Zahanati ya Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga ni miongoni mwa vituo vya afya vinavyotoa mchango mkubwa katika utoaji wa huduma bora za afya kwa jamii, hususan maeneo ya vijijini. Kwa kutambua mahitaji yanayoongezeka ya huduma za afya.
Zahanati hiyo imeboresha miundombinu yake kwa kujenga jengo jipya la kisasa la wagonjwa wa nje (OPD). Ujenzi wa jengo hili ni hatua muhimu inayolenga kuongeza ufanisi wa utoaji huduma, kupunguza msongamano wa wagonjwa, na kuhakikisha upatikanaji wa huduma kwa wakati kwa watu wa rika na hali mbalimbali za kiafya.
Jengo la OPD lililojengwa lina vyumba vya kisasa kwa ajili ya usajili, uchunguzi wa awali, matibabu ya wagonjwa wa nje, na huduma za ushauri wa kiafya. Kupitia jengo hili, wagonjwa wanahudumiwa kwa heshima na kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu vinavyohitajika katika utoaji wa huduma za afya.
Jitihada hizi ni sehemu ya dhamira ya Kanisa Katoliki Jimbo la Mbinga kuendelea kushirikiana na serikali na wadau wengine katika kuboresha afya za wananchi, hasa wale wanaoishi maeneo ya pembezoni. Hili ni jambo la kupongezwa kwani linadhihirisha uwajibikaji wa taasisi za dini katika kuchangia maendeleo ya jamii.
Regional Commissioner Office
Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.
Simu: 0252602256
Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174
Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz
Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.