• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

VIONGOZI wa vijiji Namtumbo wapatiwa mafunzo ya utawala bora

Imewekwa kuanzia tarehe: May 13th, 2021

Viongozi  wa serikali za vijiji 7 wakiwemo  wenyeviti wa vijiji ,watendaji wa vijiji ,wenyeviti wa kamati  ya maliasili wa vijiji  na waheshimiwa  madiwani  kutoka katika kata  za vijiji hivyo wamepatiwa mafunzo ya  utawala bora kutoka FORVAC  na MJUMITA.


Akifungua  mafunzo  hayo  mkuu wa wilaya ya Namtumbo  Sophia Mfaume  Kizigo aliishukuru FORVAC na MJUMITA kwa jitihada zao za kutoa elimu kwa jamii  kuhusu faida  ya kutunza  misitu  yao iliyopo  katika vijiji .


Kizigo  alisema mafunzo hayo yapate  wataalamu  wa uhifadhi  katika vijiji  watakaosimamia utawala bora ili lengo la uhifadhi  kwa jamii liongeze  faida  za kiuchumi,kijamii  na kimazingira  kutokana na usimamizi  endelevu wa misitu yao.


Hata  hivyo  kizigo aliwataka  viongozi  wanaopata mafunzo hayo  kuzingatia misingi ya utawala bora  ya  uwajibikaji,uwazi ,utawala wa sheria,maridhiano ,mwitiko,ushirikishwaji  na  kuleta ufanisi na tija katika jamii  wanayoiongoza.


Maulidi  Hamisi afisa misitu wilayani Namtumbo aliwaambia viongozi  wa vijiji  kuwa  viongozi  wa vijiji wengi  wanaohudhuria mafunzo ya misitu hawatoi  mrejesho  kwa wananchi  na badala yake  hubaki  nayo  wenyewe  hali  inayosababisha wananchi kutoelewa  dhana dhima ya uhifadhi wa misitu yao ya vijiji.


Hamisi aliwataka  viongozi  hao kwenda kutoa mrejesho  kwa wananchi katika vijiji  vyao ili wananchi waweze  kujua maana  na umuhimu wa uhifadhi wa misitu yao ya vijiji na kupunguza  migogoro  ambayo  inasababishwa  na kutotolewa  taarifa kwenye mikutano  ya maamuzi ya vijiji..


Naye Mwenyekiti wa  mtandao  wa jamii wa usimamizi wa misitu Tanzania  bwana  Revocatus  Njau  aliwataka viongozi hao wa  vijiji kuwa mfano wa kusimamia utawala bora katika uhifadhi wa misitu katika vijiji vyao .


Diwani wa kata ya Mkongo Daniel Nyambo  pamoja na kushukuru  FORVAC  na  MJUMITA kwa mafunzo ya utawala bora alieleza tatizo la uhifadhi katika vijiji vya Namtumbo kuwa  vijiji  vinaweza  kutenga maeneo ya hifadhi lakini wafugaji  wameenea katika maeneo yaliyotengwa na kuharibu maana ya uhifadhi .


Alisema  wakulima ni rahisi kuwaondoa lakini wafugaji  inahitajika nguvu za  ziada  za dola kuhakikisha  wafugaji  wanaheshimu  mipango ya vijiji  wanajifugia mifugo  katika maeneo ambayo hayastahili  kupelekwa  mifugo hiyo.


Mafunzo hayo  yalikuwa ya siku  moja yaliyofanyika katika ukumbi wa  Halmashauri ya wlaya  ya Namtumbo  na viongozi wa kijiji cha Kumbara,Limamu,kilangalanga,Chengena,Masuguru ,Njalamatata,Ligunga  pamoja na madiwani wa kata ya luchili,mchomoro,mkongo,mkongo gulioni  na limamu walihudhuria mafunzo hayo.

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.