• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WAZIRI MKUU sijaridhishwa na ujenzi wa hospitali ya Namtumbo

Imewekwa kuanzia tarehe: October 18th, 2022

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyesha kukerwa  na mlango mbovu uliowekwa kwenye chumba cha upasuaji wakati alipokagua ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, Oktoba 18, 2022. Aliagiza milango mibovu  iondolewe na iwekwe milango yenye ubora unaokubalika. Kulia ni Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dkt. Christopher Wabwar

  • Aagiza milango zaidi ya 10 ing’olewe, akuta varnish imepakwa leo

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Namtumbo na kusema Serikali haiwezi kukaa kimya huku baadhi ya watumishi wakifanya vitendo vya hovyo.

“Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameleta shilingi bilioni 7 za ujenzi wa hospitali hii. Fedha hizi za ujenzi ni lazima wananchi waone thamani ya fedha zao. Siwezi kukubaliana na utendaji wa hovyo. Fedha ziko hapa tangu Aprili, ni kwa nini hadi sasa majengo yapo kwenye lenta? Huu ni ubabaishaji,” amesema. 

Waziri Mkuu ametoa onyo hilo leo (Jumanne, Oktoba 18, 2022) wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Migelegele mara baada ya kukagua ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma.

“Nimekagua ujenzi wa hospitali ya wilaya lakini sijaridhishwa na hali ya ujenzi. Nimeagiza milango yenye hitilafu yote ing’olewe na iwekwe yenye hadhi ya hospitali ya wilaya. Iweje imeacha nafasi juu hadi vidole vinapita? Mtu akifunga mlango wewe uliyeko nje unaona ndani. Hii haikubaliki, RC simamieni milango hiyo itolewe, na ije yenye hadhi,” amesisitiza. 

Mapema akikagua ujenzi wa hospitali hiyo, Waziri Mkuu alikuta baadhi ya milango imepishana urefu licha ya kuwa inapaswa ikutane ili kitasa kiweze kufunga. Mingine ilikuwa inagoma kufunga, inarudi nyuma na kubakia wazi. Pia aligusa mlango na kukuta varnish bado haijauka.

Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa mbolea, Waziri Mkuu amesema Rais Samia alitoa ruzuku ya sh.bilioni 150 ili kushusha bei ya mfuko wa mbolea na kuwaeleza wakazi hao kwamba mkoa huo umepangiwa makampuni matano ya kusambaza mbolea.

“Makampuni matano ya Mohammed Enterprises, Yara, OCIP, Premium na ETG yamepangiwa kuleta mbolea hapa mkoani, na hadi sasa tayari tani za mbolea 9,000 zimeshawasili. Kati ya hizo, tani 2,467 zimeshaenda vijijini.”

“Mahitaji ya mkoa mzima ni tani 67,000 kwa hiyo hizi tani 9,000 hazitoshi. Watu wa TFL simamieni ili iletwe haraka. Mbolea za kupandia zije sasa na za kukuzia zije baadaye. Jitahidini kuongeza idadi ya mawakala ili wananchi wafikiwe huko waliko,” amesisitiza.

Mapema, akizungumza na wananchi hao, Waziri wa Nchi (OR-UTUMISHI), Bibi Jenista Mhagama aliishukuru Serikali ya Rais Samia kwa ujenzi wa hospitali na kwamba wanufaika wakubwa ni wanawake, watoto na wazee.

Alisema Serikali itaendelea kuwapangia watumishi wa sekta ya afya ili waweze kufika kutoa huduma kwenye hospitali hiyo. “Mwaka 2022/2023 Serikali itaajiri watumishi 30,000 kwenye ajira mpya, na wengi ni wa sekta ya afya na elimu,” alisema.

Naye, Naibu Waziri wa Nchi (OR-TAMISEMI), Bw. David Silinde alisema Rais Samia ameamu kujenga shule za wasichana katika mikoa yote 26 na iliyopo katika Halmashauri ya Namtumbo ni miongoni wa shule 10 za kwanza nchini ambazo zimepatiwa fedha mwaka huu.

“Shule hizi zimetengewa shilingi bilioni 4 kila moja na zikikamilika zitakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi kati ya 1,000 na 1,200 ambao watakuwa wanasoma masomo ya sayansi.”

Naye, Mbunge wa Namtumbo, Bw. Vita Kawawa alisema anamshukuru Rais Samia kwa kutoa sh. bilioni 15.5 kwa ajili ya shughuli za maendeleo wilayani humo. Pia aliishukuru Serikali kwa kuwapatia mradi ya maji wa sh. bilioni 5 ambao umesaidia wananchi kupata maji bila mgao.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.