• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MTO Ruvuma moyo wa utalii ukanda wa Kusini

Imewekwa kuanzia tarehe: April 21st, 2025

Na Albano Midelo

Ukitaka kushuhudia maajabu ya asili, historia ya ukombozi wa Afrika, na uzuri wa utalii wa kipekee unaovutia kwa macho na roho, basi safari yako lazima ipitie Mto Ruvuma ,mto mrefu kuliko yote Afrika Mashariki na kati.

Mto Ruvuma ni mto ambao haupokei sifa kwa ukubwa wake pekee, ukiwa na urefu wa zaidi ya kilomita 800 na upana wa hadi mita 500 – bali kwa , mazingira ya kuvutia, na nafasi yake muhimu katika maendeleo ya utalii na maisha ya watu kanda ya kusini.


Chanzo Kidogo, ukubwa wa kushangaza 

Kama simulizi ya hadithi za kale, chanzo cha Mto Ruvuma kipo  katika milima ya Matogoro, Manispaa ya Songea  mkoani Ruvuma.

Kisima kidogo tu kilicho meta 1500 kutoka usawa wa bahari. Lakini kutoka hapo, mfereji huo mdogo huanza safari ya kuandika historia katika wilaya zote tano za Mkoa wa Ruvuma: Songea, Mbinga, Nyasa, Namtumbo na Tunduru.

“Chanzo hiki si tu cha kijiografia bali pia ni ushahidi wa maajabu ya Mungu,” anasema Deborah Mwakanosya, Mratibu wa Utalii Kanda ya Kusini. “Kisima kidogo kinachobeba mto mkubwa wa kimataifa “


Mto wa Uzima na Maendeleo

Mto Ruvuma si mto tu wa kupendezesha mandhari; ni moyo unaodunda katika miradi ya maendeleo. Katika shamba la AVIV, Songea.

Maji ya mto Ruvuma yanatumika kumwagilia kahawa ,mazao ya biashara yenye thamani kubwa na kutoa ajira kwa zaidi ya watu 3,000.

Mbali kidogo, katika eneo la Tulila wilayani Mbinga, shirika la watawa wa Mtakatifu Agnes Chipole wilayani Songea,linatumia maporomoko ya mto huo kuzalisha umeme. 

Mradi huo wa hydro-power unazalisha hadi megawati tano kupitia mashine mbili, na bwawa lake lina uwezo wa kuhifadhi meta za ujazo milioni 1.14 za maji. 

Hapa, utalii wa kupiga picha, kuogelea na kuendesha mtumbwi huenda sambamba na nishati safi kwa jamii.


Fukwe, Visiwa na Wanyama Pori

Kuelekea wilaya ya Namtumbo na Tunduru, Mto Ruvuma hubadilika kuwa mto wa ndoto kwa watalii. 

Hifadhi ya mazingira asilia ya Mwambesi inatoa mandhari ya kipekee ,visiwa vidogo, fukwe nzuri, na safari za mitumbwi. 

Hapa, tembo, simba, swala, mamba, na samaki wa aina mbalimbali hutawala kando mwa Mto Ruvuma wakivutia watalii kutoka ndani na nje ya nchi.

Katika Pori la Akiba la Liparamba wilayani Nyasa, maporomoko ya Nakatuta ni kivutio kingine. Wageni huja kuvua samaki, kupiga picha, na kupanda miamba ya asili iliyobeba historia ya miaka mingi.


Historia Iliyogubikwa na Maajabu

Mto Ruvuma haujaishia kwenye uzuri wa kiasili pekee; ni shahidi wa harakati za uhuru. Katika eneo la Mwambesi, maji haya yalitumika katika Vita ya Majimaji (1905–1907), na maporomoko ya Sunda yalitumika kama “darubini ya vita ya porini” ya Golira War iliyopiganwa Msumbiji.

Katika eneo hili, ndege mdogo zaidi duniani  pantiole  huogelea na kuwinda samaki hai, tukio adimu la kihistoria na kibaiolojia.


Mto Ruvuma Unaounganisha Mataifa

Safari ya Mto Ruvuma inaishia katika daraja la Umoja, mpakani mwa Tanzania na Msumbiji, wilayani Nanyumbu. Daraja hilo lenye urefu wa zaidi ya meta 700 linaunganisha mataifa mawili  na siyo kwa daraja pekee, bali kwa urithi wa pamoja wa historia, utalii na amani.

“Mto huu siyo tu mpaka wa kijiografia, bali ni mpaka wa kipekee unaounganisha historia ya ukombozi wa Msumbiji kupitia kijiji cha Negomano, ambacho maana yake ni ‘makutano ya mito’,” anasema Afisa Mahusiano wa Kituo cha Uhamiaji Mtambaswala, Mwamba Lihami.


Bahari ya Hindi: Hitimisho la Safari 

Mwisho wa safari ya Mto Ruvuma ni katika Bahari ya Hindi, eneo la Msimbati, Mtwara. Hapa, maji ya mto huingia katika Hifadhi ya Bahari ya Ghuba ya Mnazi na Maingilio ya Mto Ruvuma, hifadhi yenye ukubwa wa kilomita za mraba 650. 

Ni eneo lenye utajiri wa viumbe vya majini, mikoko, na mandhari ya kupendeza .

Hakuna shaka  Mto Ruvuma si tu kivutio, bali ni chemchemi ya uhai kwa Watanzania na majirani zao wa Msumbiji. 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • MBUNGE Kawawa aleta neema Namtumbo

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.