• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WILAYA ya Nyasa ilivyojipanga kuongeza ufaulu shule za msingi

Imewekwa kuanzia tarehe: February 19th, 2020

Ofisa Elimu Msingi wa Wilaya ya Nyasa Said Kalima, amewataka walimu wakuu na Maafisa Elimu Kata, kuwasimamia walimu   ili wafundishe kwa bidii ili kupandisha ufaulu Wilayani hapa.

Maagizo haya aliyatoa jana, wakati akiongea na walimu wakuu wote, na Maafisa Elimu Kata  Wilayani  hapa, walipokuwa wakifundishwa kutumia mfumo wa premu, katika Ukumbi wa wa kisasa wa Kassimu Majaliwa, uliopo katika Shule ya Sekondari Mbamba-bay Wilayani nyasa kwa lengo la kuwekeana mikakati ya kuhakikisha ufaulu unapanda kwa 100% (asilimia mia moja).

Bwana Kalima alifafanua kuwa, imefika wakati kila mwalimu atambue wajibu na majukumu yake na kufanya kazi kwa bidii, ili kupandisha ufaulu katika Wilaya ya Nyasa. Walimu wakuu na Maafisa Elimu Kata ni Wasimamizi wakuu wa kila siku wa kuhakikisha walimu wanajituma, na kufanya kazi ya kufundisha wanafunzi kwa bidii, kwa kuwa kila mwalimu akisimamiwa vizuri na akatekeleza majukumu yake,  Ufaulu nyasa utapanda na kufikia100% (asilimia mia moja).

Aliongeza kuwa hatasita kuchukua hatua za haraka kwa mwalimu mkuu yeyote atakayeshindwa kusimamia ufaulu katika Shule yake, kwa kuwa atafanya ukaguzi wa kushtukiza katika shule zote wilayani hapa, ili kubaini mapungufu, na kuchukua hatua mara moja ikiwa ni pamoja na kumshusha madaraka mwalimu, mwalimu mkuu au Ofisa Elimu kata na kumchukulia hatua za kinidhamu ikiwa ni pamoja na hatua zaidi za kiutumishi.

“Nachukukua Fursa hii kuwaagiza ninyi Maafisa Elimu Kata na Walimu wakuu, kuhakikisha kuwa mnawasimamia walimu wenu, na kuhakikisha wanafanya kazi kwa juhudi na maarifa. Kwa kuwa nyie ni viongozi katika maeneo yenu.  Mkihakikisha mnatekeleza majukumu yenu katika shule na Kata zenu Halmashauri hii itakuwa na ufaulu mzuri, na kuhakikisha tunafika asilimia mia moja. Ukiwa na cheo hakikisha unakitumia vizuri, kwa lengo la kuisaidia jamii. Kama hawa wanafunzi wakifaulu kwa 100% (asilimia mia moja) unakuwa umefuta ujinga kwa wananchi wengi na unakuwa umeipa maendeleo jamii. Nitawachukulia hatua mara moja endapo nikipata taarifa ya mwalimu mtoro, mvivu, au asiyewajibika ipasavyo,”. Alisema Kalima

Aidha aliwaagiza viongozi hao kutoa taarifa za haraka na mapema kukiwa na matukio ya walimu watoro,wavivu na wasioshirikiana na viongozi hao au kutokutekeleza maagizo kwa wakati naye atachukua hatua mara moja.

Ofisa Elimu huyo aliwaagiza walimu wakuu na maafisa Elimu kata kuhakikisha wanafanya mazoezi/majaribio ya siku,wiki,mwezi, na mitihani ya Kata ya ujirani mwema na Wilaya kwa madarasa ya Mitihani ili kuwaweka sawa wanafunzi ili waweze kujiandaa vema na mitihani.

Aidha, katika hatua nyingine alimpongeza mh Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania John pombe Magufuli kwa kuhakikisha miundombinu ya Elimu ya Wilaya ya Nyasa inavutia na kuwa rafiki kwa mazingira ya kujifunzia.Hivyo alitoa siku saba kuhakikisha walimu wakuu wote waliopokea fedha za ujenzi wa miundombinu inakamilika.

“Mh Rais ametupendelea sana wana Nyasa,ametupa fedha  za kujengea miundombinu ya Elimu na anatoa Elimu bila malipo, hata ukipita kwenye shule zetu za msingi madarasa yanapendeza na vyoo pia vinapendeza, kwa hiyo kazi iliyobaki ni kumuenzi kwa kuhakikisha ufaulu unakuwa kwa 100% (asilimia mia moja) kwa Wilaya ya Nyasa kwa mwaka 2020 na kuendelea” Alisema Kalima.

Imeandaliwa na

Netho sichali

 Kaimu Afisa habari (w) Nyasa 0767417597

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.