• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

MWENGE wa Uhuru wazindua Mradi wa madarasa mawili wenye thamani ya milioni 40

Imewekwa kuanzia tarehe: September 6th, 2021

MRADI wa Madarasa mawili ya shule ya Msingi Mtyangimbole umezinduliwa na kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Lt Josephine Mwambashi na ametembelea mradi wa lishe pamoja na kukagua banda la Malaria.

Ujenzi wa Madarasa hayo umegharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 40 kutoka Serikali kuu na nguvu kazi za Wananchi shilingi milioni 5.5, na kubaki shilingi zaidi ya milioni 4 na kutumika kukarabati madarasa mengine.

Mara baada ya kuzinduliwa kwa Madarasa hayo Kiongozi huyo amesema umuhimu wa madarasa hayo yataongeza ari  ya wanafunzi kupata hamasa ya kujisomea kwa usahihi na amewaagiza wanafunzi kutumia vizuri na wengine wajao watumie.

Mwambashi ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kusimamia mradi huo kwa viwango vinavyotakiwa na kuhakikisha kiasi cha fedha zaidi ya shilingi milioni 4 kinabaki na kutumia  kukarabati madarasa mengine ya shule hiyo.

“Gharama za mradi huo tulipokea fedha kutoka Serikali kuu milioni 40 na nguvu ya wananchi ni milioni 5.5, mradi huo umejengwa kwa kutumia force account”.alisema Mkurugenzi wa Halmashauri.

Wakati huo huo katika kuboresha afya ya wananchi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Sajidu Idrisa Mohamed ameuongea  mradi wa lishe ikiwemo siku ya afya ya Lishe ya kijiji cha Likalangilo,ambayo ni mpango  jumuishi ya kuboresha upatikanaji wa Afya kwa jamii na kuwajengea uwezo wa kutambua jinsi ya kuzuia utapiamlo.

 Amesema Wilaya ya Songea inaendelea kuelimisha wananchi kuhusu lishe bora na umuhimu wa Lishe bora katika familia na jamii kwa ujumla kwa kupitia shughuli mbalimbali ikiwemo klini ya kila mwezi kwa wazazi na walezi wa watoto chini ya miaka mitano,siku za afya za Lishe zinazofanyika kila robo ya mwaka.

Hata hivyo ameelezea wananchi wa Halmashauri ya Mdaba  wanavyoelewa umuhimu wa Lishe na wanaendelea kuwafahamisha juu ya umuhimu wa lishe bora na athali zitokanazo na lishe duni na madhara ya utapia mlo.

Vile vile Mkurugenzi  kwa upande wa Malaria amesema Ugonjwa wa malaria ni miongoni mwa Magonjwa 10 yanayoongoza kuhatarisha  maisha ya jamii katika Wilaya ya Songea.

“Hali ya maambukizi imepungua kwa wastani wa kutoka asilimia 11.5 mwaka 2019  na kufikia asilimia 8.1 mwaka 2021,hii ni kutokana na hatua mbalimbali ambazo zilikuwa zikichukuliwa  na idara ya afya”.

Ameelezea utekelezaji wa kuhakikisha Ugonjwa huo unadhibitiwa kwa matibabu kwa kutumia kanuni na miongozo  ya Wizara ya Afya kwa walewanaobainika wameambukizwa Uganjwa kwa wajawazito wanaoanza kliniki na watoto chini ya miaka mitano.

Imeandaliwa na Aneth Ndonde

Kutoka ofisi ya Habari Ruvuma

Septemba 6,2021.

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.