• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SERIKALI yatoa milioni 800 kuboresha huduma za afya hospitali ya Nyasa

Imewekwa kuanzia tarehe: March 21st, 2023

SERIKALI ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  imetoa  shilingi milioni 800 kujenga Hospitali ya wilaya Nyasa,ili kusogeza na kuboresha huduma za afya kwa wananchi ambao awali walilazimika kwenda nje ya wilaya hiyo kufuata matibabu.

Kaimu Mganga mfawidhi wa Hospitali ya wilaya Nyasa Dr Simon Yasin alisema,katika ujenzi huo baadhi ya majengo ikiwemo jengo la wagonjwa wa nje(OPD),wodi ya mama na mtoto na maabara yamekamilika na yameanza kutoa huduma.

Dr Yasin ametaja huduma zilizoanza kutolewa katika Hospitali hiyo ni za wagonjwa wa nje,huduma ya mama na mtoto,kulaza wagonjwa na upasuaji.

“kwa sasa tuko katika awamu ya tatu  na ya mwisho kabisa ya utekelezaji wake,katika awamu hii tunajenga jengo la upasuaji  kwa wanawake na wanaume,jengo la kuhifadhia maiti  sambamba na jengo la dharura ambalo limegharimu shilingi milioni 300”alisema Dkt Yasin.

Kwa mujibu wa Dkt Yasin,majengo hayo yatakapokamilika yatasaidia wananchi wa wilaya hiyo kupata huduma bora za matibabu,kuokoa vifo vya akina wakati na baada ya kujifungua na kupunguza muda wa kwenda maeneo mengine kufuata huduma za afya.

Alisema,Hospitali hiyo ni kubwa na imejengwa eneo ambalo kila mmoja rahisi kufika na imesaidia sana wananchi wa Nyasa kupata huduma za afya karibu.

Dr. Yasini,amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na serikali yake ya awamu ya sita, kwa kuridhia kutoa fedha  zilizotumika katika utekelezaji wa mradi huo muhimu na mkubwa kwa ajili ya wananchi.

Aidha alisema kuwa,kujengwa kwa Hospitali hiyo na kuanza kutoa huduma za matibabu kumewapunguzia wananchi kero  na usumbufu wa kutembea umbali mrefu hadi katika Hospitali nyingine kufuata matibabu.Ametoa wito kwa wananchi,kutumia zahanati,vituo vya afya na Hospitali  zinazojengwa na serikali kwenda kupata huduma za matibabu kwa sababu zimejengwa kwa ajili yao.

Dr Yasin,amewashauri akina mama pindi wanapohisi dalili za ujauzito ni vyema wakawahi kliniki mapema ili kupata ushauri  kwa ajili ya usalama wao na mtoto aliyeko tumboni na wakati na baada ya kujifungua.

Kwa upande wake Muuguzi wa Hospitali Lucia Lagila ametaja faida mojawapo kwa  akina mama kuwahi kliniki ni kupunguza vifo vya mama na mtoto,kupata ushauri wa kitaalam wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua.

Mkazi wa kijiji cha Ng’ombo Blandina Chalima alisema,kujengwa kwa Hospitali hiyo ni ukombozi mkubwa kwao kwani kwa muda mrefu walitegemea kupata huduma za matibabu kwenye zahanati moja tu inayomilikiwa na Kanisa.

Chalima,ameiomba serikali kupitia Halmashauri ya wilaya Nyasa kuhakikisha inapeleka vifaa tiba na  dawa za kutosha  katika Hospitali hiyo,badala ya kuendelea kufuata baadhi ya huduma  katika vituo vingine vilivyopo mbali na makazi yao.Philip  Chambo mkazi wa kijiji cha Kihagala,ameishukuru serikali kuboresha na kumarisha sekta ya afya kwani imesaidia kupunguza vifo vingi  kwa wananchi katika  wilaya hiyo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.