• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Majibu ya haraka |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • RSFMIS |
Ruvuma Region

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Ruvuma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Uongozi wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Miundombinu
      • Maji
      • Afya
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
      • Tehama
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Songea
    • Wilaya ya Mbinga
    • Wilaya ya Nyasa
    • Wilaya ya Tunduru
    • Wilaya ya Nantumbo
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Madaba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mji
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Songea
    • Halmashauri ya Manispaa ya Songea
    • Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
  • Fursa za Uwekezaji
    • Mifugo
    • Kilimo
    • Vivutio vya Utalii
    • Madini
    • Nyaraka za uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
  • Machapisho
    • Miongozo na Nyaraka za uwekezaji
    • Taratibu
    • Taarifa
    • jarida
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • habari
    • Matukio

SEKTA ya afya,lishe na ustawi wa Jamii

TAARIFA YA KIKAO CHA BARAZA LA USHAURI MKOA WA RUVUMA(RCC) DESEMBA 2022.doc

6.3 AFYA, LISHE NA USTAWI WA JAMII

6.3.1 Sekta ya afya 

6.3.1.1 Huduma za Afya

Mkoa una jumla ya vituo 356 vinavyotoa huduma za afya. Kati ya vituo hivyo Hospitali ni 13 zikiwemo 6 za serikali, vituo vya afya 36 kati ya hivyo 10 ni vya mashirika ya dini, zahanati zipo 307 ambapo za serikali ni 246, Mashirika ya dini ni 26, na 9 ni za mashirika ya umma na 26 ni za watu binafsi.

Mapokezi ya Fedha za Utekelezaji wa Miradi ya maendeleo

 

Kwa mwaka 2020/2021 Mkoa umepokea jumla ya Shilingi 1,700,00.000.00 kwa ajili ya kujenga/kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya ambapo Sh. 1,200,000,000.00 zilikuwa kwa ajili ya umaliziaji wa maboma 50 ya zahanati na Sh. 500,000,000.00 kwa ya kituo cha Afya Magazini.

Kwa mwaka 2021/2022 Mkoa umeendelea na ujenzi wa Hospitali tano (5) za Wilaya katika Halmashauri za Wilaya za Nyasa, Namtumbo, Madaba, Songea DC na Mbinga DC kwa gharama ya Tshs. 3,700,000,000.00. Mkoa umepokea kiasi cha Tshs. 7,250,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya 12 kupitia fedha za Tozo na Serikali Kuu. Pia Mkoa unaendelea na ujenzi wa vituo vya Afya vitatu (3) kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri kwa gharama ya Tshs. 1,500,000,000.00.  Kwa upande wa Zahanati Mkoa ulipokea kiasi cha Tshs. 1,050,000,000.00 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa Zahanati 21 kwenye Halmashauri saba (7). 

Aidha, Mkoa umepokea pia kiasi cha shilingi 1,780,000,000.00 za kutekeleza Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 - (Mradi Na. 5144 TCRP) kama ifuatavyo:

Shilingi Milioni 630,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Watumishi wa sekta ya Afya kwa Halmashauri 7 (Madaba DC, Songea DC, Mbinga DC, Nyasa DC, Mbinga TC, Namtumbo DC & Tunduru DC)

Shilingi Milioni 900 kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya dharura (emergency Medical Department-EMD) kwa Halmashauri za Madaba DC, Nyasa DC & Tunduru DC

Shilingi 250,000,000.00 kwa ajili ya Ujenzi wa jengo la huduma za Wagonjwa mahututi (ICU) katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Taarifa ya Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa     

Mkoa ulipokea kiasi cha Tshs. 2,700,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa awamu ya kwanza ambao unahusisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD), jengo la mionzi na nyumba ya mtumishi.

 

6.3.1.2 Hali ya upatikanaji wa bidhaa za afya

Hali ya upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi katika vituo vya kutolea huduma za afya imeendelea kuimarika, kwani upatikanaji umeongezeka kutoka 93 (2021) hadi asilimia 96 mwezi Novemba, 2022. Upatikanaji huu umetokana na kuongezeka kwa mapato ya ukusanyaji ya mapato ya uchangiaji wa huduma za afya, ufuatiliaji na usimamizi pamoja na ruzuku ya dawa kutoka serikali kuu.

                                                                                                                                                         6.3.1.3 Huduma ya Afya ya Uzazi na Mtoto

Vituo vinavyotoa huduma ya Afya ya Uzazi na mtoto vimeongezeka kutoka 324 hadi 348 sawa na asilimia (98%) ya vituo vyote vinavyotoa huduma katika Mkoa. Kati ya vituo vinavyotoa huduma ya afya ya uzazi na mtoto, Vituo 316 sawa na asilimia 92 vinatoa huduma ya chanjo. Aidha kati ya vituo vya afya 36, vituo 14 (38.8%) ya vituo vya Afya (H/C) vinatoa huduma kabambe za dharura za mama wajawazito na Watoto wachanga (CEmONC).

Kwa upande wa huduma ya wazazi, kiwango cha akina mama waliojifungulia kituoni kimeongezeka kutoka asilimia 84.4 mwaka 2020 hadi asilimia 85.4 Desemba 2021. Kiwango hiki ni juu ya lengo la taifa la asilimia 80.

Jedwali Na. 47: Kuonesha mwenendo wa vifo vya kina mama wazazi Mkoa wa Ruvuma kwa miaka minne (4)- 2019-2022

Na
Mwaka
Idadi ya vifo
02

2019

34

03

2020

31

04

2021

24

05

2022

20

Idadi ya vifo vya wazazi vimepungua kutoka vifo 24 Disemba mwaka 2021 hadi vifo 20 sawa na vifo 39 /100,000 vizazi hai Novemba mwaka 2022. Sababu zilizochangia vifo ni Kutokwa na damu nyingi PPH, Kifafa cha mimba, mgando katika mishipa ya damu (Embolism), Upungufu wa damu na madhara ya dawa za usingizi (anaethetic complication).

Vifo vya watoto chini ya mwaka mmoja kwa mwaka 2022 vimepungua kutoka 131 sawa na vifo 3 kati ya watoto 1000 waliozaliwa hai mwaka 2021 hadi vifo 88 sawa na vifo 2 kati ya watoto 1000 waliozaliwa hai Disemaba mwaka 2022. Sababu zilizochangia vifo hivyo ni magonjwa ya watoto wachanga (perinatal condition). Vifo 35 sawa na asilimia 40.0 Prematurity vifo 25 sawa na asilimia 28.4, Pneumonia vifo 13 sawa na asilimia15.0, Malaria vifo 7 sawa na asilimia 8.0, Septicemia vifo 5 sawa na asilimia 6.0   na Anaemia vifo 3 sawa na asilimia 3.4 ya vifo vyote.

Takwimu za vifo vya watoto chini ya miaka mitano vilivyotolewa taarifa ngazi ya vituo na jamii kwa mwaka 2022 vilikuwa 124 sawa na vifo 3 kati ya watoto 1000 waliozaliwa hai. Idadi ya vifo hivi imepungua ukilinganisha na vifo 204 sawa na vifo 4 kati ya watoto 1000 waliozaliwa hai mwaka 2021. Sababu zinazoongoza kwa vifo hivyo ni Neonatal condition vifo 41 sawa na asilimia 33.0, Pneumonia vifo 33 sawa na asiimia 26.6 malaria vifo 24 sawa na asilimia 19.3, Septicaemia vifo 15 sawa na asilimia 12.0 na Anaemia vifo 11 sawa na asilimia 9.0 ya vifo vyote.

6.3.1.4 Hali ya chanjo

Katika kipindi cha Januari hadi Novemba, 2022 Mkoa umekuwa na mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma za chanjo mbalimbali kama ifuatavyo;

Chanjo ya kifua kikuu (BCG) ni 141%, chanjo ya kuzuia kupooza (Polio) 125%, chanjo ya Donda koo, kukakamaa na kifaduro (DTP3) 123% chanjo ya kuzuia homa ya mapafu (Pneumonia) 122%, chanjo ya kuzuia kuharisha (Rota virus) 99.5%, chanjo ya surua (Measles Rubella) 122%, chanjo ya Pepopunda (Td) kwa wajawazito 117% na chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi (HPV) kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 ni 115%.

Mkoa umeendelea kutoa chanjo ya ugonjwa wa Korona ikiwa ni jitihada za kupambana na ugonjwa huu ambapo kwa kipindi cha kuanzia tarehe 04 Agosti, 2021 hadi tarehe 31 Oktoba, 2022 jumla ya watu 1,045,390 wamekamilisha dozi ya chanjo ya korona sawa na asilimia 109. Mkoa uliwekewa kuchanja jumla ya watu 670,577 ambao ni sawa na asilimia 70 ya watu wote wenye umri wa miaka 18 na kuendelea (ambao ni 957,938).

Mkoa wa Ruvuma umeongoza Kitaifa kwa utoaji wa chanjo ya UVIKO-19 na kupewa vyeti 2 na tuzo kwa vipindi tofauti tofauti kwa mwaka 2021 hadi Mei, 2022. Pia katika mazoezi ya Kitaifa ya utoaji wa chanjo ya polio Mkoa wa Ruvuma umefanya vizuri katika awamu zote 4 (awamu ya kwanza nay a pili Tuliongoza Kitaifa iliyofanyika mwezi Machi na Mei, 2022). Utoaji wa chanjo za kawaida tunaendelea kufanya vizuri tangu tutangazwe kuwa vinara 2021.

6.3.1.5 Huduma za VVU na UKIMWI 

Kati ya vituo 356, vituo 328  sawa na asilimia 92 vinatoa huduma za unasihi na upimaji wa VVU (HTS); vituo 285 sawa na asilimia 80 vinatoa huduma za Kuzuia Maambuzi ya VVU toka kwa Mama kwenda kwa Mtoto (PMTCT); vituo 147 sawa na asilimia 41 vinatoa huduma za tiba na matunzo ya VVU na UKIMWI (CTC); vituo 41 sawa na asilimia 12 vinatoa huduma za Dawa Kinga ya Kuzuia Maambukizi ya VVU (PrEP) na vituo 45 sawa na asilimia 13 vinatoa huduma ya Tohara ya Kitabibu kwa Vijana Wanaume (VMMC).

Kiwango cha maambukizi ya VVU katika Mkoa wa Ruvuma kimepungua kwa 1.4 sawa na asilimia 20 kutoka asilimia 7.0 mwaka 2011 kutokana na matokeo ya Utafiti Viashirikia vya UKIMWI na Malaria (THMIS) wa mwaka 2011/2012 hadi asilimia 5.6 mwaka 2016  kwa matokeo ya utafiti matokeo ya Utafiti wa Viashiria vya UKIMWI (THIS) wa mwaka 2016/2017. Kiwango cha maambukizi ya VVU kwa wanawake ni asilimia 6.6 na wanaume ni asilimia 4.5 (THIS 2016/2017).

Katika utekelezaji wa malengo ya kitaifa ya kimkakati ya 95-95-95 (Tisini na Tano TaTu) kwa mwaka 2022, Makadirio ya idadi ya Watu Wanaoishi na Maambukizi ya VVU (WAVIU) katika Mkoa ni 63,088, ambapo wanawake ni 38,716 na wanaume ni 24,372. Kufikia robo ya Julai - Septemba 2022, 95 ya Kwanza; watu 60,862 kati ya WAVIU 63,088 sawa na asilimia 96.5 wamepimwa na kutambua hali zao za maambukizi ya VVU. 95 ya Pili; watu  60,133 kati ya WAVIU 60,862 wanaotambua hali zao za maambukizi ya VVU sawa na asilimia 98.8, wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU (ARVs). Na 95 ya Tatu; watu 57,367 kati ya WAVIU 60,133 wanaotumia dawa za ARV sawa na asilimia 95.4, wamefubaza makali ya VVU. Utekelezaji wa malengo ya Kitaifa ya Kimkakati ya 95-95-95 kwa halmashauri umeainishwa katika jedwali namba 48:


Jedwali Na 48: kuonyesha Utekelezaji wa Malengo ya Kitaifa ya Kimkakati ya 95-95-95 kwa Halmashauri kwa mwaka 2022 kufikia Robo ya Tatu, Julai - Septemba.

Halmashauri

Idadi ya WAVIU 

95 

ya Kwanza

95 

ya Pili

95 

ya Tatu

Maoni

Madaba DC

3,536

112.6

98.5

96.3

Malengo yamefikiwa
Mbinga DC

7,841

105.8

98.8

95.4

Malengo yamefikiwa
Mbinga TC

7,620

88.9

98.9

95.7

95 ya kwanza haijafikiwa
Namtumbo DC

7,533

62.2

98.9

94.8

95 ya kwanza na 95 ya tatu havijafikiwa
Nyasa DC

5,525

122.9

98.5

94.3

95 ya Tatu haijafikiwa
Songea DC

5,730

105.7

98.6

95.6

Malengo yamefikiwa
Songea MC

16,776

99.6

99.6

96.1

Malengo yamefikiwa
Tunduru DC

8,528

88.8

97.5

94.5

95 ya kwanza na 95 ya tatu havijafikiwa
Jumla Mkoa

63,088

96.3

98.8

95.4

Malengo yamefikiwa

Chanzo cha Taarifa: DHIS-2, 10 Desemba, 2022.

Pamoja na mfanikio haya, Mkoa kupitia Timu ya Usimamizi na Uendeshaji wa Huduma za Afya Mkoa (RHMT) imejipanga kuendelea kufanya yafuatayo ili kufikia adhma ya malengo ya 95-95-95 kwa kila mwaka na 0-0-0 (Sifuri Tatu) ifikapo mwaka 2030:

  • Kuimarisha  hudumaza rafiki za upimaji wa VVU miongoni mwa watoto (chini ya miaka 15), vijana balehe (miaka 15 - 19), vijana (miaka 20 - 24), wanaume pamoja na watu wa makundi maalumu yenye hatari kubwa ya kupata maambukizi ya VVU (KVPs),
  • Kuimarisha utoaji wa dawa kinga (PrEP) kwa makundi maalumu pamoja na usambazaji wa mipira ya kinga (kondomu) katika jamii katika maeneo yenye hatari kubwa ya maambukizi ya VVU kama vile nyumba za kulala wageni, baa, sokoni, machimbo, ofisi za umma na binafsi, pamoja na vituo vyote vya kutolea huduma za afya katika halmashauri,
  • Kuimarisha ufuatiliaji kwa wakati wa watoro wa huduma za utumiaji ARVs kupitia watoa huduma za afya na wahudumu ngazi ya jamii katika vituo vya tiba na matunzo ya VVU/UKIMWI (CTCs), hasa kwa makundi ya watoto, vijana balehe, vijana, wanaume na KVPs,
  • Kuimarisha mikakati ya utoaji elimu ya kujikinga na maambukizi ya VVU, ufuasi wa dawa za ARVs pamoja na kuzuia unyanyapaa kwa WAVIU katika jamii kupitia vyombo vya habari, elimu ya VVU/UKIMWI pahali za kazi, mikutano ya hadhara na vituo vya kutolea huduma za afya.

6.3.2 Huduma za Ustawi wa Jamii

6.3.2.1 Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF)

Mkoa wa Ruvuma unatekeleza Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa kwa mujibu wa Waraka Na.1 wa Mwaka 2018 wa Maboresho ya Mfuko wa Afya ya Jamii ambao umeleta tija kubwa kwa wananchi katika kupata huduma za afya za uhakika. Hadi kufikia 30 Novemba, 2022 jumla ya kaya 25,745 (7.4%) zimeandikishwa kwenye Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa (iCHF).

Jedwali Na.49: Hali ya iCHF Mkoa wa Ruvuma hadi 30 Novemba, 2022

NA
HALMASHAURI
IDADI YA KAYA
KAYA ZILIZOSAJILIWA
ASILIMIA
MAKUSANYO
1
MADABA DC
12,250
1,636
13.4%

49,080,000.00

2
MBINGA DC
57,738
4,965
8.5%

148,950,000.00

3
TUNDURU DC
82,129
6,659
8.1%

199,770,000.00

4
MBINGA TC
33,256
2,579
7.8%

77,370,000.00

5
NAMTUMBO DC
45,856
3,488
7.6%

104,640,000.00

6
SONGEA DC
33,933
2,510
7.4%

75,300,000.00

7
SONGEA MC
57,640
2,549
4.4%

76,470,000.00

8
NYASA DC
37,367
1,359
3.6%

40,770,000.00


JUMLA
360,169
25,745
7.4%

772,350,000.00

6.3.2.2 Usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya Miaka Mitano (U5BR) 

Mkoa unaendelea kutekelezwa mpango wa usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano bure ulioanza Machi, 2020 katika Halmashauri zote za Mkoa wa Ruvuma. Usajili na utoaji vyeti hufanywa na Wauguzi kwenye vituo vyote vya huduma za afya vinavyotoa huduma za afya ya mama na mtoto.

Lengo la Mkoa wa Ruvuma ni kusajili na kuwapatia vyeti watoto 242,140, ambapo hadi tarehe 30 Novemba, 2022 Mkoa umesajili na kutoa vyeti kwa watoto 242,083 (99.9%).

 

 

6.3.3 Huduma za Lishe

Katika kuendelea na kupambana na tatizo la utapiamlo nchini hususani udumavu (asilimia 41, TNNS 2018), Mkoa wa Ruvuma unatekeleza viashiria mbalimbali vilivyoainishwa katika mkataba wa Lishe ulioingiwa baina ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma. Utekelezaji wa mkataba kwa mwaka 2020/2021 Mkoa wa Ruvuma ulikuwa ni mshindi wa pili kitaifa na mwaka 2021/2022 Mkoa umeshika nafasi ya 4 Kitaifa. Matokeo haya kwa kiasi kikubwa yametokana na; -

Matumizi ya Kifungu/Lengo Y (Objective Y) katika kutekeleza shughuli zisizo za Lishe.

Kutumia vifungu/malengo mengine (objectives) kutekeleza shughuli za Lishe.

Haya yote yaliyotajwa hapo juu yamesababisha Mkoa kutofanya vizuri katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe katika mwaka wa fedha 2021/2022. Hivyo, ili kutekeleza Mkataba wa Lishe kwa Kiwango kinachotakiwa tunapendekeza yafuatayo; -

Waweka hazina wa Halmashauri wahakikishe vifungu vya Lishe (Objective Y expenditure codes) vinatumika kulipia shughuli za lishe tu

Maafisa Mipango wahakikishe vifungu vya Lishe vinatumika kupanga shughuli za Lishe tu

Maafisa Lishe wa ainishe vifungu sahihi vya shughuli anayokwenda kutekeleza.

Wakaguzi wa ndani ya Halmashauri wahakikishe wanafanya uhakiki wa fedha za lishe kila robo mwaka ili kubaini changamoto mapema na kuzitatua kwa wakati.

Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Mkoa kupitia Halmashauri zake umeendelea kutekeleza afua mbalimbali ikiwemo utengaji na utoaji wa fedha kwa ajili kutekeleza afua za lishe, ambapo jumla ya TZS. 355,274,918.3 zimepangwa na hadi kufikia Novemba, 2022 jumla ya TZS. 122,852,599 sawa na asilimia 34.6 tu zimetolewa kutekeleza afua za lishe katika Halmashauri kama inavyoonesha katika jedwali namba 50.

Jedwali Na. 50: Matumizi ya fedha zilizopangwa kutekeleza afua za lishe kwa Halmashauri katika mwaka wa fedha 2022/2023


NA
HALMASHAURI

FEDHA ILIYOTUMIKA JULAI - NOVEMBA, 2022 IKILINGANISHWA NA FEDHA ILIYOPANGWA MWAKA  2022/2023

KIASI CHA FEDHA KILICHOPANGWA KWA MTOTO (PER CAPITA PLANNED) FY 2022/2023

KILICHOPANGWA

KILICHOTUMIKA HADI NOVEMBA, 2022

%

IDADI YA WATOTO

TZS

1
SONGEA MC

39,860,000

24,404,000

61.2

32216

1237

2
MBINGA TC

23,971,068

7,526,000

31.4

20961

1144

3
SONGEA DC

38,729,712

6,570,000

17.0

21396

1810

4
MBINGA DC

92,711,750

37,140,000

40.1

41575

2230

5
TUNDURU DC

71,204,134

21,254,600

29.9

47833

1489

6
NAMTUMBO DC

39,432,000

  5,070,000

12.9

36712

1074

7
NYASA DC

23,823,206

11,744,000

49.3

27023

882

8
MADABA DC

25,543,048.3

9,143,999

35.8

7684

3324

JUMLA KUU

355,274,918.3

122,852,599

34.6

235400

1509


NB: - Halmashauri saba (7) ziliweza kupanga kwa kufuata kigezo cha kima cha chini cha TZS. 1000 kwa kila mtoto chini ya miaka mitano, isipokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa ambayo ina jumla ya Watoto wenye umri chini ya miaka mitano 27023 lakini wamepanga TZS. 23,823,206 badala ya kima cha chini cha TZS. 27,023,000. Athari ya hii itafanya Halmashauri kutofikia matumizi ya kima cha chini cha TZS. 1000 wakati wa tathmini na mwisho wa siku itaathiri matokea ya Mkoa Kitaifa.

Ushauri: Tunapoelekea kwenye re–allocation Halmashauri ihakikishe inafanya marekebisho ili kuepuka hii changamoto kama iliyojitokeza mwaka wa fedha 2021/2022.

 

6.3.3.1 Mambo yanayosababisha lishe duni ni: -

Ulaji duni wa chakula unaotokana na kula milo michache na kiasi kisichotosheleza mahitaji ya virutubishi mwilini, hii pia hujumuisha kutowanyonyesha watoto ipasavyo.

Magonjwa ya mara kwa mara yanayoondoa hamu ya kula na, kusababisha ufyonzaji duni wa virutubishi na huongeza mahitaji ya virutubishi mwilini.

Matumizi mabaya ya chakula mfano kuuza chakula chote, kutumia nafaka kutengenezea pombe nk.

Utayarishaji mbaya wa chakula unaopoteza virutubishi kama kuosha mboga za majani baada ya kukatakata.

Upungufu katika matunzo ya makundi maalumu (watoto wadogo, wanawake wajawazito na wanaonyonyesha, wazee na wagonjwa) Makundi haya yanahitaji matunzo na huduma muhimu za kiafya kama vile chanjo, kupata vidonge vya nyongeza, kutibu maradhi na huduma za kilishe.

Utapiamlo huathiri afya, uzalishaji mali na maendeleo katika jamii. Athari hizi hujitokeza katika hali ya kuchelewa kwa hatua za ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili, kuongezeka kwa magonjwa na vifo vya watoto, kupungua kwa kinga mwili na kupungua kwa uwezo wa kufanya kazi za uzalishaji mali.

Hivyo, katika kuhakikisha jamii inaondokana na tatizo hili la lishe Halmashauri na Mkoa ni muhimu kuendelea kuelekeza nguvu katika kusimamia utekelezaji wa mikataba ya lishe ngazi ya Halmashauri, kata na vijiji / Mitaa ili jamii iweze:- 

kubadili tabia na kuzingatia ulaji unaofaa.

Kupata elimu sahihi ya lishe kwa kupitia njia mbalimbali kama vyombo vya habari vilivyopo, ngoma za asili, viongozi wa dini na kimila.

Kupata elimu sahihi ya lishe katika kipindi cha siku 1000 za uhai wa mtoto (yaani toka mimba ilipotungwa hadi mtoto anapofikisha umri wa miaka 2) –

Kuimarisha maadhimisho ya siku za afya na Lishe ya Kijiji zinazofanyika kila baada ya miezi mitatu.

Mkoa na Halmashauri kuhakikisha fedha inayotengwa kwa shughuli za lishe inatolewa na kufanya shughuli za lishe kama zilivyotengwa.

Mkoa na Halmashauri kuendelea kufanya usimamizi shirikishi ili kuweza kutambua changamoto zinazojitokeza kwa wakati na kuzitafutia ufumbuzi.


Matangazo

  • JARIDA la RS Ruvuma toleo la Aprili 2025 April 30, 2025
  • VIGEZO vya kupata leseni ya biashara September 30, 2025
  • FURSA za uwekezaji mkoani Ruvuma June 30, 2025
  • ORODHA ya nyumba za kulala wageni mkoani Ruvuma December 31, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • JARIDA la RS RUVUMA toleo maalum la Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Ruvuma

    May 18, 2025
  • MAKABIDHIANO mwenge wa Uhuru kati ya Mkoa wa Ruvuma na Mtwara.Ruvuma yaandika historia

    May 17, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waridhia miradi yote Tunduru

    May 16, 2025
  • MWENGE wa Uhuru waangaza Namtumbo

    May 15, 2025
  • Tazama zote

Video

HAKIKISHA unafika kanisa la Peramiho-Rais Samia
Video Zaidi

Viungio vya Haraka

  • Songea Municipal Council
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Madaba District Council
  • Nyasa District Council
  • Namtumbo Dictrict Council
  • Mbinga Town Council
  • Songea District Council

Tovuti Muhimu

  • Utumishi Portal
  • Government Portal
  • Tamisemi
  • Tanzania Revenue Authority

Waliotembelea Kijiografia

world map hits counter

Waliotembelea

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Regional Commissioner Office

    Anuwani: 1 TUNDURU ROAD, 57180 S.L.P 74,SONGEA, RUVUMA.

    Simu: 0252602256

    Simu ya Mkononi: KERO PIGA 0800110174

    Barua Pepe: ras.ruvuma@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Majibu ya haraka
    • Ramani ya Mahala
    • Huduma

Copyright ©2017 Ruvuma . All rights reserved.