• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WILAYA YA Mbinga yaanzisha shule ya vipaji maalum kwa wavulana

Imewekwa kuanzia tarehe: July 8th, 2020

MKURUGENZI  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mbinga mkoani Ruvuma Juma Mnwele amesema wilaya hiyo imeamua kuanzisha shule maalum ya wavulana(Mbinga Boys) baada ya kupata mafanikio makubwa katika shule dada ya wasichana (Mbinga Gilrs).

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma Mnwele amesema shule hiyo inaendelea kujengwa katika kijiji cha Ndongosi,na kwamba  hatua za usajili wa shule hiyo zinaanza Oktoba mwaka huu ili mapema Januari 2021  shule ianze kupokea wanafunzi.

Amesema shule hiyo itapokea vijana wa kiume wawili waliofaulu vizuri kutoka katika kila kata wilayani Mbinga na kwamba lengo la mradi huo ni kuwa na shule bora ya wavulana na yenye ufaulu mzuri  kama ilivyo kwa shule ya sekondari ya wasichana ya Mbinga iliyojengwa eneo la Mkako barabara kuu ya Songea-Mbinga.

“Shule hii itaongeza idadi ya wanafuzi wenye vipaji wanaokwenda kupata elimu ya sekondari,shule itakuwa na mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia ili kuifanya elimu kwa vijana wetu kuwa bora na yenye tija’’,alisisitiza Mkurugenzi.

Akizungumzia gharama za mradi wa sekondari hiyo,Mkurugenzi huyo amesema hadi sasa zimetumika shilingi milioni 70 kutekeleza mradi huo zilizotoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo Kampuni ya uchimbaji wa madini TANCOAL waliotoa sh.milioni 20 na shilingi milioni 50 zimetolewa na Halmashauri.

Amesema katika awamu ya kwanza ya ujenzi umehusisha vyumba vitatu vya madarasa kwa gharama ya sh.milioni 20,ambapo katika awamu ya pili iliyogharimu sh.milioni 50  umehusisha ujenzi wa maabara,ukarabati wa nyumba ya Mwalimu Mkuu,ukarabati wa hosteli,ukarabati wa vyumba sita vya madarasa na ujenzi wa vyoo vya walimu na wanafunzi.

Kulingana na Mnwele  madarasa sita kila moja  lina uwezo wa kuchukua wanafunzi 40 ambapo madarasa yote yatakuwa na uwezo wa kuchukuwa wanafunzi 240 na kwamba hadi sasa madarasa matatu yamekamilika kwa asilimia 85,madarasa matatu yamefikia asilimia 60,nyumba ya Mkuu wa shule na hosteli imefikia asilimia 80.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbinga Cosmas Nsenye akizungumzia mradi huo,amesema Halmashauri zote mbili za wilaya hiyo ambazo ni Mbinga Mji na Halmashauri ya Wilaya zina ushirikiano mkubwa  hali ambayo imesababisha kuwa na shule mbili maalum za wasichana na wavulana.

“Naomba Wilaya na Halmashauri nyingine nchini waige mfano wa wilaya ya Mbinga kwa kuanzisha sekondari za vipaji maalum ndani ya Halmashauri husika,hizi ni sekondari za bweni ambazo zina mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia’’,alisisitiza Nsenye.

Kwa upande wake Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Musa Homera akizungumza mara baada ya kukagua shule hiyo ameupongeza uongozi mzima wa Halmashauri hiyo kwa kuanzisha shule hiyo ambayo  itasaidia kuboresha elimu kwa watoto .

Amesema serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli katika kipindi cha miaka mitano imepata mafanikio makubwa katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo ya shule.

“Tangu mwaka 1961 tumepata uhuru,katika kipindi cha miaka mitano hii kuanzia mwaka 2015 hadi 2020,miradi iliyotekelezwa Tanzania karibu inalingana na miradi iliyoanzishwa kuanzia mwaka 1961 hadi mwaka 2015,Rais wetu amefanyakazi kubwa sana’’,alisisitiza Homera.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari wa Mkoa wa Ruvuma

Julai 7,2020

Mbinga

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.