• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WIZARA ya Kilimo ilivyotekeleza zoezi la upimaji udongo Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: March 22nd, 2025

Katika juhudi za kuhakikisha ardhi ya Tanzania inatumiwa kwa tija zaidi, Wizara ya Kilimo kupitia Kitengo cha Matumizi Bora ya Ardhi imepewa jukumu la kupima afya ya udongo nchi nzima.

 Zoezi hili linafadhiliwa na mkopo kutoka Benki ya Dunia (World Bank) na linahusisha upimaji wa hali ya afya ya udongo ili kuzalisha ramani zitakazobainisha aina za udongo, kutoa mapendekezo juu ya ardhi inayofaa kwa kilimo, mazao yanayofaa kwenye maeneo husika pamoja na aina za mbolea zinazokidhi mahitaji ya udongo huo.

Kutokana na umuhimu wa Mkoa wa Ruvuma kama mzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula, Wizara ilianza zoezi hili katika mkoa huo. Timu ya wataalamu wabobezi hamsini (50) iliundwa kutoka taasisi mbalimbali.

 Taasisi hizo ni Pamoja na Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), Chuo Kikuu cha Nelson Mandela, pamoja na watafiti waliopo na wastaafu wa masuala ya afya ya udongo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) Mlingano Tanga na Uyole.

 Pia, wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo kupitia Idara ya Matumizi Bora ya Ardhi walihusika katika utekelezaji wa zoezi hili.

Timu ya wataalamu iliwasili mkoani Ruvuma mnamo Septemba 2024 na kuanza kazi ya uchukuaji wa sampuli za udongo kwa kutumia mwongozo wa picha za satelaiti na "coordinates".

 Halmashauri na vijiji vyote vya Songea Vijijini na Manispaa, Nyasa, Mbinga Mji, Mbinga Vijijini, Tunduru na Namtumbo vilihusika katika zoezi hili.

Hata hivyo, kutokana na ufinyu wa bajeti, Halmashauri ya Madaba haikuweza kushirikishwa, lakini mipango ipo kwamba sampuli za udongo kutoka eneo hilo zitakusanywa kupitia mradi mwingine utakaotekelezwa mkoani Njombe.

Baada ya sampuli kukusanywa, zilipelekwa maabara kwa ajili ya uchambuzi zaidi ili kuhakikisha zoezi la upimaji linafanikiwa. Lengo kuu ni kusaidia wakulima wa Tanzania kupata taarifa sahihi kuhusu udongo wao, hivyo kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu aina ya mazao ya kupanda na mbolea zinazofaa kwa matumizi yao.

 Hii ni hatua muhimu katika kuboresha kilimo na kuongeza uzalishaji wa mazao kwa tija zaidi.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.