• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

JIWE la Pomonda ziwa Nyasa lina vivutio vya kila aina

Imewekwa kuanzia tarehe: January 21st, 2021

KAMA unadhani jiwe la Mwanza lililopo katika ziwa Viktoria ndiyo kivutio pekee cha utalii katika maziwa hapa nchini utakuwa unajidanganya.

Katika ziwa Nyasa Mkoa wa Ruvuma kuna jiwe linaloitwa Pomonda ambalo linavivutio lukuki vya utalii ambavyo vinavutia wengi waliobahatika kufika katika jiwe hilo.Jiwe la Pomonda lenye ukubwa wa robo hekari ambalo lipo meta takribani 300 ndani ya ziwa Nyasa  kutoka bandari ya Liuli.

Muongozaji watalii katika bandari ya Liuli Joseph Ndomondo ambaye pia ni Mmiliki wa fukwe ya Pomonda anasema Jiwe la Pomonda ambalo wajerumani walilipa jina la sphinxhaven kutokana na kuwa na vivutio lukuki.

Utalii wa kihistoria ni aina ya kwanza ya utalii ambayo inapatikana katika jiwe hilo ambapo tangu vita ya kwanza ya dunia mwaka 1914 hadi 1918  na vita ya pili ya dunia mwaka 1939 hadi 1945  wakoloni walitumia jiwe hilo kujificha.

Anasema wajerumani na waingereza walitumia pango kubwa lililopo katika jiwe la Pomonda ambalo lipo kama ukumbi wenye kubeba watu kati ya 60 hadi 100 hivyo wanajeshi  wa kiingereza na kijerumani walitumia jiwe hilo kama sehemu ya kujificha wakati wa  mapambano.

Katika jiwe hilo inaaminika kuna sahihi ya Dk.David Livingstone Mvumbuzi maarufu ambaye alivumbua milima Livingstone ambayo pia imepewa jina lake kuzunguka ziwa Nyasa.

Dk.Livingstone alizaliwa huko Blantyre,Uingereza Machi 19 mwaka 1813.Alisoma masomo ya udaktari wa binadamu katika Chuo Kikuu cha Cambridge.Alifanya safari za kuja Afrika mara tatu kwa nyakati tofauti.

Ilikuwa ni mwaka 1866 ambapo Dr. Livingstone alikuja Afrika kwa mara ya tatu.Lengo la safari yake lilikuwa ni kuchunguza chanzo cha mto Nile.Safari yake ilianzia katika chanzo cha mto Ruvuma, Mikindani Mtwara hadi ziwa Nyasa, Banguela na Mweru.

Uchunguzi ambao umefanywa katika Jiwe la Pomonda umebaini kuwa kilele cha jiwe hilo ambacho kina urefu wa takribani meta 40 kwenda juu ipo taa maalum  kubwa yenye rangi nyekundu ambayo ilikuwa itatumiwa  na nchi tatu za Tanzania,Malawi na Msumbuji.

Taa hiyo ilitumika wakati wa wakoloni wa kijerumani,kireno na waingereza kwa ajili ya alama ya kuongozea meli katika ziwa Nyasa ili wasiweze kupotea  wanapotaka kutia nanga kwenye bandari ya Liuli,taa hiyo iliwawezesha kuiona bandari ya Liuli  hata wakiwa katika nchi za Malawi na Msumbiji.

Kivutio kingine cha utalii ambacho kinapatikana katika eneo la jiwe hilo ni mawe matatu makubwa ambayo wakazi wa eneo hilo wanaamini yamepangwa na Mwenyezi Mungu ,huku mpangilio wake ukiwa ni kivutio cha ajabu utadhani yamejengwa na mafundi ujenzi huku yakiwa yameacha njia maalum ambayo unaweza kupita kwa mtumbwi au boti kutokea upande wa pili hali ambayo inawashangaza na kuwavutia wengi.

Jiwe la Pomonda pia ni sehemu muhimu ambayo inafaa kufanya utalii wa michezo ya kwenye maji(water sports) kwa mfano mchezo wa kupiga mbizi  na  kuruka toka juu ya jiwe la Pomonda hadi ziwani umbali  wa karibu mita 30.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.