• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

TARURA yasaini mikataba ya kutengeneza barabara za Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: August 7th, 2024

Na Gustaph Swai-RS Ruvuma

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Ruvuma umesaini mikataba ya matengenezo ya barabara kwa mwaka 2024/25 na Kampuni ya Kimango Engineering Company Limited.

Hafla ya utiaji saini wa mikataba hiyo imefanyika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, ikishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa, Kanali Ahmed Abbas Ahmed.

Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa TARURA Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Silvester Chinengo, amesema Serikali imeidhinisha bajeti ya shilingi bilioni 22.19 kwa ajili ya kutekeleza jumla ya kilometa 1,170 za barabara Mkoani Ruvuma.

Hata hivyo amebainisha kuwa tayari mikataba 50 yenye thamani ya shilingi bilioni 14 imesainiwa, na utekelezaji wa miradi hio utaanza muda wowote kuanzia Sasa .


"Hadi sasa tumeingia mikataba 50 ambayo ina thamani ya bilioni 14 ,na utekelezaji utaanza muda wowote kuanzia Sasa, zoezi linalofuata baada ya hatua hii ni kuwakabidhi wakandarasi kazi kwenye maeneo ya wilaya zetu ambako ndiko kazi zinafanyika" amesema Mhandisi Chinengo.


Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kimango Engineering Company, Happyness Kimaro, ameahidi kufanya kazi kwa weledi na kwa kiwango cha juu, huku akiishukuru Serikali kwa kuongeza kiwango cha mikataba kutoka shilingi bilioni 10 hadi bilioni 50 kwa wakandarasi wazawa.


Akizungumza kwenye hafla hiyo Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas , amesisitiza umuhimu wa wakandarasi kufanya kazi kwa ubora unaolingana na thamani ya fedha.

Kanali Abbas amewataka wakandarasi hao kutoa taarifa endapo watakutana na changamoto ili ziweze kutatuliwa kwa haraka.


Aidha Mkuu wa Mkoa ameisisitiza TARURA kutoa kipaumbele kwa wanaruvuma na kina mama wenye uthubutu katika miradi ya Mkoa , na kuhakikisha madeni ya wakandarasi yanalipwa ili kuwezesha wakandarasi kufanya kazi kwa weledi.


I katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024, TARURA Mkoa wa Ruvuma ilitia saini mikataba 41 ya matengenezo ya barabara na ujenzi wa madaraja na makalavati yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 11.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.