• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma azindua maadhimisho ya siku ya mbolea duniani

Imewekwa kuanzia tarehe: October 11th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge amezindua maadhimisho ya siku ya mbolea duniani yaliyofanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Kabla ya kuzindua maonesho hayo RC Ibuge alikagua vibanda 41 vya washiriki wa maonesho ambayo yanafanyika kuanzia Oktoba 11 na kilele chake ni Oktoba 13.

Akizungumza na wananchi kwenye uzinduzi huo Mkuu  wa Mkoa wa Ruvuma,amesema Mkoa una chakula cha kutosha kwa muda mrefu ambapo katika msimu wa mwaka 2020/2021,Mkoa wa Ruvuma umezalisha tani 1,384,705 za mazao yote ya chakula na kuwa na ziada ya tani 894,960.

‘’Kwa zao la mahindi pekee uzalishaji ni tani 816,242 hivyo kuwa na ziada ya jumla ya tani 326,497 za mahindi’’,alisisitiza RC Ibuge.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma,amesema uzalishaji huo unaambatana na matumizi ya pembejeo bora ikiwemo mbolea .

Ameyataja mahitaji ya mbolea katika Mkoa wa Ruvuma kuwa ni jumla ya tani 50,521 kwa msimu wa  kilimo wa mwaka 2020/2021 ambapo mbolea zilizoingia na kutumika ni tani 43,000 na kwamba katika msimu wa kilimo wa mwaka 2021/2022 Mkoa unatarajia kutumia mbolea tani 50,521 za aina zote za mbolea.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Dkt.Stephano Ngailo  ameutaja mkakati mkuu wa serikali ni kuhakikisha kuwa mbolea inapatikana kwa wingi na bei nafuu kwa kuwekeza kwenye ujenzi wa viwanda vya mbolea hapa nchini.

Amesema serikali imeanza ujenzi wa kiwanda cha mbolea mkoani Dodoma ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha mbolea za aina mbalimbali zaidi ya tani laki sita kwa mwaka.

Dkt.Ngailo amesema kiwanda hicho kinatarajia kuanza uzalishaji msimu wa mwaka 2022/2023,  ambacho amesema kitakuwa ni ukombozi mkubwa kwa wakulima hapa nchini wakiwemo wa Mkoa wa Ruvuma ambao wanaongoza kwa kuzalisha mazao ya chakula nchini.

Kauli mbiu ya mwaka huu ya siku ya mbolea duniani ni tumia mbolea bora, kwa tija na kilimo endelevu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Oktoba 11,2021

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.