• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

HOSPITALI YA RUFAA Ruvuma kutumiwa na nchi jirani

Imewekwa kuanzia tarehe: May 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed  amesema serikali inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo katika Mkoa wa Ruvuma ikiwemo ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa ambayo ujenzi wake unaendelea katika eneo la Mwengemshindo Manispaa ya Songea.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Ruvuma Manispaa ya Songea kwenye tamasha la JIKUNE lililoandaliwa na Kituo cha redio cha Selous FM,Kanali Abbas amesema hospitali ya Rufaa ya Mkoa licha ya kutumiwa na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma,pia inaweza kutumiwa na wananchi kutoka  nchi Jirani za Msumbiji,Malawi na Komoro.

Ameitaja baadhi ya miradi iliyotekelezwa katika sekta ya afya kuwa ni ujenzi wa zahanati,hospitali  za wilaya, nyumba za watumishi,ununuzi wa vifaa na vifaatiba vya kisasa ambapo hivi sasa kuna xray na CT Scan kubwa  na za kisasa hivyo kurahisisha matibabu na kuokoa Maisha.

Ameitaja miradi mingine ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa mkoani Ruvuma kuwa ni  ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kitai- Ruanda wilayani Mbinga hadi Lituhi wilayani Nyasa.

“Barabara hiyo licha ya kutumika kusafirisha watu,lakini pia itasaidia usafiirishaji katika migodi mikubwa ya makaa ya mawe ya Kampuni za JITEGEMEE,TanCoal na Ruvuma Coal kwa sababu kwa kiwango kikubwa makaa ya mawe ni lazima yasafirishwe Kwenda kwenye bandari zetu  za Mtwara,Dar es salaam na Tanga ili yaweze Kwenda nje ya nchi na kuiwezesha serikali kupata mapato’’,alisema Kanali Abbas.

Akizungumzia mradi wa utoaji mbolea ya ruzuku,Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma amesema mbolea hiyo ikitumiwa vizuri itawezesha kuzalisha chakula cha kutosha ndani ya Mkoa na ziada Kwenda kuuzwa kwa majirani zetu na mikoa mingine.

Amesisitiza kuwa Mkoa wa Ruvuma gwiji la uzalishaji wa mazao ya nafaka  na kwamba Mkoa unafahamika kama ghala la chakula la Taifa kutokana na kuongoza kitaifa katika uzalishaji.

Katika sekta ya elimu Mkuu wa Mkoa amesema serikali imetoa fedha kutekeleza ujenzi wa shule na madarasa katika shule za awali,msingi, sekondari,ujenzi wa nyumba za walimu na kwamba katika Mkoa wa Ruvuma serikali imetoa fedha za kujenga sekondari maalum ya wasichana ya Mkoa  wilayani Namtumbo.

Sekondari hiyo ambayo imesajiriwa jina la Dkt.Samia Suluhu Hassan imeanza kuchukua wanafunzi wa kike wa kidato cha tano na kwanza   ambapo hadi sasa serikali imetoa Zaidi ya shilingi bilioni nne kutekeleza mradi huo.

Akizungumzia sekta ya kilimo,Kanali Abbas amesema Mkoa umezindua mnada wa kwanza wa ufuta,mnada ambao umefanyika kwa kutumia teknolojia  ya kidijitali inayomwezesha mnunuzi kuomba kununua ufuta hata akiwa nje ya Mkoa.

Amebainisha kuwa mfumo huo humwezesha mtu kununua mazao akiwa Ulaya au Mkoa wowote  na kwamba uzinduzi huo wa mfumo umeonesha bei nzuri ya mazao ya mkulima kwa sababu mfumo unaanza na bei elekezi na baadaye mnunuzi ananunua kulingana  bei iliyoanza kutamkwa na Wizara ya Kilimo.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.