji wa gazeti hili,mawasiliano yake ni baruapepe albano.midelo@gmail.com,simu 0784765917

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.