• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

AKINAMAMA Nyasa washerekea baada ya kukabidhiwa gari la kubebea wagonjwa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 16th, 2020

Akina mama  wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma wamesema wamepata hamu ya kuzaa, baada ya kukabidhiwa rasmi Gari ya kubebea wagonjwa ya Kituo cha afya Mbamba-bay.

Gari hiyo imekabidhiwa jana katika Kituo cha afya cha Mbamba-bay Wilayani hapa na Mbunge wa Jimbo la Nyasa Mhandisi Stela Manyanya ambaye pia ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara na kupokelewa na Uongozi wa Kituo cha afya Mbamba-bay Wilayani hapa.

Akinamama hao walimueleza mbunge kuwa ,Hamu ya kuzaa imeongezeka kutokana na kupewa gari mpya ya kubebea wagonjwa, kwa kuwa mwanzo walikuwa wakikumbana na adha ya Uzazi pale wanaposhindwa kujifungua na kulazimika kupata gharama nzito ya kukodi gari ili kwenda, Hospitali kubwa kwa uchunguzi zaidi.lakini kwa sasa, hawana tena wasiwasi kwa kuwa gari ipo.

“Tunaishukuru sana Serikali ya Rais John pombe magufuli, na mbunge wetu wa Nyasa  kwa kutuletea gari ya Wagonjwa   katika kituo chetu cha afya cha Mbamba-bay, Awali tulikuwa hatuna hamu ya kuzaa kwa kuwa tulikuwa tukuhofia usalama wetu wa afya ya uzazi kama tulikuwa tukipata matatizo ya Uzazi kulikuwa hakuna usafiri wa uhakika wa kutufikisha hospitali kubwa lakini kwa sasa Hamu ya kuzaa imeongezeka kutokana na kukabidhiwa gari jipya ambalo tumekabidhiwa leo”.alisema mariana Kapinga

Awali akitoa Taarifa fupi  ya Kituo cha Afya kwa Mgeni Rasmi Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mbamba-bay Michael Mabisi alisema Kituo hicho kwa sasa kinaendelea vizuri na changamoto nyingi za vifaa tiba na vitendea kazi viko katika Hali nzuri na kumpongeza Mh. Mbunge kwa mchango mkubwa wa kukiboresha Kituo cha Afya cha Mbamba-bay na Wilaya ya Nyasa kwa ujumla wake.

“Mh Mbunge sisi wafanyakazi wa kituo cha Afya Mbamba-bay tunatambua mchango wako wa hali na mali wa kuboresha sekta ya Afya, Hususani kuboresha Kituo hiki kwa kutatua changamoto nyingi zilizokuwa inakikabili na Leo hii umetukabidhi gari la Wagojwa tunakushukuru sana.Kama wafanyakazi tunatembea kifua mbele kwa kwa tuna Mbunge anayejali Watumishi, anayejali afya ya Jamii”Alisema Dkt  Mabisi.

Akikabidhi Gari ya Wagojwa Mbunge wa Nyasa Mhandisi Stela Manyanya,  Alisema anamshukuru Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe magufuli kwa kuwajali wananchi wa Nyasa , kwa kutupa miradi mbalimbali ya Afya kwa kuwa tumejengewa Hospitali ya Wilaya na Vituo vya afya vya Mkili, Kihagara, Kingerikiti na Kuboresha Miundombinu ya Vifaa tiba ,na Miradi mingine mingi ya Maendeleo kwa Wilaya ya Nyasa.Inaonyesha ni jinsi gani anatupenda Wananyasa na leo hii ametupatia gari ya Wagonjwa mpya ambayo itasaidia kubeba wagonjwa na shughuli zingine za Afya.

Amewataka Uongozi wa Afya kituoni hapo kulitunza gari hilo ili liweze kuwa zima muda wote kwa kuwa gari ni mali ya Wananchi na Dereva atakayepata alitunze atembeze kwa uangalifu na kutunza Siri za akina mama hao.

Imeandaliwa na Netho c. Sichali, 0767417597/0623714299

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • AMEUONA Mwenge Songea baada ya miaka 63 ya Uhuru

    May 14, 2025
  • MWENGE wa Uhuru watingisha Manispaa ya Songea,wapitia miradi ya bilioni 1.8

    May 14, 2025
  • MWENGE wa Uhuru wakagua jengo la OPD zahanati ya Jimbo katoliki Mvinga

    May 14, 2025
  • MWENGE wa Uhuru wakagua mradi wa jengo la OPD zahanati ya Jimbo Katoliki Mbinga

    May 14, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.