• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

CHAMA cha Msingi cha Ushirika Kingerikiti Nyasa chatoa elimu ya kilimo bora za kahawa

Imewekwa kuanzia tarehe: August 2nd, 2020

KINGERIKITI AMCOS YATOA ELIMU YA KAHAWA KWA WAKULIMA

Chama cha  cha Ushirika cha Msingi cha  Mazao na  Masoko cha Kingerikiti (Amcos),  kwa kushirikiana na Wafadhili wa chama hicho kutoka Nchini Marekani kupitia Shirika la USADF,  Hivi karibuni  Kimetoa Mafunzo kwa wakulima wa kahawa, yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kuzalisha na kuandaa kahawa bora ili kuongeza kipato kwa Mkulima.

Mafunzo hayo ya siku mbili, yametolewa katika Ofisi za Chama, zilizopo Katika Kijiji cha Kingerkiti, Kata ya Kingerikiti Wilaya ya Nyasa, na yametolewa na wakufunzi kutoka Shirika la Sturbucks yenye lengo la kuwafundisha wakulima namna ya kulima, kuitunza na kuandaa kahawa yenye Ubora ili kuifikisha Sokoni.

Akifungua Mafunzo hayo Afisa Ushirika wa Wilaya ya Nyasa Bw.Menance  Ndomba alikipongeza chama hicho kwa kutoa  mafunzo kwa wakulima yatakayowawezesha Wakulima,  kukabiliana na wadudu waharibifu wa zao la kahawa  ambalo pia ni zao la  Kimkakati.

Aidha ametoa Wito kwa wanaushirika kushikamana, ili kuuendeleza Ushirika kwa kuwa ndiyo nguzo pekee kwa Wakulima wa Zao la Kahawa ambayo huwawezesha kuunganisha nguvu zao wakati wakuyafikisha mazao yao sokoni na kuhakikisha chama kinakwenda vizuri kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana hivyo wana kila sababu ya kushikamana.

“Ndugu zangu wanaushirika wa Chama Cha Msingi cha Mazao cha Kingerikiti, Nichukue Fursa hii kuwapongeza Viongozi wa Chama na wafadhili wa Chama hiki, USADF kwa kutoa mafunzo ambayo yanawajengea uwezo wakulima namna ya kulima, kupambana na wadudu waharibifu na kuiandaa kahawa bora itakayo washawishi  wanunuzi, wanunue kahawa iliyokuwa na viwango vinavyokubalika na kwa bei nzuri, Aidha napenda kuwafahamisha rasmi kwamba kufuatia mafunzo haya mmeanzisha rasmi mchakato wakuyafikia masoko maalumu na kwa sasa tunajisajiri SOKO la CAFÉ Practice  Nasema ahsante sana, Nitoe Wito kwa wanachama wa Chama hiki kushirikiana na kuendeleza Ushirika huu kwa kuwa Vyama vingi  vikishapata mafanikio basi kutoelewana kunaanza kwa lengo la kuvuruga Ushirika, ” Alisema Ndomba.

Bw Ndomba aliyataja mafanikio yaliyopatikana Kingerikiti Amcos ni pamoja na kuwa na Mfuko wa Pembejeo wenye thamani ya milioni 38 ambao huwakopesha wakulima pembejeo na kulipa kipindi cha mavuno hali iliyosababisha kuongezeka kwa uzalishaji kutoka tani 10.3 mwaka 2017/2018 hadi kufikia tan 360.34 kwa Msimu wa mwaka 2019/2020. Mafanikio mengine nikukarabati ofisi na kununua vifaa vya ofisi, na kununua Mtambo wa kuchakata kahawa wenye thamani ya miliono 47.

Naye Mkufunzi wa mafunzo hayo  kutoka Shirika la Sturbucks Bi Bahati Mlwilo amesema mafunzo yaliyotolewa kwa wakulima yamewajengea uwezo wa kulima kahawa ya Kisasa, kupambana na Wadudu wanaoharibu kahawa,  namna ya kupambana na magonjwa ya kahawa.lakini pia wamejifunza namna ya kuiandaa na kuifiiksha kahawa yenye ubora na kuongeza kipato kwa kaya na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wao Washiriki wa mafunzo hayo Samweli Kinunda na Severine Mbunda,  waliwapongeza wafadhili pamoja na viongozi wa Chama hicho, kwa kuandaa Mafunzo hayo ambayo yamewasaidia kutambua Changamoto katika zao la kahawa kwa kuwa awali walikuwa wanalima kienyeji na kupata mazao kidogo yasiyo na ubora,  lakini kwa sasa watatumia mafunzo waliyopewa kuboresha na kuitunza kahawa na kuipeleka kiwandani ikiwa na ubora wa hali ya juu ili kujiongezea kipato.

Imeandikwa na Netho Credo

Afisa Habari Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.