• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MAAMBUKIZI ya malaria Manispaa ya Songea yafikia asilimia 5.9

Imewekwa kuanzia tarehe: April 30th, 2021

Mstahiki Meya Manispaa ya Songea Michael Mbano ameongoza mamia ya Wananchi Manispaa ya Songea katika kuadhimisha siku ya Malaria Duniani ambayo huadhimishwa duniani kote kila  mwaka  ifikapo tarehe 25 aprili  yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi matarawe yaliyoambatana na zoezi la upimaji BURE wa Malaria  ambapo watu 88 walipata kupimwa kati ya hao watu 3 walikutwa na malaria na kupewa matibabu.

 Mbano ambaye  pia ni  Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Manispaa ya Songea katika hotuba yake iliyosomwa viwanjani hapo alisema” ushiriki hafifu  wa jamii katika kuboresha mazingira ya makazi na kutoondoa mazalia ya mbu ni chanzo kikuu cha ongezeko la maambukizi ya malaria kwa jamii.”

Alisema lengo la Serikali katika kuadhimisha maadhimisho haya  kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji, usimamizi, na tathimini ya mwenedo wa ugonjwa wa malaria ambao kwa mwaka 2020 hali ya maambukizi Manispaa ya Songea ni  asilimia 5.9% ikiwa Kimkoa ni asilimia 11% na Kitaifa ni  asilimia 7%.

Aliongeza kuwa,  baadhi ya tabia za  jamii  kutokuchukua hatua za haraka za kupata matibabu kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, kutozingatia matumizi sahihi ya vyandarua, na kutopata vipimo  vya malaria kabla ya  matibabu ni moja ya changamoto ambazo hukwamisha mapambano dhidi ya malaria.

Amewataka wananchi hao kuboresha mazingira yao ya makazi kwa kufanya usafi wa mazingira na ujenzi wa nyumba bora, kuwahi matibabu mara waonapo dalili za ugonjwa, kupata vipimo vya malaria kabla ya matibabu kwani sio kila homa ni malaria.

Katika kupambana na malaria Mstahiki Meya manispaa ya Songea,  amegawa   chandarua 20 kwa watu wenye mahitaji maalumu  waishio katika kata ya Matarawe Manispaa ya Songea.

Ametoa Rai kwa wataalamu wa Manispaa ya Songea kufanya kazi kwa weredi sambamba na kutoa elimu kwa jamii juu ya kubadili tabia zinazochangia maambukizi ya ugonjwa wa Malaria kwa kutumia wahudumu wa afya ngazi za mitaa kwa kushirikiana na wataalamu wa idara ya afya,  kutoa tiba ya tahadhari kwa wa mama wajawazito wahudhuriapo kiliniki pamoja na kuendelea kuchukua hatua za kisheria kwa wakazi wanaokiuka taratibu, kanuni na sheria za Afya na ustawi wa mazingira.” Mbano alisisitiza”.

Naye Mratibu wa Malaria Manispaa ya Songea Maxensius Mahundi alisema Malaria ni miongoni mwa magonjwa 10 yanayoongoza kwa matibabu ya nje na ndani kwa watoto walio chini ya miaka mitano 5 na akinamama wajazito.

Akizitaja dalili za ugonjwa huo ni pamoja na homa,maumivu ya viungo, mwili kulegea, kichwa kuuma, baridi na kutetemeka mwili, kutapika, kuharisha, maumivu ya kifua, kukosa hamu ya chakula, kuvimba wengu, kuvimba bandama, degedege na upungufu wa damu.

Mahundi alibainisha kuwa mwaka 2020 Manispaa ya Songea walioripotiwa kuugua ugonjwa wa malaria na kupata matibabu nje ni 19,929 sawa na asilimia 7.2% ya wagonjwa wote 276,063 waliopata matibabu nje, aidha  waliolazwa kwa ugonjwa wa Malaria mwaka 2020 ni 1,785 sawa na asilimia 11.7% ya wagonjwa wote 15,219 waliolazwa.

Aliongeza kuwa watoto chini ya miaka 5 walioripotiwa ugonjwa wa malaria na kutibiwa kwa matibabu ya nje ni 5,976 sawa na asilimia 2.2 ya wagonjwa 270,087 ya waliotibiwa magonjwa mengine pia watoto chini ya miaka 5 waliopata matibabu ya ndani 3,846 kati ya hao watoto 645 walitibiwa na kulazwa kwa ugonjwa wa malaria sawa na asilimia 16%.

Vifo vilivyoripotiwa dhidi ya ugonjwa wa malaria mwaka 2020 ni 11 sawa  na asilimia 37.9% ya vifo vyote 29 vilivyoripotiwa kwa magonjwa mengine.  Vifo vya Watoto chini ya miaka mitano  ni vifo 5 sawa na asilimia 62.5% ya vifo vyote 8 vya watoto chini ya miaka mitano.

Mahundi alifafanua kuwa hali hiyo inatokana na baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Songea kutofuata maelekezo ya matumizi sahihi ya vyandarua, kutopima kwa uthibitisho, kutozingatia matibabu sahihi, na akina mama wajawazito kutowahi kliniki mara anapohisi kuwa ana ujauzito pamoja na kuchelewa kupata tiba za tahadhari.

Ili kukabiliana na changamoto hizo, Manispaa ya Songea imeweka mpango wa kupulizia dawa za  kuuwa viluilui vya mbu kwenye mazalia ya mbu ambapo kwa mwaka 2020 Manispaa ya Songea ilipulizia mazalia ya mbu mita za mraba 11088, pamoja na kuendelea kusambaza chandarua mashuleni kila mwaka mbapo 2020 viligawiwa vyandarua 19,860 kwa shule za Msingi 85 kwa darasa la 1,2,3,5 na la 7  pamoja na uendeshaji wa usafi kila mwisho wa mwezi.

Akitoa shukrani kwa wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali PSI, MSD kupitia kampuni ya Simba Logistic katika kupambana na ugonjwa malaria  Manispaa ya Songea.

Kauli mbiu ya mwaka 2021  ya Maadhimisho ya siku ya Malaria Duniani  ni;  

 “ZIRO MALARIA INAANZA NA MIMI, NACHUKUA HATUA KUITOKOMEZA”.

Imenadikwa na Amina Pilly

Afisa Habari Manispaa ya Songea

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.