• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI Mkumbo alivyoshangazwa na uwekezaji mkubwa sekta ya kilimo wilayani Songea

Imewekwa kuanzia tarehe: August 26th, 2023

WAZIRI wa Mipango na Uwekezaji Prof.Kitila Mkumbo ameshangazwa na uwekezaji mkubwa katika sekta ya kilimo ambapo katika Halmashauri ya Madaba na Songea mkoani Ruvuma wawekezaji toka nje wamewekeza katika mashamba yenye ukubwa wa hekta zaidi ya 2500.

Akiwa katika Halmashauri ya Madaba,Waziri Mkumbo alishuhudia uwekezaji mkubwa wa Kampuni ya kigeni ya Silver Ndolela iliyowekeza katika shamba lenye ukubwa wa hekta 1500 ambapo kampuni hiyo inazalisha mbegu za aina nne kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji.

Meneja wa shamba hilo alizitaja mbegu zinazozalishwa na Kampuni hiyo kuwa ni maharagwe,mahindi,ngano na  viazi ambapo Waziri Mkumbo alisisitiza uwekezaji katika mbegu bora ni muhimu hapa nchini kwa kuwa moja ya changamoto katika kilimo ni upatikanaji wa mbegu bora.

“Wakulima wetu wanatumia mbegu hafifu wanalima eneo kubwa na kupata mavuno kidogo,hivyo uwepo wa shamba hili la mbegu bora itasaidia  kuboresha kilimo  hapa nchini ’’,alisisitiza Waziri Mkumbo.

Waziri wa Mipango na Uwekezaji pia alikagua shamba kubwa la kilimo cha umwagiliaji la Kampuni ya AVIV katika Kijiji cha Lipokela Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Prof.Mkumbo amefurahishwa na uwekezaji mkubwa katika shamba kahawa uliofanywa na Kampuni ya AVIV TANZANIA LTD ambapo Kampuni hiyo inalima na kuchakata kahawa kwa mwaka tani zaidi ya 2000 katika shamba la kahawa lenye ukubwa wa hekta zaidi ya 1000.

Waziri Mkumbo amesisitiza kuwa kulima na kuchakata kahawa ni uwekezaji mkubwa ambao umefanywa kwa kuwezeshwa na Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC) ambapo amesema uwekezaji huo unashughulikia sekta ya kilimo ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Ameipongeza Kampuni ya AVIV kwa kutekeleza mambo matatu kwa wakati mmoja ikiwemo kilimo cha kahawa,kuchakata mazao ya kilimo hivyo kutoa ajira kwa watanzania na kuongeza mauzo nje ya nchi.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mheshimiwa Kapenjama Ndile akizungumza baada ya Waziri kutembelea maeneo ya uwekezaji katika shamba la Madaba na Lipokela,ameutaja Mkoa wa Ruvuma  kwa miaka 13 sasa unaongoza kwa uzalishaji wa mazao ya chakula nchini.

Amesema katika kutambua mchango wa Mkoa wa Ruvuma kwenye uzalishaji chakula ,mwaka huu kwenye maadhimisho ya Nanenane Kitaifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan alitoa chetu maalum kwa Mkoa  wa Ruvuma kwa kushika nafasi ya kwanza kwa uzalishaji nafaka.

Awali akitoa taarifa ya Kampuni ya AVIV, Meneja Msaidizi wa Kampuni ya AVIV TANZANIA Muthana Namb amesema asilimia 80 ya kahawa inayochakatwa na Kampuni hiyo inauzwa katika nchi mbalimbali Duniani zikiwemo Marekani,Saudi Arabia,India, Japan, Jordan na Afrika ya Kusini.

Naye Mwakilishi wa Kampuni hiyo anayesimamia kilimo Johson Kishumba amesema Kampuni ya AVIV TANZANIA imekuwa kampuni ya kwanza katika bara la Afrika kupewa Tuzo ya Water Stewardship inayotolewa na SGS ya nchini Afrika ya Kusini kwa kufanya vizuri kwenye kilimo na mazingira.

Hata hivyo amesema kampuni hiyo inashirikiana na wananchi wanaozunguka shamba hilo ambao wamekuwa wanasaidiwa katika sekta za afya,maji na mazingira na kwamba baadhi ya wananchi wanapata ajira kwenye shamba la kahawa.

Waziri wa  Mipango na Uwekezaji alifanya ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Ruvuma kwa lengo la kukutana na wawekezaji,kusikiliza mafanikio na changamoto zao ili kuzitafutia ufumbuzi hatimaye kuimarisha zaidi eneo la uwekezaji.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.