• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MATOGORO mlima wa maajabu unaobeba chanzo cha Mto Ruvuma na siri nzito ya vita ya Majimaji

Imewekwa kuanzia tarehe: July 13th, 2025

Na Albano Midelo

Ukitafuta mahali pa kutuliza akili, kukutana na historia ya kweli, kushuhudia maajabu ya maumbile, na kusikia sauti ya asili ikizungumza na moyo wako, basi jibu lipo katika Msitu wa Hifadhi ya Matogoro Mashariki.

Takriban kilomita 15 kutoka katikati ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, unapokaribia milima ya Matogoro, upepo unaanza kubeba harufu ya miombo, milio ya ndege wa porini na upekee wa mazingira ambayo hayajaguswa na mikono ya uharibifu.

 Huu si msitu wa kawaida ni nyumba ya historia, chemchemi ya mito mikuu, na mahali ambapo roho ya vita ya Majimaji bado inanong’ona kwenye mapango ya matambiko.

Mlima Uliojaa Hazina ya Kipekee

Kwa mujibu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Msitu wa Matogoro Mashariki ulitangazwa rasmi kuwa Hifadhi ya Taifa mnamo Novemba 6, 1951 kwa Tangazo la Serikali Na. 260. Awali ulikuwa na ukubwa wa hekta 3,533, lakini baada ya upimaji mpya sasa unaenea kwa hekta 7,457, ukiwa ni moja ya maeneo makubwa zaidi ya hifadhi ya asili mkoani Ruvuma.

Msitu huu unajumuisha milima mikubwa yenye miteremko mikali, mabonde ya kina, na vilele vya mawe vilivyopo kati ya mita 1,800 hadi 2,150 kutoka usawa wa bahari. Kilele chake cha juu kipo kwenye urefu wa mita 2,051, na ndiyo sehemu ya juu kabisa katika mkoa wa Ruvuma – kivutio kikubwa kwa wapenda mandhari na wapiga picha wa asili.

 Chanzo cha Mito Mikuu na Uhai wa Maelfu

Msitu wa Matogoro unashangaza. Hapo ndipo Chanzo cha Mto Ruvuma kinapopatikana — mto unaoelekea Bahari ya Hindi na kutenganisha Tanzania na Msumbiji.

Pia kuna Mto Luhira unaotiririsha maji hadi Ziwa Nyasa. Ndani ya msitu huo, kuna mito midogo kama Liwoyowoyo, Lipasi, Mkurumusi, Limbyanda, na Masumela, yote ikianza safari yake kutoka vyanzo vya milimani baraka kwa wakazi wa mabondeni wanaotegemea kwa kilimo, malisho na matumizi ya nyumbani.

 Aina Adimu za Viumbe na Mimea

Matogoro si tu msitu  ni hifadhi ya maisha. Kuna misitu ya miombo, msitu wa mito, na hata mashamba ya miti ya kupandwa. Ndani yake wanaishi wanyama kama pundamilia wa milimani (klipspringers), digidigi, nyani, tumbili na hata chui. Wanyama  wakiwemo  mamba , chatu, swila, na kobra pia hupatikana. Aidha, ndege wa kuvutia kama vipanga na tai huruka juu ya miti kwa mandhari ya kupendeza.

 Mapango ya Vita na Matambiko

Juu ya kivutio cha asili, Matogoro ni nyumba ya historia. Kuna mapango yaliyotumiwa na wapiganaji wa Majimaji kati ya 1905 hadi 1907, walipojificha na kujiandaa kwa mapambano dhidi ya ukoloni wa Kijerumani. Leo hii, mapango haya bado yanatumika kwa shughuli za matambiko ya kimila  yakihifadhi roho za mababu na hadithi za kishujaa zisizopaswa kusahaulika

 Shughuli Bora za Utalii

Kama wewe ni mpenzi wa utalii wa kiikolojia, Matogoro ndiyo paradiso yako. Wageni wanaweza kufanya:Safari za kutembea kwa miguu (walking safaris),Kupanda milima (hiking),Kutazama ndege (bird watching),Shughuli za kitamaduni na matambiko,Picha za kipekee (photographic safaris),Sherehe na matamasha (ceremonies & festivals) na Elimu ya mazingira (eco-education)

Bei za kuingia Kwa Mtanzania ni Tsh 3,000 tu kwa mtu mzima, watoto ni nusu bei, na watoto chini ya miaka 5 ni bure kabisa. Kwa wageni wa nje, ni Tsh 30,000  thamani ndogo kwa utajiri mkubwa wa asili.

Matogoro ni Zaidi ya Msitu – Ni Nyumba ya Uhai na Historia

Matogoro si tu kivutio cha kijiografia — ni kiini cha uhai, kumbukumbu ya ukombozi, na shule ya asili kwa kizazi cha sasa na kijacho. Ni mahali ambapo historia ya Majimaji inakutana na chemchemi ya mito mikuu, mahali ambapo utalii unavikwa taji la maana halisi ya urithi wa taifa.

Katika enzi hii ya maendeleo ya haraka, kuna kila sababu ya kuilinda Matogoro sio kwa ajili ya sisi pekee, bali kwa vizazi vijavyo, ambavyo navyo vinapaswa kujifunza kupumua hewa ya usafi wa Matogoro, kusikiliza sauti ya mito yake, na kuandika historia mpya ya utalii wa Tanzania.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MATOGORO mlima wa maajabu unaobeba chanzo cha Mto Ruvuma na siri nzito ya vita ya Majimaji

    July 13, 2025
  • JIWE LA BWANA kivutio kinachoongoza kuvutia watalii wa picha Tunduru

    July 13, 2025
  • RUVUMA yafanya maajabu kitaifa katika sekta ya elimu

    July 13, 2025
  • MLIMA Chingoli wa Tunduru wafichua siri ya udongo wa dhahabu kivutio cha uwekezaji kwenye kilimo

    July 13, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.