• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

ZAIDI ya watu 68,000 wanaishi na Virusi vya UKIMWI Ruvuma

Imewekwa kuanzia tarehe: November 26th, 2024

JUMLA ya watu 68,237 wanaishi na virusi vya UKIMIWI (VVU) Mkoani Ruvuma.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed  wakati anazungumza kwenye ufunguzi wa maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani  ambao umefanyika katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Kanali Abbas amesema kati ya watu hao,wanaume ni 24,959  na wanawake ni 43,238 na kwamba Watoto chini ya  umri wa miaka  15 wenye VVU ni 2,382 sawa na asilimia 3.5 na watu wazima wenye umri wa kuanzia miaka 15 ni 65,855 sawa na asilimia 96.5.

Amezitaja Halmashauri zinazoongoza kuwa na idadi kubwa ya watu wenye VVU kuwa ni Manispaa ya Songea yenye watu 18,398,Tunduru watu 9,888 na Halmashauri ya Mbinga watu 9,003.

“Natoa wito kwa waathirika wote kuzingatia tiba na matunzo,ufuasi wa dawa za ARV ni uzima na zinaimarisha afya ya watu wanaoishi na VVU ,hivyo nawaasa wananchi kuacha unyanyapaa na ubaguzi,Mkoa utaendelea kuwajengea mazingira mazuri  watu wanaoishi na VVU ili kujiwezesha kiuchumi’’,alisisitiza Kanali Abbas.

Amesema maambukizi ya VVU katika Mkoa wa Ruvuma katika mwaka 2022 hadi 2023 ni asilimia 4.9  na kwamba kiwango hicho kimepungua ukilinganisha na mwaka 2016/2017 ambacho kilikuwa ni asilimia 5.6 .

Hata hivyo  amesema  kiwango hicho cha maambukizi katika Mkoa wa Ruvuma bado kipo juu  zaidi ya kiwango cha kitaifa kwa asilimia 0.5 ambacho ni asilimia 4.4.

Amesema kiwango cha maambukizi mapya ya VVU kimepungua kwa asilimia 28.6 kutoka watu 3.035 mwaka 2017 hadi kufikia watu 2,168 mwaka 2022 ambapo kwa mwaka 2023 watu 1,889 walipata maambukizi mapya ya VVU katika Mkoa wa Ruvuma

Kaulimbiu ya maadhimisho ya UKIMWI kwa mwaka huu ni chagua njia sahihi,tokomeza UKIMWI ambapo kilele cha maadhimisho hayo ni Desemba Mosi ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais Dkt.Philip Mpango

Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MWENGE wa Uhuru waikubali miradi yote Madaba

    May 09, 2025
  • RC Ruvuma ALIVYOSHIRIKI Makabidhiano mradi wa ujenzi wa Chuo cha Uhasibu Songea

    May 08, 2025
  • SERIKALI yatenga bilioni 18.5 kujenga chuo kikuu Ruvuma

    May 08, 2025
  • MWENGE wa Uhuru kukagua,kuzindua miradi 76 Ruvuma

    May 08, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.