• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WILAYA ya Mbinga walivyodhamiria kukabiliana na udumavu na utapiamlo

Imewekwa kuanzia tarehe: August 20th, 2023

Mbinga. Katika juhudi ya kutekeleza agizo la utoaji wa vyakula vyenye virutubisho shuleni, Halmashauri ya Mji wa Mbinga (MTC) jana Agosti 17 ilifanya kikao na wamiliki wa mashine za kuzalisha unga pamoja na SANKU---mtoa huduma katika programu ya kuchanganya virutubishi kwenye unga wa mahindi.

Kikao kilicho wakutanisha SANKU pamoja na wamiliki wa mashine za nafaka kutoka kata nane za Mbinga Mji kililenga kihamasisha wana Mbinga Mji kuwa na mashine nyingi za kuchanganya virutibishi kwenye unga wa mahindi.

Akizungumza wakati wa kikao msimamizi wa kanda wa SANKU Christian Lutaja alisema mashine na virutubishi hotolewa bure na kwamba wahitaji wanachotakiwa kufanya ni kununua mifuko tuu.

"Oda ya kwanza inatakiwa isipungue mifuko 2,000," alisema bwana Lutaja.

Alisema mfuko wa kilo 5 huuzwa kwa Sh475, wakati kilo 50 ni Sh900.

Katika mkoa wa Ruvuma tayari mashine 30 za kuchanganya virutubishi kwenye unga wa mahindi zimefungwa huku Halmashauri ya Mji wa Mbinga ikiwa ni mashine tatu, kwa mujibu wa Lutaja.

Taarifa za uwepo wa kikao na SANKU zilitolewa jana asubuhi na kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga Dkt Kung'e  Nyamuryekung'e wakati wa kikao cha kamati kuhusu taarifa ya utekelezaji wa shughuli za lishe Robo ya nne ya 2022/23 kilichofanyika MTC.

"Tunataka kuhamasishana na kuwapa elimu kuhusu umuhimu wa kufunga mashine hizo za kuongeza viini lishe," alisema Dkt Nyamuryekung'e ambaye pia ni mkuu wa Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe katika halmashauri ya Mji wa Mbinga.

Alisema uamuzi huo ni utekelezaji wa moja ya maazimio ya kikao cha kamati ya lishe ngazi ya halmashauri kilichofanyika Agosti 6 mwaka huu.

Aliongeza kuwa katika kikao hicho ilibainika kuwa utoaji wa vyakula vyenye virutubisho shuleni ni changamoto kwasababu mashine za kuongeza viini lishe ni chache.Kutokana na changamoto hiyo, kamati iliadhimia kuwa wananchi wahamasishwe kulima mazao yenye viini lishe ili watoto wale vyakula vyenye lishe.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.