• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ELIMU na vifaa vya WWF vilivyowawezesha wananchi Tunduru kuwadhibiti tembo waharibifu

Imewekwa kuanzia tarehe: October 8th, 2021

SHIRIKA la  kimataifa la Uhifadhi (WWF),limetoa elimu na vifaa katika vijiji vitano vilivyoathirika na tembo waharibifu wa mazao Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma,ili kuwadhibiti wanyama hao.

Mhifadhi kutoka  WWF Deogratias Kilasara amevitaja vijiji vilivyonufaika na mradi huo kuwa ni Misiaji, Mpanju, Malumba,Mbati na Machemba ambapo amesisitiza WWF imedhamiria kuhakikisha tembo waharibifu wanadhibitiwa bila madhara.

‘’Wilaya ya Tunduru imekuwa na matukio mengi ya tembo waharibifu wanaovamia maeneo ya mashamba na makazi ya binadamu,WWF inashirikiana na wadau wengine kuhakikisha kuwa haya matukio yanapungua kwa kutoa elimu na vifaa vya kukabiliana na tembo’’,alisisitiza.

Amesema katika msimu uliopita WWF ilitoa elimu ya matumizi ya pilipili na uzio wa kitambaa kwa kutumia mafuta machafu na kutoa matokeo mazuri ambapo amekitaja kijiji cha Misiaji kuwa cha mfano wa kuweka uzio kuzui tembo katika mashamba.

Hata hivyo amesema WWF imetoa mabomu 400 ya kufukuza tembo waharibifu wilayani Tunduru kwa ajili ya matumizi msimu ujao wa kilimo.

Wakizungumza namna walivyonufaika na elimu ya kukabiliana na tembo waharibifu wa mazao katika msimu uliopita,wananchi wa kijiji cha Misiaji Tunduru wamelishukuru Shirika la WWF kwa elimu hiyo ambayo imewawezesha kuvuna mazao yao bila kuathiriwa na tembo.

Said Amigo Mkazi wa Misiaji Tunduru amesema  baada ya kupata elimu,aliweka  uzio wa pilipili kwenye shamba lake la mahindi na viazi ambapo amefanikiwa kuvuna mahindi gunia 36 na viazi  anaendelea kula hadi sasa na kwamba tembo wanafika lakini hawaingii kwenye mashamba yake.

Rashid Kassim Mkazi wa Misiaji na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Chingoli Tunduru amesema katika msimu uliopita walifanikiwa kufunga uzio wa pilipili kwenye mashamba ya vijiji vya Misiaji  na Malumba kupitia ufadhili wa WWF na kwamba tembo walipofika kwenye mashamba yenye uzio hakuna shamba lililoshambuliwa.

Amesema wakulima kutoka vijiji hivyo wameamini na kuridhika kuwa pilipili na mafuta machafu ni kiboko ya tembo waharibifu wa mazao kwa sababu mazao yao yamesalimika.

Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Agustino Maneno  amewapongeza WWF kwa mafunzo ya kukabiliana na tembo waharibifu ambayo yamewawezesha wananchi kuvuna mazao yao katika msimu uliopita.

“Nawapongeza sana kwa msaada wa mafunzo na mabomu 400 ya kufukuza tembo waharibifu,hata hivyo kwa ukubwa wa wilaya na changamoto iliyopo kwa mwaka walau tunahitaji mabomu 200 kukabiliana na tembo waharibifu’’,alisema.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kusini Mheshimiwa Daim Idd Mpakate  amewashukuru WWF kwa kutoa elimu na vifaa vya kukabiliana na tembo waharibifu ambapo amesema idadi ya tembo watapungua na kwenda kwenye maeneo yao ya asili .

Mbunge wa Tunduru Kaskazini Mheshimiwa Hassan Myao ametoa rai kwa WWF kushirikiana na TAWA TANAPA,TFS na wadau wengine wa mazingira kutafuta njia nyingine mbadala za kukabilina na tembo waharibifu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 8,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.