• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

WATANO washinda 500,000 za NMB mchongo wa kusini Tunduru

Imewekwa kuanzia tarehe: December 21st, 2022

WATEJA watano wa Benki ya NMB Kanda ya Kusini wamejishindia shilingi 500,000 kupitia NMB Bonge la Mpango Mchongo wa kusini.

Wateja hao wameshinda katika droo iliyochezeshwa kwenye tawi la Benki ya NMB Tunduru,kupitia droo hiyo Chama cha Ushirika cha Msingi (AMCOS) cha Tuyangatane cha Newala mkoani Mtwara kimejishindia pikipiki yenye thamani ya shilingi milioni tatu.

Mwakilishi wa Meneja wa NMB kanda ya Kusini Roman Degeleki amesema NMB Bonge la Mpango Mchongo wa Kusini linashirikisha wateja wa NMB kutoka mikoa ya Ruvuma,Lindi na Mtwara .

Amewataja wateja watano wa NMB Bonge la Mpango Mchongo wa Kusini waliojishindia shilingi laki moja kila mmoja kwenye droo ya Tunduru kuwa ni Daudi Salim Randy wa Ndanda Mtwara,Erick Christopher Chisigalile wa Newala Mtwara,Mangungu Murtaza Ally wa Kilwa Lindi,Dismass Agustino Tarimo wa Newala Mtwara na Abubakar Mohamed Msham wa Kilwa Lindi.

Amelitaja tawi la NMB Tunduru kuwa ni miongoni mwa matawi 19 ya benki hiyo katika Kanda ya kusini ambayo yana wateja wengi wanatumia huduma za NMB ndiyo maana benki hiyo imeamua kuchezesha droo ya NMB bonge la Mpango kwenye tawi hilo.

‘’NMB bonge la mpango mchongo wa kusini ni kampeni maalum iliyoandaliwa na NMB kwa ajili ya wakazi wa kusini tu”,alisisitiza Roman.

Kwa upande wake mgeni kwenye hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mheshimiwa Julius Mtatiro ameipongeza NMB kwa kuamua kuchezesha droo bonge la mpango mchongo wa kusini katika tawi la Tunduru.Amesema droo hiyo imetoa fursa kwa wateja wa NMB binafsi na vyama vya Ushirika vya msingi kushinda pikipiki na pesa tasilimu.

Ameitaja NMB kuwa ndiyo benki kubwa nchini ambayo imekuwa inatoa huduma za kibenki mijini na vijijini hivyo kuwa karibu zaidi na wateja.

Kwa upande wake Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Bisani George akizungumza kwenye hafla hiyo ametoa rai kwa vyama vya Ushirika vya Msingi kujiunga na NMB ili kunufaika na huduma mbalimbali. Afisa Ushirika huyo pia ameipongeza NMB kwa kuwahudumia wakulima na wanachama wa vyama vya Ushirika katika Halmashauri hiyo kwa kutoa mikopo na huduma nyingine za kibenki.

Naye Salum Mohamed mwananchi wa Tunduru ameipongeza NMB kwa kuchezesha droo hiyo katika tawi la Tunduru ambapo amesema italeta hamasa kubwa wananchi kujitokeza kwenye droo ya NMB bonge la mpango mchongo wa kusini kwenye droo zitakazofuata.

Imeandikwa na Albano Midelo wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Desemba 21,2022

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI mwenge wa Uhuru aonya rushwa kwenye uchaguzi

    May 10, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.