• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

RC RUVUMA awaagiza wakurugenzi kusimamia afua za lishe

Imewekwa kuanzia tarehe: May 3rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amewataka wakurugenzi wa Halmashauri zote za mkoa wa Ruvuma kuhakikisha wamiliki wa mashine za kuongeza virutubishi katika chakula wanapata elimu za urutubishaji wa chakula na kufungiwa mashine za kuongeza virutubishi.

Ametoa maagizo hayo wakati wa kikao kilicholenga kutoa Elimu kwa viongozi wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri kuhusu uongezaji wa virutubishi kwenye chakula kilichofanyika katika ukumbi wa Hunt Club uliopo Ruhuwiko Manispaa ya Songea.

"Ili watoto wetu wafikie ukuaji timilifu na kuweza kutokomeza udumavu katika mkoa wetu, nitoe maelekezo kwa wakurugenzi wa halmashauri za mkoa wa Ruvuma kuhakikisha kuwa wamiliki wa mashine waliopo kwenye halmashauri zenu wanapatiwa elimu ya urutubishaji wa chakula na kufungiwa mashine za kuongeza virutubishi ili waweze kuifikia jamii yetu kwa idadi kubwa," alisema Kanali Ahmed.

Maagizo mengine ni kufuatilia ili kuhakikisha urutubishaji vyakula unafanyika wakati wote ili kuleta matokeo mazuri katika kukabiliana na hali duni ya lishe.

Kanali Ahmed ameeleza kuwa hali ya lishe katika mkoa wa Ruvuma bado si nzuri hivyo amesisitiza umuhimu wa kuboresha hali ya lishe katika jamii hususan kwa watoto na wanawake ili mkoa na Taifa kwa ujumla liwe na jamii yenye siha nzuri.

Amebainisha kuwa hali ya udumavu katika mkoa ni asilimia 35.2, uzito pungufu asilimia 12.2, upungufu wa damu kwa watoto asilimia 45 na upungufu wa damu kwa wakina mama wajawazito ni asilimia 30, hivyo kutokana na hali hiyo mkoa umeendelea kuandaa mipango harakishi na shirikishi ya kupunguza udumavu kwa kushirikiana na wadau wanaoongeza virutubishi kwenye mazao lishe na unga wa mahindi ili kupunguza tatizo la madini na vitamin katika jamii.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Dr. Louis Chomboko, amesema kanuni zinawataka wasindikaji wote wa unga wa mahindi wanaofungasha kuongeza virutubishi ikiwa malengo ya Serikali ni kuhakikisha viwanda vyote vinavyosindika unga wa mahindi vinarutubisha unga huo.

Amesisitiza umuhimu wa jamii kutumia chakula kilichoongezwa virutubishi kwa kuwa ndio kinga ya kuepuka athari zinazojitokeza kwa kukosa madini na vitamin zikiwepo watoto kuzaliwa na tatizo la kichwa kujaa maji, mgongo wazi, ukuaji duni kwa watoto kimwili na kiakili, ufupi, goita na upungufu wa damu mwilini.

Mkurugenzi wa kampuni inayojihusisha na teknolojia ya urutubishaji wa chakula (Sanku) upande wa Mashirikiano na Serikali, Gwao Omari Gwao, amesema asilimia kubwa ya jamii ya Ruvuma na watanzania wanatumia unga wa mahindi kutoka viwanda vidogo na vya kati ambavyo havijasajiliwa na haviongezi virutubishi kwenye unga wanaozalisha hivyo kuiweka jamii hatarini kiafya na lishe.

Mkoa wa Ruvuma una jumla ya mashine 937, kati ya hizo wanaofungasha ni 130, zinazoongeza virutubishi kwenye unga wa mahindi ni 40 ambayo ni sawa na asilimia 31.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MBINGA-MBAMBABAY : barabara inayojenga utalii kwenye milima ya Kusini

    June 01, 2025
  • PICHA ya Rais Samia yapamba mti wa kihistoria Namtumbo

    June 01, 2025
  • TAIFA lamlilia Songambele Shujaa wa Uhuru aliyeishi karne moja

    June 01, 2025
  • SHAMBA la AVIV Tanzania ni mfano wa kuigwa nchini

    June 01, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.