• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SENSA ya mifugo,kilimo,uvuvi kufanyika Ruvuma kwa siku 60

Imewekwa kuanzia tarehe: August 31st, 2020


ZOEZI  la sensa ya mifugo,kilimo na uvuvi linatekelezwa kwa miezi miwili ndani ya Mkoa wa Ruvuma kwa kufanya madodoso  katika kaya 1498 .

Meneja wa Takwimu mkoani Ruvuma Mwamtum Athuman Uhenga  amesema zoezi hilo ambalo linaendelea katika nchi nzima katika Mkoa wa Ruvuma limeanza Agosti 5 mwaka huu na linaratajia kukamilika Oktoba 3 mwaka huu.

Amesema katika zoezi hilo kutakuwa na madodoso matatu ambayo yatakwenda kuhojiwa katika kaya zilizochaguliwa.

Ameyataja madodoso hayo kuwa ni dodoso la wakulima wakubwa,dodoso la wakulima wadogo na  dodoso la jamii ambalo linachukuliwa katika ngazi ya  kijiji au mtaa ambao umechaguliwa katika sensa hiyo.

“Taarifa ambazo zinakwenda kukusanywa ni za uzalishaji kwa mwaka wa kilimo wa 2019/2020,taarifa zinazoanzia  Oktoba Mosi,2019 hadi Septemba 30,2020’’.alisema.

Hata hivyo Uhenga  amesema hadi sasa hakuna changamoto iliyojitokeza ambapo amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa watalaam wa takwimu wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo la kitaifa.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Seligius Ngai  akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mbingamhalule wilayani Songea baada ya kukagua zoezi la madodoso ,amesema takwimu ni uti wa mgongo wa shughuli za serikali.

Ngai amesema takwimu bora zinahitajika kwa maendeleo bora ambapo amezitaja sifa za takwimu bora kuwa ni zile ambazo zimekusanywa na mamlaka husika,kwa kufuata sheria ya takwimu ya mwaka 2015.

Amesisitiza kuwa ofisi ya Taifa ya Takwimu inahusika moja kwa moja na kukusanya,kuchakata na kutoa taarifa rasmi ambapo amesema zoezi linaloendelea limejikita katika sekta tatu za kiuchumi ambazo ni mifugo,kilimo na uvuvi.

“Katika kilimo tunataka kujua hali ya mazao yetu na changamoto zake,katika mifugo kujua idadi ya mifugo iliyopo,magonjwa ya mifugo na masoko ya mazao ya mifugo’’,alisema.

Ngai amesema mipango yote ya maendeleo inayotekelezwa na serikali,nyuma yake kuna takwimu na kwamba hata Benki ya Dunia ilivyoitangaza Tanzania kuingia kwenye uchumi wa kati nyuma yake kuna takwimu.

Naye Said Ameir Afisa Mawasiliano Ofisi ya Taifa ya Takwimu Makao makuu ametoa rai kwa wananchi kutoa taarifa sahihi ambazo zitatoa takwimu sahihi ambazo zitaleta mpango ambao unawakilisha hali halisi na kutengeneza sera na kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya kilimo,uvuvi na mifugo.

Franki Hyera Mkazi wa kijiji cha Mbingamhalule ameishukuru serikali  kwa kuanza kufanya sensa ya mifugo,kilimo na Uvuvi ambapo amesema mpango huo utaleta manufaa makubwa kwa wananchi baada ya kupata takwimu katika kijiji hicho ambacho kinazalisha kwa wingi mazao ya chakula.

Zoezi la Sensa ya kilimo,mifugo na uvuvi  hapa nchini linafanyika kwa mara ya tano mwaka huu.Zoezi hili lilianza kufanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini mwaka 1972,na kufanyika tena mwaka 1994,2003 na mwaka 2008.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Agosti 30,2020

 

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.