• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

Imewekwa kuanzia tarehe: May 12th, 2025

Mwenge wa Uhuru 2025 umeikubali miradi yote tisa yenye thamani ya shilingi bilioni1.6 iliyopitiwa  katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma.

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na mradi wa maji safi na salama katika gereza la kilimo Kitai ambao umefunguliwa na Mwenge wa Uhuru ukiwa na uwezo wa kuhudumia wakazi1468.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ,Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mbinga Mashaka Sinkala alisema mradi huo umegharimu Zaidi ya shilingi milioni 400 kutoka serikali kuu.

Mradi mwingine uliozinduliwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Wilaya Ya Mbinga ni mradi  wa  jengo la huduma ya mionzi katika hospitali ya Mtakatifu Gaudensia iliyopo Mkako.

Akitoa taarifa ya mradi huo ,Mkurugenzi wa Hospitali ya Mtakatifu Gaudensia Dr.Thadei Kinyero alisema jengo hilo linatoa huduma na ambazo alizitaja kuwa ni  huduma ya mionzi,kipimo cha kutambua hali ya moyo,radiolojia na kipimo cha umeme wa moyo na kwamba hadi sasa jengo hilo limetoa limetoa huduma ya wagonjwa  4049.

Hata hivyo amesema mradi huo wa jengo la radiolojia umegharimu Zaidi ya shilingi milioni 435.

Mradi mwingine ambao umepitiwa na mwenge wa Uhuru ni mradi wa uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji katika shule ya msingi Kiamili kijiji cha Kigonsera ambapo wanafunzi wameweza kuchimba mabwawa manne kwa gharama ya shilingi 700,000.

Mwenge wa Uhuru pi umetembelea mradi wa uwekezaji  katika shamba la miti la Mbuji lenye ukubwa wa hekari 65.7 zenye thamani ya Zaidi ya shilingi milioni 29.

Mwenge wa Uhuru pia umepita katika mradi wa ,mabweni mawili katika shule ya sekondari Mbuji ambapo serikali imetoa Zaidi ya shilingi milioni 275 kutekeleza mradi huo.

Miradi mingine iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru ni mradi wa  klabu ya wapinga rushwa na shamba la kahawa la mkulima binfasi Herbahat Raphael lililopo katika kijiji cha Nyoni.

Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati anakagua miradi hiyo,Kiongozi wa Mwenge wa Uhuru kitaifa 2025 Ndugu Ismalil Ali Ussi  amewapongeza viongozi katika ngazi zote na wananchi wilayani Mbinga kwa kusimamia utekeleza wa miradi hiyo  ambayo inakwenda kuleta manufaa makubwa kwa wananchi.

Amesema Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan amekuwa anatoa fedha nyingi zikiwemo za maji,afya,barabara na elimu ili kuhakikisha wananchi wanatatuliwa changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Ametoa rai kwa wananchi wote waliojiandikisha kuhakikisha wanajitokeza kwenye uchaguzi mkuu kupiga kura mwezi Oktoba ili kuwachagua madiwani,wabunge na Rais.

 Mwenge wa Uhuru upo mkoani Ruvuma ambapo unatembelea miradi katika Halmashauri zote nane na utakabidhiwa mkoani Mtwara Mei 17 mwaka huu

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru wamulika maendeleo Nyasa

    May 12, 2025
  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.