• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru wamulika maendeleo Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: May 12th, 2025

MWENGE wa uhuru 2025 umepitia na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi tisa yenye thamani ya shilingi bilioni 82 katika wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

Mkuu wa Wilaya ya Nyasa Mheshimiwa Peres Magiri amesema kati ya miradi hiyo,Mwenge wa Uhuru umekagua miradi mitatu,umeweka jiwe la msingi mradi mmoja na kuzindua miradi mitatu na miradi miwili kugawa vyandarua

Akitoa taarifa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025,Meneja wa RUWASA Wilaya ya Nyasa Mhandisi Masoud Samila amesema utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 40 na kwamba wananchi 4,490 watapata maji safi kupitia mradi huo.

Mwenge wa Uhuru pia umezindua mradi wa mtambo za kufua hewa tiba (Oxygen plant)  ambapo kiasi cha shilingi milioni 480 zimetumika kujenga miundombinu ya gesi na ununuzi wa mtambo wa kuchakata hewa tiba.

Mradi huu umekuwa na faida kubwa katika utoaji wa huduma za afya hospitalini ikiwemo kusogeza huduma jirani na kupunguza gharama za kununua huduma.

Mwenge wa uhuru  umekagua shughuli za kikundi cha  wajasiriamali vijana katika kijiji cha Ruhekei Kata ya Kilosa ambapo kikundi hicho kimefanikiwa kupata mkopo wa shilingi milioni 16.5 .

Akitoa taarifa ya kikundi hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nyasa Khalid Khalif amesema mkopo huo unatokana na fedha za asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo.

Mradi mwingine uliozinduliwa na Mwenge wa uhuru ni ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya sekondari Limbo ambapo serikali ilitenga shilingi milioni 72 kutekeleza mradi huo.

Kukamilika kwa mradi huo kumeboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia wanafunzi hivyo kupunguza mlundikano wa wanafunzi darasani.

Mwenge wa Uhuru pia umetembelea na kukagua mradi wa kimkakati wa ujenzi wa bandari  na  barabara ya kuingia bandari ya Mbambabay kwa kiwango cha zege.

Meneja wa Bandari katika ziwa Nyasa Manga Gassaya  amesema serikali imetenga Zaidi ya shilingi bilioni 82 kutekeleza mradi wa bandari ya Mbambabay na kwamba mradi huo unatarajia kukamilika Januari,2026.

Mwenge wa Uhuru ukiwa wilayani Nyasa pia umepitia miradi ya wapinga rushwa katika sekondari ya Kingerekiti na utekelezaji wa shughuli za lishe ambapo wilaya hiyo imetumia Zaidi ya shilingi milioni 33 sawa na asilimia 100 kugharamia afua za lishe kwa watoto 32,574.

Mwenge wa uhuru umekagua mradi wa kugawa  vyandarua vyenye thamani ya shilingi 500,000  ambapo katika wilaya ya Nyasa mwaka 2024 jumla ya watu 14,412 waliugua ugonjwa wa malaria.

Wilaya ya Nyasa inaendelea na mapambano dhini ya malaria kwa kugawa vyandarua kwa watoto chini ya miaka mitano jumla ya wajawazito 7,325 na watoto 9,114 walipatiwa vyandarua mwaka 2024.

Akizungumza baada ya kukagua miradi hiyo ukiwemo mradi mkubwa wa kimkakati  wa ujenzi bandari ya Mbambabay,Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru 2025, Ismail Ali Ussi  Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ametoa mabilioni ya fedha kuhakikisha mradi wa bandari ya kisasa unakamilika.

“Leo hii tumekuja kujionea bandari ya kisasa inayokwenda kutuunganisha na nchi jirani.serikali imefanya uwekezaji mkubwa wa bandari,mradi ambao unatarajia kukamilika mapema mwaka 2026”,alisema.

Katika hatua nyingine Kiongozi huyo wa mwenge wa Uhuru amewakumbusha wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu kwenda kupiga kura.

Amesema Mwenge wa uhuru ni chombo kinachomwakilisha Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan na kwamba unapouona mwenge wa Uhuru  utambue kuwa Rais yupo katika eneo hili.

Mwenge wa uhuru upo mkoani Ruvuma kuanzia Mei tisa hadi Mei 17 utakapokabidhiwa mkoani Mtwara.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru wamulika maendeleo Nyasa

    May 12, 2025
  • MWENGE wa Uhuru 2025 waikubali miradi yote Mbinga

    May 12, 2025
  • WANANCHI walivyojitokeza kuupokea mwenge wa Uhuru katika kijiji cha Maguu Mbinga

    May 11, 2025
  • MAHABA ya wananchi wa Mbuji wilayani Mbinga kwa Mwenge wa Uhuru 2025

    May 11, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.