• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VIAZI mviringo kuanza kulimwa Ruvuma-UTAFITI

Imewekwa kuanzia tarehe: May 24th, 2024

Hekari moja kuingiza milioni 16

Na Albano Midelo,Songea

UTAFITI uliofanywa na Taasisi ya Kuendeleza Kilimo Nyanda za Juu Kusini (SAGCOT) katika Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma kuanzia mwaka  2020 hadi 2024 umebaini kuwa viazi mviringo vimetoa matokeo mazuri katika uzalishaji.

Afisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Onesmo Mpuya  akizungumza kwenye zoezi la kuzindua uvunaji wa zao la viazi mviringo katika shamba darasa la majaribio Kata ya Tanga Manispaa ya Songea ya Songea, amesema  SAGCOT wamefanya utafiti wa kulima viazi mviringo katika vijiji vya Liganga,Mang’ua na Tanga wilayani Songea  na zao hilo kuonesha mafanikio makubwa katika uzalishaji.

“Watu wengi wanaamini viazi mviringo vinastawi  vizuri mkoani Njombe na hata mimi nilikuwa naamini hivyo,kumbe kama huna utafiti huna haki ya kusema,utafiti wetu wilayani Songea umebaini viazi mviringo vinafanya vizuri sana’’,alisisitiza Mpuya.

Ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuona fursa ya kutengeneza uchumi na kuongeza kipato kupitia zao la viazi mviringo ambapo utafiti umebaini kuwa heka moja ya viazi mviringo inazalisha magunia 200 hivyo kumuingizia mkulima wastani wa shilingi milioni 16.

Amesema Idara ya kilimo Mkoa wa Ruvuma kwa kushirikiana na SAGCOT inahamasisha kilimo cha parachichi katika  Mkoa wa Ruvuma ambapo hadi sasa  kuna Zaidi ya hekari 500 ambazo zimepandwa parachichi ambazo  ambazo huanza kuzaa baada ya miaka mitatu.

Mgeni rasmi kwenye hafla ya uvunaji viazi mviringo,Mstahiki Meya wa Manispaa ya Songea Mheshimiwa Michael Mbano amesema wakulima wa Songea kwa muda mrefu wamekuwa wakitegemea zao moja la mahindi ambapo  amesema zao la parachichi na viazi mviringo linakwenda kuleta fursa mpya na  tija kwa wakulima.

Mbano amesisitiza kuwa wakati anapata taarifa za uzinduzi uvunaji viazi mviringo hakuamini kama ardhi ya Songea inafaa kwa kilimo cha zao hilo na kwamba wananchi wengi wa Songea hawana taarifa kama viazi mviringo vinaweza kustawi na kuwaongezea kipato.

Amesema  tani 20 za viazi mviringo ambazo zinavunwa kwa hekari moja  ni uchumi ambao kila mwananchi wa Mkoa wa Ruvuma anatamani kupata ambapo pia ametoa rai kwa wananchi wa Songea kulima zao la parachichi ambalo pia linatoa kipato kikubwa

Amesema utafiti umebaini mti mmoja wa parachichi kwa mwaka unaweza kumuingia mkulima kati ya shilingi 500,000 hadi 800,000 hivyo ametoa rai kwa wananchi wa Manispaa ya Songea  kupanda miti ya matunda kama parachichi  na viazi mviringo ili kukuza uchumi wao.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima cha LUSITU AGRI BUSSINESS ambaye pia ni Mkulima  Mwezeshaji Beno Mgaya ameitaja Taasisi ya Kuendeleza Kilimo Nyanda za Juu Kusini (SAGCOT) imedhamiria kutoa mafunzo ya kilimo biashara ili wakulima waweze kujitambua kwa kuhamasisha kilimo cha parachichi na viazi mviringo katika Mkoa wa Ruvuma.

Amesema utafiti walioufanya katika wilaya ya Songea kuhusu zao la viazi mviringo kwa kutumia mbegu za aina mbili kutoka nchini Uholanzi  zimetoa matokeo mazuri na kwamba hapa nchini hivi sasa kuna aina 16  za mbegu za viazi mviringo.

Mgaya amelitaja lengo la kuanzisha kilimo cha viazi mviringo ni kumwezesha mkulima kupata kipato wakati anasubiri zao la parachichi ambalo huchukua miaka  mitatu hadi kuanza kuzaa mkoani Ruvuma.

Amesema SAGCOT imedhamiria kuwa na mashamba darasa katika zao la viazi mviringo katika maeneo ya Shule ya Tanga, Liganga,Litapwasi,Namatuhi na Peramiho wilayani Songea na kwamba mashamba darasa yote yapo katika mfumo wa umwagiliaji.

Hata hivyo amesema wakulima wa viazi mviringo mkoani Ruvuma wataweza kuzalisha kwa kutumia umwagiliaji hivyo kuzalisha  mwaka mzima na kumwezesha mkulima kupata kipato kizuri Zaidi.

Mwenyekiti huyo anamshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuiamini SAGCOT ili iweze kufanya kazi Tanzania nzima ambapo hadi sasa imeenea katika mikoa tisa. 

Kandidus Komba Mkulima Mwamasishaji kutoka Kijiji cha Liganga wilayani Songea, ameipongeza SAGCOT kwa kusimamia mradi huo kwa zao la  parachichi ambapo wakulima wa vijiji vya  Liganga, Peramiho,Litapwasi,Ndongosi,Lipokela, na Mang’ua,Mtakanini na Geraza la Kitai ,wamenufaika na mradi huo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.