• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru 2025 wapongeza utekelezaji wa miradi ya Mbinga Mji

Imewekwa kuanzia tarehe: May 13th, 2025

Mwenge wa uhuru umeendelea na mbio zake mkoani Ruvuma kwa kupitia miradi kumi  yenye thamani ya shilingi bilioni 1.2 katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga.

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa wa uhuru 2025 Ndugu Ismail Ali Ussi amepongeza usimamizi wa miradi ya maendeleo uliofanywa na viongozi kwa kushirikiana na wananchi hali iliyosababisha miradi kuwa na viwango bora.

Moja ya miradi iliyopitiwa na mwenge wa uhuru ni ujenzi wa shule mpya ya sekondari Kata ya Betherehemu ambapo serikali imetenga kiasi cha shilingi milioni 740 kutekeleza mradi huo kupitia program ya uboreshaji elimu ya sekondari (SEQUIP).

Mwenge wa uhuru pia umekagua  na kufungua mradi wa maji Mkwaya unaokadiriwa kugharimu Zaidi ya shilingi milioni 375  na unatarajia kuhudumia wananchi 1,853.

Meneja wa RUWASA wilaya ya Mbinga Mhandisi Yona Ndomba amesema hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 100 na tayari kaya 13 zimeunganishwa  na huduma ya maji majumbani.

Mwenge wa uhuru ukiwa katika Halmashauri ya mji wa Mbinga umekagua mradi wa huduma za afya zinazotolewa na  jengo la OPD katika zahanati ya Mtakatifu Gabriel inayomilikiwa na Jimbo katoliki la Mbinga.

Askofu wa Jimbo la Mbinga Mhashamu John Ndimbo amesema ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje OPD ni sehemu tu ya ujenzi wa mradi mzima wa kituo cha afya tarajiwa cha St.Gabriel Jimbo katoliki la Mbinga.

Amesema mradi  wa OPD umegharimu Zaidi ya shilingi milioni 100 ukiwa ni msaada kutoka  kwa wafadhili na majitoleo ya waumini.

Mwenge wa uhuru ukiwa katika Halmashauri ya Mji wa Mbinga pia umekagua mradi wa shamba la miti linalomilikiwa  na Ndugu Lukas Nchimbi Mkazi wa kijiji cha Utiri .

Shamba hilo lina ukubwa la hekari 10.4 likiwa na jumla ya miti ya kupanda 4,600 na kwamba mradi huo una thamani ya shilingi milioni 32.

Mwenge wa uhuru pia ukiwa mjini Mbinga umetembelea na kukagua kikundi cha UMOJA  kinachofanya  shughuli za ufundi seremala na kuchakata mazao ya misitu ili kuongeza kipato cha wanakikundi  ambapo hadi sasa mradi umegharimu  shilingi milioni 33.

Akizungumza baada ya kukamilisha kupitia miradi hiyo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa 2025 Ndugu Ismail Ali Ussi ameupongeza uongozi wa Wilaya,Halmashauri na wananchi kwa usimamiaji mzuri wa miradi ukiwemo mradi mpya wa shule ya sekondari Kata ya Betherehemu  ambayo itawapunguzia watoto umbali wa kwenda mbali kufuata shule ya sekondari.

Amepongeza ujenzi wa shule hiyo ambayo amesema ni bora na ina viwango vinavyolingana na thamani ya fedha

“Mimi binafsi wakati naingia katika shule hii nilikuwa najiuliza hii ni shule au hoteli,mkuu wa wilaya aliniambia hii ni shule,shule kama hii tulikuwa tumezoea kuiona katika maeneo maalum kama Dar es salaam,tuna kila sababu ya kumpongeza Rais kwa kutoa fedha za ujenzi wa shule hii’’,alisisitiza Ussi.

Kiongozi huyo wa mwenge wa uhuru ameendelea kuwakumbusha wananchi kuwa mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi hivyo wote waliojiandikisha wasisite kujitokeza kuwachagua viongozi katika uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Mwenge wa Uhuru upo mkoani Ruvuma tangu Mei 9  hadi Mei 17 mwaka huu utakapokabidhiwa  katika Mkoa wa Mtwara

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru 2025 wapongeza utekelezaji wa miradi ya Mbinga Mji

    May 13, 2025
  • MWENGE wa Uhuru wamulika maendeleo Nyasa

    May 12, 2025
  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.